Ananiganda sana mpaka sina raha

Ananiganda sana mpaka sina raha

martinezstavo

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2020
Posts
735
Reaction score
1,560
Wakuu mwanzoni kwa mwaka huu nilienda kutafuta kibarua cha kijishkiza ili siku ziende huku tukisubili kama t unaweza kubahatika kufanya shughuri tulizosomea niilifika kwenye kampuni moja kubwa sana nkapata kibarua cha muda kweli mule ndani kulikuwa kuna pisi moja miyeyusho sana kwa vitendo vyake yaani ni mtu anaenata sana as if hafi ukizingatia na kitengo alichopo basi tabu tupu.

Huyu bibie kunasiku alinikuta sijakamilika kikazi basi akanijia juu sana mpaka kufikia hatua ya kuniitia walinzi wanitoe nje ya geti kitu kilichopelekea kupoteza kibarua.

Siku kadhaa mbele niliibuka kufatilia baadh ya malipo yangu nikakutana nae kwenye bajaji nilimsalimu alivoitikia nikajaribu kumkumbusha kama ananikumbuka akadai hanikumbuki nkaona sio kesi nka jaribu kumuweka sawa mpaka pale tulipobadilishana namba za simu kwa lengo la kushughurikia swala langu ili niludi kazini.

Siku zkapita tukiwasiliana kwa salamu za hapa na pale story kidogo mwisho tukazoeana na kujikuta tunaanzisha mahusiano bila kutegemea kitu kilichonipelekea kuona kuwa ni fursa yangu ya kulipiza kisasi kwa kuwa sikuwa nampenda kiukweli licha ya watu kupagawa na jinsi alivyoumbika kuanzia sura mpaka umbo.

Kwa Bahati mbaya nilimuonesha nnapoishi mapema sana na kula tunda mala kadhaa kitu kilichopelekea kupata ujauzito japokuwa nilikuwa natamani nimjaze kisha nihame kabisa mji lakini nilisitisha baada ya baadhi ya memba humu kunipa ushauri.

Sasa huyu bidada anaujauzito wa miezi miwili kasoro, mwanaume sina jambo mfukoni, hapajui kwetu wala ndugu z angu hawamtambui, najulikana kwa mama ake na ndugu wachache kwa picha tu, sina malengo nae kwa sasa kwa kuwa sijajipanga japokuwa yeye anauwezo wa kumhudumia mtoto na kwao kiukweli sio wanyonge wanajiweza sana tu.

Huyu mwanamke this time around anajikuta anajiweka Karibu sana na Mimi richa ya mimi kumuweka wazi baadhi ya mambo na kuonesha kuchukia waziwazi na kuraani kitendo alichonifanyia pamoja na hali yangu ya maisha kuwa ngumu.

Wakuu kwa sasa sielewi nawezaje unakubaliana na hali na kuishi bila kinyongo na huyu mwanamke, Mda mwingine nawish hata nimkimbie tu yaani hichi kipindi bira jamii forums nahisi ningekuwa naokota makopo

========
Mwendelezo: Anzeni vikao vya Send-off wanajamvi
 
Mkuu tuliza , akili yote mitihaninkikubwa tulia swala la kulipa kisasi kwa sasa futa akilini huyo ni mzazi mwenzako sasa wewe focus katika kupata kazi kwingine isiwe pale
yaani mkuu sitamani hata kumuona while kazidisha vitu ambavyo alikuwa hafanyi mwanzo kama kuja kwangu kupika vyakula nnavovipenda, kuniwezesha pesa ndogondogo ambazo sifurahii hata kuwa Nazo naona kama chochote anachofanya ni haramu
 
Hizo kumbumkumbuke ulizohifadhi kichwani ndizo zinakutesa na kukufanya umchukie huyo bibie, sahau yaliyopita na upambanie yajayo...pambana kwaajili ya mwanao atakaezaliwa na kumkimbia siyo suluhisho Bali suluhisho ni wewe kuwa na uwezo wa kumuhudumia yeye na mtoto atakaezaliwa, watu tuna historia mbaya za jinsi tulivyokutana na wenza wetu ila yote tulisahau na tunaishi vizuri tu na yote yaliyopita tunakumbushana na kucheka Kama utani siku zinasonga.
 
