Ana hasira, STD Seven, nipo njia panda!

Ana hasira, STD Seven, nipo njia panda!

kitalembwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2014
Posts
6,142
Reaction score
15,756
Wakuu Wasalaam, ni muda kidogo sijaweka andiko hapa!

Kwanza kabisa poleni kwa msiba mkubwa wa kitaifa kupitia kuzama kwa Kivuko cha MV NYERERE, kama watanzania tulivyo ndugu kila mmoja aliguswa kwa namna yake, M/Mwenyezi azipokee roho za wale marehemu na pia awape nafuu wale majeruhi waweze kupona haraka!

Back to the topic, Mara baada ya kuhitimu chuo kuna mdada nilikutana nae, kwa kweli alinivutia sana, kama kawaida nikafunguka ya moyoni alinielewa japo kwa shida sana mwishoni akakubali tukawa wapenzi! Niseme tu ukweli ni kwamba nilitamani kupita nae tu maana nilikuwa na mtu wangu tulotoka chuo pamoja! Lakini kadri siku zilivyozidi kwenda nilijikuta nazidi kuvutiwa nae, hatimae likawa koloni la kudumu....yule wa chuo tulipotezeana na kikubwa kilichochangia ni umbali kwani kulingana na majukumu ya kikazi mimi nilibaki dsm na yeye yupo mkoa mwingine, maisha yakaendelea na huyu mpenzi mpya kama kawaida!

Huyu mpenzi mpya ni mtu flani muelewa sana, hana makuu , hajikwezi, yupo natural , neno samahani anajua kulitumia vyema pale linapohitajika! kwa kifupi ni wife material....hata kupewa kale kamchezo kwa mara ya kwanza tuseme nilimbaka...maana nilifanya kuforce sana baada ya kumkaribisha kwangu.....nakumbuka ile siku nilipiga kimoja kwa shida na alilia sana akinipa lawama, sijui hatujapima, mara nikimuonja ntamuacha nk!

Tuje kwenye maisha ya kawaida huyu ni mjasiriamali mdogo......ana pato la wastani, anajua kumake bajeti vizuri, anasomesha wadogo zake(baba yake alishafariki), pia hapa town keshanunua kiwanja! hapo namzungumzia mdada wa 20-26! ananishauri mambo mengi sana, pia anapenda sana kunikutanisha na ndugu zake pia hata mama yake aliyeko mkoani huwa nikiwa nae ananipa simu namsalimia! Pia ni mtu flani hana tabia hizi za wadada wa mjini...sijui mambo ya kula bata,gharama kubwa za saloon, mavazi nk! akiniazima hela anairudisha tar aliyoahidi akishindwa ataomba nimpe muda lakini huwa anairudisha, na akiniomba hela anaomba kiasi fulani na atakupa sababu za kukuomba na hela ataifanyia nini ! mapema mwaka huu mwezi april nilisafiri kwenda nyumban alinipa zawadi kadhaa nimpelekee mama (vitenge viatu n.k)

Ok kwa muhtasari huo nadhani nimeeleweka aina ya mtu niliye nae kwenye mahusiano! Shida iliyonileta hapa ni hii..huyu mtu kaishia darasa la saba, ugumu wa maisha ulimfanya asiendelee na elimu ya juu, hii ikapelekea kuishia la saba na kutafuta kazi! kwa elimu hiyo nawaza hata tukioana si atashindwa hata kumuelekeza mtoto home work ? maisha yanaenda kasi sana kiingereza kina umuhimu wake japo wengi mtanipinga! Jambo lingine na kubwa zaidi huyu mtu ana hasira japo kiasi chake.....anaweza kukujibu vibaya akiwa na hasira baadae akipoa atakuomba msamaha na machozi juu.....alishawahi kufanya jaribio la kutaka kijiua , ni hivi alikunywa sumu ila aliwahiwa wakampeleka hsp akapona! sababu kubwa ni matatizo ya kifamilia (ni story ndefu kidogo)! kipindi alichokunywa sumu tulikuwa bado hatujaonana, ni yeye alinipa story nzima ilivyokuwa........

Nawaza mengi....atakuwa wife material kweli ???? ni move on nitafute mwingine ? japo najua ni ngumu sana kumpata mtu wa aina yake, ana mengi mazuri na hayo mapungufu machache, ishu ya elimu sio kikwazo.....hizo hasira ndio shida! Wana MMU mawazo yenu ni muhimu
 
Swala la kutaka kujiua hilo pengine lilitokana na maisha aliyokuwa nayo. Jambo ambalo linaweza kumkuta kila mtu. Akiwa na maisha mazuri yenye mwelekeo hatawaza kujiua.
 
Swala la kutaka kujiua hilo pengine lilitokana na maisha aliyokuwa nayo. Jambo ambalo linaweza kumkuta kila mtu. Akiwa na maisha mazuri yenye mwelekeo hatawaza kujiua.
inawezekana mkuu
 
Mkuu wewe una elimu gani? Unaoa elimu ya mtu au unataka mke bora? Kupanga ni kuchagua.. Ushauri wangu kama ni mtu mwenye potentials elimu si kitu
 
Wazee wetu wangekuwa wanaangalia Elimu basi hiki kizazi kisingekuwepo.

Wewe unataka Ndoa au Elimu?

Muoe mpeleke "kwa Ras Simba" ili mkipata watoto iwe Rahisi kuwafundisha(maana una malengo watoto wako waje kusoma English medium)
 
Mkuu wewe wazazi wako walisoma?

Ondoa kigezo cha elim hapo, mana asilimia kubwa ya waliosoma wazazi wao hawakusoma.

Hasira hata kuku anazo.
 
Utapoona umeshindwa tupia humu namba yake. "Dhahabu" hiyo.
 
Mkuu kweli bila english hii dunia ni shinda kuishi, lakini mimi naona ni vizuri umupeleke shule, siku hizi sio lazima mtu aende shule iko aina ya software unaweza mununulia asome english poa kwanza kisa umufundise umuhimu wa maisha vile unataka je unataka awe housewife jambo ambao sio sawa siku hizi, sasa akisasoma unaeza muwekea bussiness, hapo atakuwa na elimu ya kufanya bookkeeping, balancing accounts, knowing profits and loss, assets and liabilities and such things. kuhusu hizo hasira zinaletwa na kukosa elimu, unajua kitu kinaitwa EMOTIONAL INTELLIGENT??????hio ndicho anakosa na hicho unaweza kukitoa akipata elimu sababu elimu nio huondoa IGNORANCE AND STUPIDITY, so plan how to educate her, and the rest will follow, hope i have adviced you on the best way forward sir, be blessed and nice week.
 
Wacha upimbi oa huyo mke haraka.Utaishia kuwapata wakina MUNALOVE! Shauri yako! Homework zako alikusadia nani?
 
Back
Top Bottom