Anaomba second chance

Anaomba second chance

tang'ana

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2015
Posts
12,054
Reaction score
16,509
Amani ya Bwana iwe nanyi enyi watu wa Mungu!
basi tukiwa bado tunatafakari kauli ya mheshimiwa Trump kuhusu bara la Africa na watu wake,ningependa kushare nanyi huu mkasa wangu.
ways back kama miaka minne iliyopita,nilikua nadate binti flani hivi ambae kwa kipindi hicho ndio alikua kamaliza form six,well naweza kukiri mwanzo alionyesha mapenzi ya hali ya juu sana kwangu mpaka nikawa nishamwekea malengo ya kumuoa..akachaguliwa kwenda chuo huko mzumbe na mapenzi yalizidi kunoga mpaka anaingia mwaka wa pili ndio mambo yakaanza kuchange..ikafikia point kila jema nililokua namfanyia kwake ilikua kero,akaanza kuniomba vitu ambavyo kwa wakati huo mimi sikuweza kuvimudu asee..baada ya kumfanyia intelijensia kwa mara ya kwanza sikugundua kitu chochote,nikabadili mbinu za kumspy sikugundua kitu pia na wakati huo huo ndio vituko vyake ndio vikawa vinazidi...so kama ilivyo ada kwangu mie sinaga muda wa kupigizana kelele na wanawake au kubembelezana na binadamu mwenzangu..nikaamua kumchunia tu yule manzi,nae bahati nzuri akaamua kuuchuna..sasa cha kushangaza leo kaanza kunitafuta kwa fujo..kanipigia tumeongea mengi ananiambia eti sababu za kipindi kile kuwa vile ulikua ni utoto unamsumbua so kaniomba msamaha na anaomba nimpe second chance katika maisha yake ili tuweze kuendeleza pale tulipoishia.
Nimemtafakari sana leo,ofcourse naelewa huko alikokua atakua katendwa so kaamua kuja kujificha kwa boya wake(mimi) lakini pia nimefanya cost benefit analysis nimeangalia mazuri yake aliyonitendea ni mengi kuliko mabaya hivyo uwezekanao wa kupewa hiyo second chance upo,but kabla sijatoa go ahead ya mawazo yangu nikaamua niwashirikishe na nyie watu Mungu ili nisikie mnatoa mawazo gani hapa.
Asanteni
NB; ukijisikia kutukana wewe tukana tu maana Tnzania ni nchi huru but nakuonya you are not free to that extent,Mods wako kazini muda wote.
 
Huyo amekuona wewe ni pipa lake la taka, amerejesha uchafu baada ya kuwa ameshatumika vya kutosha..

Miaka minne ndo aje sasa ivi? Shtuka wewe
 
ikiwezekana msainishe kitu kinachoitwa relationship agreement
ukitaka muongozo nitakupa

once nilimsainisha mtu alivyokiuka tulibwagana
ebu nipe huo muongozo mkuu
 
Msamehe tuu kama kweli wampenda ila mpende kwa akili kubwa sana
 
05191f654f8db0946288e8bdb329d37c0a4e55-wm.jpg
 
Watu wameto..mbaaaa ndo inaletwa hata ivyo makombo kula tu
 
Kwa thread yako unaonesha bado unamuhitaji, fanya vile moyo wako unataka ila kumbuka. hawa viumbe uwa hawatabirki.
 
Bro alikutupa mara ya kwanza. Usitegemee hatokutupa mara ya pili. Sio sahihi kwako. Tafuta mwanamke mwenye msimamo na maisha yake. Wanawake wapo wazuri wenye heshima. Ila kwa ninavyo relate text yako inaonyesha kuwa bado una mashaka nae lakini nia yako ni kumgegeda tena mtoto wa watu ili u revenge. Ila kama huna maana hiyo basi kuwa makini sana na uende kwa akili nyingi
 
Mleta mada naona unajifanya Ally Kiba kula makombo. Huyu demu alikutema kipindi hicho kwa sababu alikuwa na mtu anayempa support ya gegedo na matumizi yake binafsi na akakuona wewe sawa na mavi na ndiyo maana alikuchunia kwa sababu hakuona umuhimu wa kuwa nawe. Na kama ujuavyo, wanawake vicheche siku zote huishia pabaya (wanatemwa baada ya kuchezewa). Huyo demu baada ya kuchanganya akili huku na kule na kuona giza, akahamua kuja kuomba msamaha kwako ili umrudie na aanze kukuchuna tena kabla ya kupata mwingine. Achana naye, huyo hakufai....waswahili wanasema nyota njema uonekana alfajiri, na huyu demu alishakuonyesha dalili.
 
ikiwezekana msainishe kitu kinachoitwa relationship agreement
ukitaka muongozo nitakupa

once nilimsainisha mtu alivyokiuka tulibwagana
Naihitaji hiyo agreement mkuu nisainishe mtu
 
Back
Top Bottom