Kiganyi
JF-Expert Member
- Apr 30, 2012
- 1,242
- 765
Makamu wa Rais Dokta MOHAMMED GHARIB BILAL Jumapili ijayo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Uzinduzi wa Vitabu Viwili vilivyotungwa na Katibu Mkuu Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi-CCM Mzee YUSUF MAKAMBA. Uzinduzi wa Vitabu hivyo ambavyo ni Binadamu na Kazi pamoja na Ukweli utafanyika katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa pia na wananchi, viongozi mbalimbali wakiwemo wa Chama, Dini na serikali.
Akizungumza na mtandao huu wa Francis Godwin Mzee Wa Matukio Daima Mtunzi wa Vitabu hivyo Mzee MAKAMBA amesema tayari Kitabu chake cha Kwanza kinachoitwa Makatazo ya Rushwa kilichozinduliwa na Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa FREDIRICK SUMAYE, serikali imetoa ruhusa kitumike kufundishia shule za msingi kuanzia Darasa la Tano hadi la Saba.
Pamoja na mambo mengine Mzee MAKAMBA amesisitiza kuwa katika Vitabu hivyo viwili kuna maudhui pia ya Masuala ya Dini ambayo yanahimiza nidhamu ya kazi kwa wananchi kwa kufanya kazi kwa bidii.
Kuhusu uwajibikaji wa kazi, amewaomba wananchi kutokubali kurubiniwa na baadhi ya wanasiasa kwa kufanya mandamano barabarani na badala yake amewataka kufanya kazi kwa bidii ili kuisaidia serikali kufikia malengo iliyojiwekea.
sosi; Fransis Godwin!
Akizungumza na mtandao huu wa Francis Godwin Mzee Wa Matukio Daima Mtunzi wa Vitabu hivyo Mzee MAKAMBA amesema tayari Kitabu chake cha Kwanza kinachoitwa Makatazo ya Rushwa kilichozinduliwa na Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa FREDIRICK SUMAYE, serikali imetoa ruhusa kitumike kufundishia shule za msingi kuanzia Darasa la Tano hadi la Saba.
Pamoja na mambo mengine Mzee MAKAMBA amesisitiza kuwa katika Vitabu hivyo viwili kuna maudhui pia ya Masuala ya Dini ambayo yanahimiza nidhamu ya kazi kwa wananchi kwa kufanya kazi kwa bidii.
Kuhusu uwajibikaji wa kazi, amewaomba wananchi kutokubali kurubiniwa na baadhi ya wanasiasa kwa kufanya mandamano barabarani na badala yake amewataka kufanya kazi kwa bidii ili kuisaidia serikali kufikia malengo iliyojiwekea.
sosi; Fransis Godwin!