Anayejua free VPN ya kweli anisaidie

Anayejua free VPN ya kweli anisaidie

Ndio maana nashangaa natumia S8+ ya t mobile nashangaa 3g hamna.....

Kibongo bongo nini faida na hasara za kukosa 3g kwenye t mobile.?
kama unaishi dar au majiji mengine kama Arusha, Tanga, Mwanza Etc na unapata 4g hutaona hasara sababu 4g ni nzuri kushinda 3g.

ila siku ukienda mikoa au wilaya zisizo na 4g utapata speed ya internet ya konokono, sababu itakuwa ni E tu.
 
Natamani sana kujua mambo haya lakini huwa sielewi hata nikifuatilia, sijui nitajuaje kuya kamilisha humu kichwani mwangu.

Swali langu moja, yani unakuwa hujazi hata data/ bila hata MB kwenye simu.

Juzi nilikerwa sana nilipo wapigia Halotel kwa mambo yangu binafsi, wakaniambia aina ya simu ninayo tumia, mahali nilipo,
Kiukweli nili kasirika sanaaaa, kw kitendo kile cha kunijua nilipo.


Je hyo vpn haya mambo yote itaweza zuia nisijulikane kabisa maaan dahhh nilipatw na hasira sannnnaaaaAaaaaaaa
 
Daaah mm huwa natumia hizi softwre, ila kama kuna njia ya kunielewesha namna ya kutumia open vpn na kuweka hizo config, nitashukuru mno, maana huku mambo yamekuwa balaa. Software fungafunga


Habari.
Kutokana na ujuzi mdogo nilionao kaka, Open vpn inanisaidia kuniunganisha na virtual private network ya ofisini (vpn) nikiwa popote pale duniani through Tunneling protocol, Kwa mimi huwa natumia linux operating system (ubuntu), lakin waweza kuitumia openvpn hata ukiwa na windows. Ili iwe rahisi kwako ni vizuri ukawa na vpn server ambayo uta install openvpn upande wa server na uta install tena openvpn upande wa client.
Kwa mimi nimetengeneza kwanza vpn server ambayo nayo nimetumia ubuntu server 16.04 lts na nime install openvpn server, ili uweze kutumia lazma ufanye editing ya file linaitwa server.conf liko kwenye upande wa server /etc/openvpn/server.conf hii itakulazimu ulifanyie editing kidogo kwenye text editor kama vile nano , vim or gedit inategemea na wewe unatumia text editor gan. Sorry kaka naelezea kwa ufupi kidogo but i'm sure ukipitia tutorials za youtube na ukifanya practice utanielewa tu.
Then itakubidi u generate keys na certificates kwa ajili ya authentication na uzi copy kwenye client machine.

Then itakubidi uingie tena kwenye client computer ui install tena openvpn na uingie kwenye /etc/openvpn/client.conf uedit tena configuration za client huwa tukimaliza mara nyingi extension yake inakuwa ni .ovpn

Then utarestart service command zake huwa systemctl restart openvpn kitu kama hicho.
Kwa ubuntu ni lazma ui import vpn onfiguration kwenye network manager
Ili uweze kupata ile tun0 interface kwa ajili ya vpn.

Thanks.
 
Natamani sana kujua mambo haya lakini huwa sielewi hata nikifuatilia, sijui nitajuaje kuya kamilisha humu kichwani mwangu.

Swali langu moja, yani unakuwa hujazi hata data/ bila hata MB kwenye simu.

Juzi nilikerwa sana nilipo wapigia Halotel kwa mambo yangu binafsi, wakaniambia aina ya simu ninayo tumia, mahali nilipo,
Kiukweli nili kasirika sanaaaa, kw kitendo kile cha kunijua nilipo.


Je hyo vpn haya mambo yote itaweza zuia nisijulikane kabisa maaan dahhh nilipatw na hasira sannnnaaaaAaaaaaaa
vpn haiwezi kuzuia isp wako asijue mahala ulipo sababu hio ip yenyewe ya kuingilia internet anakupa yeye. ni kama unaomba ushauri kwa watu jinsi gani utamfanya baba mwenye nyumba wako asijue mahala ulipopanga. ila itakusaidia isp asijue unafanya nini.
 
