Ametoa mimba nashindwa kumwacha

Ametoa mimba nashindwa kumwacha

Mlanje

Senior Member
Joined
May 16, 2013
Posts
141
Reaction score
77
Ndugu wanajamii mimi ni mwanaume wa miaka 27 na nimekuwa na mahusiano ya kwanza na mwanamke kuanzia 2011.Tangu nibalehe sikuwahi kufanya ngono kutokana na msimamo wangu wa kidini,tarehe 30 may 2012 nilivunja msimamo wangu baada ya kujiridhisha na mwanamke ambaye nilijua nitamwoa na nilifanya baada ya yeye kuwa na wasiwasi kuwa huenda nina mapungufu na alikuwa tayari kuachana nami kama ningemkatalia.Haikuwa shida nilifanya kumthibitishia uwezo wangu na baada ya hapo nilitaka tufunge ndoa maana sikutaka kuzini tena ila alikataa akiomba amalize masomo ya chuo kikuu kwanza pale UDSM.Tuliendelea na ule mchezo na mwaka huu alishika mimba na nikamhakikishia kuitunza hivyo asitoe baada ya miezi miwili aliniambia kuwa alikosea tu kujua mzunguko wa siku zake na hakuwa na mimba,ilinishangaza sana baada ya muda aliniambia kaka yake amegundua kuwa alikuwa na mimba baada ya kuona meseji kwenye simu yake ya dakitari aliyetoa akidai ampelekee pesa yake hivyo aliniomba niseme sijawahi kufanya nae ngono ikiwa babaye au kaka yake angeniuliza.Baba yake hakuniuliza na sasa anadai alikuwa sahihi maana aliogopa baba yake angeacha kumlipia ada maana hana mkopo,kiukweli nampenda sana na ndoa tulitaka kufunga December mwaka huu ila kwa hili nashindwa kuendelea na hata yeye hajutii na hajaniomba msamaha natamani kumwacha lakini moyoni nampenda sana naombeni ushauri wenu maana tayari hata pete ya uchumba nimemvisha home wanamjua na kwao wananijua Kiukweli nimeumia sana na nina msongo wa mawazo sana (Samahani kwa maneno mengi niliyotumia)
 
Kushindwa kufanya maamuzi magumu ni upuuzi, wanawake wapo wengi bwana piga chini time will heal pains za penzi hilo la sivyo subiri urudi kuomba ushauri. Yaani hata dhambi ya uuaji uioni? Halafu unasema ulikuwa na msimamo wa kidini. Kweli penzi limezidi îmani.
 
Chezea UD wewe mfanyie uchunguzi wa kutosha then ufanye maamuzi binafsi, usijekuta kushusha injini hakuanzia kwako.
 
hiyo mimba haikuwa yako na alikulazimisha mfanye kwa sabb tayari alikuwa na guy mwingine wa chuo wanayepeana piga chini
 
Make decision mpendwa
Kujitoa kwa mtu kiasi hicho afu mwenyewe haeleweki haipendezi
 
hiyo mimba haikuwa yako ndo mana kaitoa kuficha ushahidi.......
 
Je, nyumbani kwa binti wamekufahamu kwa kipindi gani mpaka sasa?
 
so unasema kuwa wamemgegedea demu wake lol
kwa asilimia kubwa yawezekana ikawa hvyo......mana hakuwa na sababu ya kufanya hvyo kama anauwakika ile mimba ni ya mchumba wake ambaye hata pete amemvalisha.....na nyumbani wanamfaham........hafu anaelekea mzoefu mana hata hashtuki kama kakosea......yeye anaona poa tu.
 
Mimba sio mpango wa Mungu ila mtoto ndio mpango wa Mungu... Mimba kitu gani banaaa ata ng'ombe anabeba.. Mi binafsi nawaoneaga sana huruma wadada wanaoflash.. ila ujue anayefanya ivyo yamemfika kooni.. Anyway amua kwa makini...
unaweza tafuta mwingine kumbe katoaga mimba 20 huko nyumaa...
 
hIYO MIMBA ILIKUWA YA KWAKO; NA NAAMINI ILI UPUNGUZE MAWAZO ITAKUBIDI UMUOE HUYO HUYO ILI KILA AKIPATA MIMBA AWE ANATOA; MTAISHI MAISHA MEMA KWANI FAMILIA YENU HAITAONGEZEKA; MTABAKIA WAWILI TU. (TUMIA AKILI ZAKO VIZURI)
 
Aisee! Yan hapo huyo binti anaonekana ni muongo afu keshazoea hako kamchezo ka kuchoropoa! Unadhan kwanini hajakushiriksha ktk kuitoa?think twice! itakuuma bdaye iktokea umemuoa alaf no kids huku ukijua kilitokea nin huko nyuma! What is uchumba by the way ? Znavunjika ndoa loh but ckilza moyo wako unataka nini! All the best!
 
Mimba sio mpango wa Mungu ila mtoto ndio mpango wa Mungu... Mimba kitu gani banaaa ata ng'ombe anabeba.. Mi binafsi nawaoneaga sana huruma wadada wanaoflash.. ila ujue anayefanya ivyo yamemfika kooni.. Anyway amua kwa makini...
unaweza tafuta mwingine kumbe katoaga mimba 20 huko nyumaa...

mmh wewe huyu huyu unasema mimba kitu gani wewe huyu huyu unawaonea huruma wanaoflash
which is which
 
Mkuu kwao wananifahamu tangu mwezi wa kumi mwaka jana
 

kuna mawili hapoooo
huenda mimba haikua yako
au hakupendi kama wewe unavyompenda
pia atakua mzoefu ndio maana hajakushirikisha
kwny utoaji!!piga chini usijejuta ndoa si lelemama!!
 
Back
Top Bottom