Elections 2010 Ananilea Nkya (TAMWA) very good

QUALITY

JF-Expert Member
Sep 27, 2010
853
115
Ndugu zangu wote walioangalia ITV jana, waliona jinsi kiongozi wa TAMWA, Ananilea Nkya alivyolaani kitendo cha JWTZ kujiingiza katika masuala ya CCM. Hivi ndivyo inavyopaswa kuwa sababu hasa wote ambao wanajihusisha na masuala ya elimu ya uraia semeni wazi. Kama kuna anayeweza kuingiza ile picha ya mama Ananilea Nkya, itakuwa vyema kwa ambao hawakuona. karibuni jamvini
 
Huwa na mu-admire sana mama huyu kwa misimamo yake. Hasa yale matangazo ya TV kuhusu rushwa katika uchaguzi, kwani huwa yanawachoma sana CCM waliozea kutoa rushwa.
 
Mama mzalendo sana huyu! Kwanza akiongelea joambo unaona kabisa anauchungu. Mungu akutie moyo mama
 
Ivi mlimsikia JK aliahidi kuwa uongozi ujao ni 50 kwa 50 kati ya wanaume na wanawake
 
kwa bahati mbaya JK hana nafasi tena ya kuunda serikali. CHADEMA ikishinda, nafasi za kupeana bila maarifa zitafutwa ili tupate hela za elimu na afya bure. Mungu ambariki kile anayepinga mafisadi, Amen:A S 13:
 
ni kweli kabisa mama ameongea vizuri lakini je, amiri jeshi mkuu ana maoni gani kuhusu vijana wake waliamua na wao kuingia kwenye siasa wakiwa wamevaa combat zao??

binafsi sidhani kama kuna mtanzania anahitaji kuhutubiwa na mnadhimu mkuu wa jeshi kuhusu kazi ya jeshi kulinda amani... nadhani JWTZ waliamua kutumia gobore kuua nzi

je, kauli ya mama nkya ina impact yoyote kwa amiri jeshi mkuu na jeshi lake?? au ndio watamuona na yeye katuni tu?
 
Back
Top Bottom