Nadhani tatizo hapa ni wewe mkuu. Hebu jichunguze vizuri. Wewe mwenyewe unajipenda, kujithamini na kujiamini? Ukikosewa huwa mwepesi wa kusamehe? Yaonekana kama vile kuna jambo la kuumiza sana lilishawahi kukutokea maishani na jambo hilo liliacha alama hasi ya kudumu ambayo mpaka leo haijafutika moyoni mwako.

Sioni kama kitendo alichofanya huyo binti hakisameheki (na inavyoonekana wewe ndiyo ulikuwa na makosa). Na maadam sasa ameonekana kukupenda na kukujali; na kama kweli kaamua kutulia na kuanzisha familia itakuwa busara sana kama utamsamehe kwa kosa alilofanya na mkaanzisha familia pamoja. Inaonekana ni mwanamke mwema na kwa vile mmeshashea damu sasa, hata ukimkimbia haitasaidia cho chote. Sana sana utakuwa unakimbia kivuli chako tu na huko utakakokimbilia mambo yatakuwa yale yale; na utakuja kupenda usipopendeka uumizwe mpaka maji uyaite mma.

Una bahati sana japo hujui....na kwa wengi wetu bahati huwa haiji mara mbili hasa kwenye hii ishu ya mapenzi.....
 
Mada zenu humu kila mtu kaumbika, ni Mrembo ana umbo sijawahi ona uzi hata mmeandika vinginevyo
Urembo mara nyingi umo machoni mwa mtazamaji bro. Mtu atakwambia kapata pisi kali lakini we ukija kuiona hiyo pisi unaiona ya kawaida sana na sometimes hata haistahili cheo cha pisi kali kabisa...

Lakini pia wakati mwingine ni ego tu na kujimwambafai. Pisi kali ajabu na yenye hadhi kazini imeangukia kwa njemba aliyeifokea mpaka ikafukuzwa kazi...it makes a nice story hasa kama itaishia na "...and they lived happily ever after"
 
Urembo mara nyingi umo machoni mwa mtazamaji bro. Mtu atakwambia kapata pisi kali lakini we ukija kuiona hiyo pisi unaiona ya kawaida sana na sometimes hata haistahili cheo cha pisi kali kabisa...

Lakini pia wakati mwingine ni ego tu na kujimwambafai. Pisi kali ajabu na yenye hadhi kazini imeangukia kwa njemba aliyeifokea mpaka ikafukuzwa kazi...it makes a nice story hasa kama itaishia na "...and they lived happily ever after"
umeongea vizuri mkuu
 
Nadhani tatizo hapa ni wewe mkuu. Hebu jichunguze vizuri. Wewe mwenyewe unajipenda, kujithamini na kujiamini? Ukikosewa huwa mwepesi wa kusamehe? Yaonekana kama vile kuna jambo la kuumiza sana lilishawahi kukutokea maishani na jambo hilo liliacha alama ya kuumiza sana ambayo mpaka leo haijafutika...

Sioni kama kitendo alichofanya huyo binti hakisameheki (na inavyoonekana wewe ndiyo ulikuwa na makosa). Na maadam sasa ameonekana kukupenda na kukujali; na kama kweli kaamua kutulia na kuanzisha familia itakuwa busara sana kama utamsamehe kwa kosa alilofanya na mkaanzisha familia pamoja. Inaonekana ni mwanamke mwema na kwa vile mmeshashea damu sasa, hata ukimkimbia haitasaidia cho chote. Sana sana utakuwa unakimbia kivuli chako tu na huko utakakokimbilia mambo yatakuwa yale yale; na utakuja kupenda usipopendeka uumizwe mpaka maji uyaite mma.
Hutaki anayekuganda?....angalia usije mpata utakayemganda wewe
 
1599765549221.png
 
Hutaki anayekuganda?....angalia usije mpata utakayemganda wewe
Mkuu, mimi siyo mhusika wa hii hadithi.

Siku hizi kupata anayekuganda (tena pisi kali) ni bahati sana halafu yeye anaichezea. Ngoja naye Karma itakapobadili kibao agande asipotakiwa ndiyo atajua wahenga walimaanisha nini waliposema mkuki kwa nguruwe....
 
Back
Top Bottom