Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Amos Makalla amesema madai kwamba Chama Cha Mapinduzi kinajiweka madarakani ni dhana potofu.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara mjini Newala mkoani Mtwara leo Jumanne Aprili 16, 2025, Makalla amesema: "Wapo wanaosema wamekichoka CCM. Wanasahau sisi hatujiweki madarakani, tunawekwa na Watanzania kupitia sanduku la kura kwa kazi tunazofanya."
Ameongeza kuwa: "Kama kuna mtu ana sera au ilani bora kuliko ya CCM, aje tulinganishe. Wananchi wataamua."
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Aidha, amesisitiza kuwa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba, mwaka huu hautasimama kwa sababu ya chama kimoja kutoshiriki na kwamba upo kwa mujibu wa sheria. "Uchaguzi upo kwa mujibu wa Katiba, si kwa ridhaa ya chama fulani."
Katika mkutano huo, Kapteni George Mkuchika amesisitiza nia yake ya kutogombea tena ubunge katika Jimbo la Newala, huku Nape Nnauye akimsifu kama kiongozi wa mfano. "Ukijua mlango wa kuingia, tafuta wa kutoka kabla hawajakutoa," amesema Nape.
Ameongeza kuwa: "Kama kuna mtu ana sera au ilani bora kuliko ya CCM, aje tulinganishe. Wananchi wataamua."
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Katika mkutano huo, Kapteni George Mkuchika amesisitiza nia yake ya kutogombea tena ubunge katika Jimbo la Newala, huku Nape Nnauye akimsifu kama kiongozi wa mfano. "Ukijua mlango wa kuingia, tafuta wa kutoka kabla hawajakutoa," amesema Nape.