mwanafyale
JF-Expert Member
- Sep 27, 2010
- 1,641
- 539
Kuna rafiki yangu wa karibu, mwanamke (sio gf wangu) amekutana na mtu online na kuanzisha mahusiano. Kwa maelezo yake mahusiano hayo yana Kama miezi miwili hivi, na jamaa anaonekana kafika kwa huyo mdada. Mwezi mmoja baada ya kukutana, jamaa akaingizana Dar na wakakakutana USO kwa macho. Jamaa ni daktari bingwa huko majuu. Baada ya huyo jamaa kuondoka akiwa amepata pochi la uhakika na ki-IST kamuachia, huko aliko sasa anamlazimisha wafanye mapenzi online. Mdada hajazoea na jamaa anamwambia hawezi kuvumilia mpaka watakapoonana, vinginevyo amruhusu awe a natafuta mtu wa chapuchapu kumaliza hamu yake. Mdada kachanganyikiwa, ameniambia ushauri na mie nimeshindwa ni shauri nini. Msaada bandugu