The Burning Spear
JF-Expert Member
- Dec 23, 2011
- 8,551
- 20,346
Anaandika Askofu BENSON BAGONZA (PhD)
UCHURO WA TAIFA: Tuzinduke.
Nianze kwa kutoa salaam zangu za pole kwa familia ya hayati Job Ndugai. Pole kwa Ofisi nzima ya Bunge (Kupitia Katibu wa Bunge). Pole kwa Mh. Rais. Pole zaidi kwa taifa letu kutokana na msiba huu.
Kuna kitu kisicho cha kawaida katika taifa letu. Dalili zake ni hizi;
1. Akifa Mwana siasa kutoka chama tawala, watu wanashangilia na kukejeli.
2. Akifa kiongozi wa kitaifa au jamaa yake, watu wanashangilia.
3. Watumishi wa serikali kutoka idara fulani fulani zinazogusa masuala ya haki za watu, wakipata janga lolote, watu wanashangilia.
4. Watu wasio serikalini au kwenye siasa lakini wana ukaribu na wana siasa na viongozi wa serikali, wakipata majanga au misiba, watu wanashangilia.
5. Viongozi wa dini, wa ukweli na wa uwongo (Mungu ajua), wakiwatabiria mabaya wanasiasa, wanaaminika. Wakiwatabiria mazuri, wanatukanwa. Mungu amemilikishwa kwa watu wenye chuki dhidi ya viongozi.
HUU NI UCHURO WA TAIFA. HAUKUBALIKI.
Kwa nini tumefika hapa?
a. Mifumo ya utoaji haki katika taifa imefunikwa na giza linalokatisha tamaa wanyonge. Kimbilio lao limekuwa ni Mungu wa visasi. Shida zimewasahaulisha Mungu
wa Upendo.
b. Watu maskini na wanyonge wana hasira inayogeuka kuwa ukatili. Wanajiona yatima wasio na mtetezi. Adui yao mkuu siyo umaskini, ujinga na maradhi bali watawala, rafiki za watawala na ndugu wa watawala. Ukisikia wanasema “wao wana fedha, sisi tuna Mungu” elewa huyo Mungu ni silaha ya kuwaua watawala. Tuzinduke.
c. Tulifuta ukabila, udini, ueneo, na ubaguzi wa rangi. Bila kushtuka au kukubali kushtuliwa, tumeunda matabaka mawili makubwa: Watawala na watawaliwa. Moja lina uhakika wa kuishi na kutawala, jingine halina uhakika wa kuishi, kutawala, ajira, na usalama. Ndani ya matabaka hayo, yameibuka matabaka mengine madogo madogo yanayogombania makombo. Tabaka moja linasema “utanifanya nini?” Na jingine linasema “namwachia Mungu”.
Kutokana na kiwango cha UCHURO WA TAIFA tulichofikia, hakuna mtu au kundi lililo salama. Mkosoaji, chawa, na vizalia vyao, hawako salama. Ghadhabu ya watu maskini inawaka vifuani huku viburi na jeuri ya wenye madaraka ikitamalaki. Tushtuke.
TUSIPUUZE WITO WA KURUDI MEZANI
TUHARAKISHE MJADALA WA KITAIFA
HAKUNA HEKIMA ILIYOCHELEWA..
C&P
UCHURO WA TAIFA: Tuzinduke.
Nianze kwa kutoa salaam zangu za pole kwa familia ya hayati Job Ndugai. Pole kwa Ofisi nzima ya Bunge (Kupitia Katibu wa Bunge). Pole kwa Mh. Rais. Pole zaidi kwa taifa letu kutokana na msiba huu.
Kuna kitu kisicho cha kawaida katika taifa letu. Dalili zake ni hizi;
1. Akifa Mwana siasa kutoka chama tawala, watu wanashangilia na kukejeli.
2. Akifa kiongozi wa kitaifa au jamaa yake, watu wanashangilia.
3. Watumishi wa serikali kutoka idara fulani fulani zinazogusa masuala ya haki za watu, wakipata janga lolote, watu wanashangilia.
4. Watu wasio serikalini au kwenye siasa lakini wana ukaribu na wana siasa na viongozi wa serikali, wakipata majanga au misiba, watu wanashangilia.
5. Viongozi wa dini, wa ukweli na wa uwongo (Mungu ajua), wakiwatabiria mabaya wanasiasa, wanaaminika. Wakiwatabiria mazuri, wanatukanwa. Mungu amemilikishwa kwa watu wenye chuki dhidi ya viongozi.
HUU NI UCHURO WA TAIFA. HAUKUBALIKI.
Kwa nini tumefika hapa?
a. Mifumo ya utoaji haki katika taifa imefunikwa na giza linalokatisha tamaa wanyonge. Kimbilio lao limekuwa ni Mungu wa visasi. Shida zimewasahaulisha Mungu
wa Upendo.
b. Watu maskini na wanyonge wana hasira inayogeuka kuwa ukatili. Wanajiona yatima wasio na mtetezi. Adui yao mkuu siyo umaskini, ujinga na maradhi bali watawala, rafiki za watawala na ndugu wa watawala. Ukisikia wanasema “wao wana fedha, sisi tuna Mungu” elewa huyo Mungu ni silaha ya kuwaua watawala. Tuzinduke.
c. Tulifuta ukabila, udini, ueneo, na ubaguzi wa rangi. Bila kushtuka au kukubali kushtuliwa, tumeunda matabaka mawili makubwa: Watawala na watawaliwa. Moja lina uhakika wa kuishi na kutawala, jingine halina uhakika wa kuishi, kutawala, ajira, na usalama. Ndani ya matabaka hayo, yameibuka matabaka mengine madogo madogo yanayogombania makombo. Tabaka moja linasema “utanifanya nini?” Na jingine linasema “namwachia Mungu”.
Kutokana na kiwango cha UCHURO WA TAIFA tulichofikia, hakuna mtu au kundi lililo salama. Mkosoaji, chawa, na vizalia vyao, hawako salama. Ghadhabu ya watu maskini inawaka vifuani huku viburi na jeuri ya wenye madaraka ikitamalaki. Tushtuke.
TUSIPUUZE WITO WA KURUDI MEZANI
TUHARAKISHE MJADALA WA KITAIFA
HAKUNA HEKIMA ILIYOCHELEWA..
C&P