Mh nahisi hapa nimekosea njia,sorry wakuu napita tu,Giza nene kwangu.
 
vpn haiwezi kuzuia isp wako asijue mahala ulipo sababu hio ip yenyewe ya kuingilia internet anakupa yeye. ni kama unaomba ushauri kwa watu jinsi gani utamfanya baba mwenye nyumba wako asijue mahala ulipopanga. ila itakusaidia isp asijue unafanya nini.
Mkuu hivi BACK GLASS Cover ya Simu ya Samsung unaweza kubadilisha au Baada ya Back Glass kuna Back cover nyingine.
 
vpn haiwezi kuzuia isp wako asijue mahala ulipo sababu hio ip yenyewe ya kuingilia internet anakupa yeye. ni kama unaomba ushauri kwa watu jinsi gani utamfanya baba mwenye nyumba wako asijue mahala ulipopanga. ila itakusaidia isp asijue unafanya nini.


Kama hajui unafanya nini kwa nini asumbuke kufuatilia uko wapi?
 
Kwa hiyo upo nchi ambayo sites ziko blocked? Upo china au? Hapo utapata wakati mgumu sana maana wachina wanablock VPN actively yaani ikitokea VPN mpya wanaipiga nyundo kwenye firewall yao.

Si kweli kwamba VPN hazifanyi kazi China.

Study ya TechRadar.Com ya mwezi huu inaonyesha zipo zinapiga kazi freshi.
 
kwa hiyo mkuu ina maana kwa kutumia vpn unaweza kutembelea website zilizofungwa?
Ndiyo maana yake hata yule malaika wa kichaa akishuka kufunga mitandao ya kijamii kama jf unaweza kuifungua Kwa kutumia vpn
 
c7bae573063a87baf57c5404300f7ef3.jpg
Nimefanikisha kuconnect kwa simu
Tutumie link ya kuipata maana, ukiingia google play zipo kibao hata hatuelewi ipi inafanya kazi
 
Kama hajui unafanya nini kwa nini asumbuke kufuatilia uko wapi?
kwani mitandao ya simu inahudumia internet tu? huku kwetu Tanga kulikuwa na kifurushi cha Tigo cha stand. mpaka uende stand ya mabasi ndio kinaunga. miaka kadhaa iliopita kulikuwa hakuna line za chuo, mpaka uwe eneo la chuo ndio kifurushi cha chuo unajiunga. mtu anapoiba simu au kufanya uhalifu mtandao wa simu unamuona alipo na kuwezesha kukamatwa etc,

kuna mambo mengi tu ambayo mtandao wa simu wanatumia mahali ulipo kukamilisha.
 
Nawapa trick ambayo ni ngumu zaidi ila inalipa zaidi ukifanikiwa kufuata process nzima. Itachukua muda na kama huna ujuzi wa computer itakusumbua sana ila its worth it.

VPN Services hua si za kuziamini, ni bora kua na ya kwako mwenyewe, that way unajua fika kua all traffic inapita kwako tu na si kwa mtu mwingine. Sasa kua na VPN server yako mwenyewe unafanyeje?

1. Register Amazon AWS. Hapa ukijiunga wanakupa mwaka mzima bure kabisa, alafu mwaka unaofuata unapewa 700 hours per month ambayo ni basically mwezi mzima kama unatumia micro instance.
2. Ukisharegister, umepata account, chagua region unayotaka VPN yako iwe, mfano kama unataka US, then chagua US region sehemu yoyote.
3. Tengeneza micro instance, hii hua ina 700hours free usage kila mwezi. Kumbuka una mwaka mzima wa bure kwanza.
Sasa cha muhimu, ukiwa unatengeneza instance, inatakiwa utumie image ya OpenVPN. Hii image ukiwasha instance inakua na openvpn setup moja kwa moja tayari kuweza kutumia.
4. Chukua IP address ya instance yako, weka kwenye browser yako alafu ifungue. Nenda ufanye settings
5. Weka username na password, tengeneza account mpya, unaweza kuitumia wewe, ndugu zako pia bila shida.
6. Download OpenVPN kwenye computer na simu zako zote
7. Download profile kutoka kwenye instance yako
8. Tumia VPN yako mwenyewe, full protected na bure mwaka wa kwanza mzima, mwaka wa pili unaweza jiunga upya kupata bure mwaka mwingine kama una roho ngumu kulipa au kama hauna shida unalipia kama mimi $5 kwa mwezi bei ndogo sana.
 
Back
Top Bottom