Ameniomba ushauri nimsaidieje???

Ameniomba ushauri nimsaidieje???

Crazy R

Member
Joined
Jun 1, 2019
Posts
40
Reaction score
9
Wakuuu hbr za usiku huu polen na uchovu wa majukumu ya kila siku ya kujitafutia riziki.Moja kwa moja pasipo kupoteza muda nijikite katika mada husika.
Ni kwamba nina mdogo wangu jinsia KE mtoto wa ndugu yangu.Huyu binti baada ya kuhitimu masomo yake ya O level mwaka 2016 na kufanikiwa kupata division two ya 20 alijiunga na masomo ya A level mwaka 2017 combination CBG.
Baada ya kusoma kwa takriban miaka 2 hatimaye mwaka huu amefanikiwa kuhitimu salama masomo yake ya elimu ya juu na sasa yupo nyumbani akisubiri matokeo kwa ajili ya kujiunga na chuo.
Kilichonifanya niandike Uzi huu ni kwamba huyu binti ameniomba msaada wa kimawazo baada ya kuingia mgogoro kati yake na wazazi wake juu ya kozi gani asome endapo atajiunga na elimu ya chuo.Kwa upande wa binti yeye anapenda sanaaaa kusoma kozi ya biashara na ndio lengo lake hilo.Kwa upande wa wazazi wake wanataka binti aende akasomee nursing kwani wao wanaamini nursing itamsaidia kupata ajira.
Kutokana na kuwepo kwa mitazamo hiyo miwili kinzani ndipo binti akaamua kuniomba ushauri juu ya kitu gani akasomee chuoni.Naomba msaada wa mawazo ni kitu gani nimshauri huyu mdogo wangu.
Ni hayo tuu ndugu zangu.
 
Note: Advance sio elimu ya Juu mkuu,Elimu ya Juu ni kusoma Degree hapo kuhitimu elimu ya Juu umekosea kidogo.

Mwaka Jana watu waliosoma CBG hawakuruhusiwa kusoma Nursing,nursing ilichukua watu waliosoma PCB na watu wa CBG waliachwa I'm not sure mwaka huu sasa.
Kama itakuwa hivyo Wazazi watakuwa wameshindwa hii plan yao na Binti atashinda.
Mkuu,Cha msingi ni vizuri wewe umuulize kwanini Biashara na sio course zingine maana mtoto akiamua kusoma kitu ni vizuri umuulize future plan yake kuliko kumkataza ili na wewe usije ingia mtego huo huo.
 
Kwa elimu yetu ya kibongo mtu hatakiwi kusoma kwa interest, bali muelekeo wa kidunia. Kwa sasa na ck za usoni pia fani za afya bado hazina ishindani sana wa ajira pamoja na kujiajiri. Kama atapata matokeo mazuri div 1-3, mie ningemshauri akasome Course ya Pharmacy. Kwa ushauri zaidi mwambie an PM
 
Note: Advance sio elimu ya Juu mkuu,Elimu ya Juu ni kusoma Degree hapo kuhitimu elimu ya Juu umekosea kidogo.

Mwaka Jana watu waliosoma CBG hawakuruhusiwa kusoma Nursing,nursing ilichukua watu waliosoma PCB na watu wa CBG waliachwa I'm not sure mwaka huu sasa.
Kama itakuwa hivyo Wazazi watakuwa wameshindwa hii plan yao na Binti atashinda.
Mkuu,Cha msingi ni vizuri wewe umuulize kwanini Biashara na sio course zingine maana mtoto akiamua kusoma kitu ni vizuri umuulize future plan yake kuliko kumkataza ili na wewe usije ingia mtego huo huo.
Nimepoke ushauri wako mkuuu pia nimefurahi kwa kunikosoa na kunirekebisha asante
 
Wakuuu hbr za usiku huu polen na uchovu wa majukumu ya kila siku ya kujitafutia riziki.Moja kwa moja pasipo kupoteza muda nijikite katika mada husika.
Ni kwamba nina mdogo wangu jinsia KE mtoto wa ndugu yangu.Huyu binti baada ya kuhitimu masomo yake ya O level mwaka 2016 na kufanikiwa kupata division two ya 20 alijiunga na masomo ya A level mwaka 2017 combination CBG.
Baada ya kusoma kwa takriban miaka 2 hatimaye mwaka huu amefanikiwa kuhitimu salama masomo yake ya elimu ya juu na sasa yupo nyumbani akisubiri matokeo kwa ajili ya kujiunga na chuo.
Kilichonifanya niandike Uzi huu ni kwamba huyu binti ameniomba msaada wa kimawazo baada ya kuingia mgogoro kati yake na wazazi wake juu ya kozi gani asome endapo atajiunga na elimu ya chuo.Kwa upande wa binti yeye anapenda sanaaaa kusoma kozi ya biashara na ndio lengo lake hilo.Kwa upande wa wazazi wake wanataka binti aende akasomee nursing kwani wao wanaamini nursing itamsaidia kupata ajira.
Kutokana na kuwepo kwa mitazamo hiyo miwili kinzani ndipo binti akaamua kuniomba ushauri juu ya kitu gani akasomee chuoni.Naomba msaada wa mawazo ni kitu gani nimshauri huyu mdogo wangu.
Ni hayo tuu ndugu zangu.
Hapo kwenye red,Mtoto wa ndugu yako atakuwaje kua mdogo wako?!
 
Kuna fundi wangu wa nguo yeye alikuwa na kipaji cha kushona na kupenda urembo. Baba yake alikuwa mwana sheria. Alimwambia yeye hakuzaa fundi charahani.

Yule dada alisoma PCM, alikwenda chuo cha Ardhi na kumaliza kama architect. Alimwambia Baba yake alisoma amridhishe lakini yeye ana furaha kuwa fundi charahani.
 
Akasomee anachokipenda.

Wengi waliosoma kwa kufuata maelekezo ya wazazi wameishia kupata ajira ambazo hawazifurahii.
 
Sawa mkuu
Kuna fundi wangu wa nguo yeye alikuwa na kipaji cha kushona na kupenda urembo. Baba yake alikuwa mwana sheria. Alimwambia yeye hakuzaa fundi charahani.

Yule dada alisoma PCM, alikwenda chuo cha Ardhi na kumaliza kama architect. Alimwambia Baba yake alisoma amridhishe lakini yeye ana furaha kuwa fundi charahani.
 
Back
Top Bottom