Jimmy George Sanga
Senior Member
- Jan 28, 2022
- 134
- 251
Habari za wakati huu wakuu,
Leo nimekutana na jamaa yangu ivi muhitimu wa chuo kikuu akiwa anauza ubuyu ni classmate wangu primary, Basi tukapata wasaa wa kupiga stori mbili tatu ambazo kwa kiasi kikubwa ulipelekea kuamini ule msemo wangu kwamba kwa Tanzania hii elimu sio dili, jamaa alikua ana akili balaa sema ndo ivo tu sasa hivi anatembeza ubuyu kazi ambayo ilipaswa kufanywa na watu wa aina yetu sisi.
Tuliokimbia shule kitambo

lakini saivi angalau nasi tunamiliki funguo ya chumba. Sijisifii ila huo ndo ukweli hata wewe apo unaesoma huu uzi kama umefika elimu ya juu jilinganishe uwezo wako kimaisha na yule ulie mwacha darasa la saba ni Mbingu na Ardhi.
Jamaa kwa jina anaitwa Jimmy, ni muhitimu wa kozi ya ualimu katika masomo ya jiografia na kiswahili (EGK) 2021. Katika moja ya chuo kilichopo visiwani. Ni kijana alietoka katika familia ya wakulima, akipata mkopo wa serikali wa 50% ambao amekua akijilipia ada pamoja na kusaidia nyumbani kwao.
Baada ya kuhitimu masomo yake akaamua kuomba nafasi katika shule mbalimbali kwa kujitolea ili aweze kuongeza uzoefu ili zikitokea nafasi sehemu awe na uzoefu fulani, lakini wahenga husema "Ng'ombe wa maskini hazai, akizaa kitoto kinakufa" ndo kitu kilichomtoke kwani mpaka wakati huu hakuna jibu lolote toka kwenye shule alizoomba kijana huyu, mpaka inafika mahali anakata tamaa ya kuendelea kufanya maombi hayo.
Kwa sasa kijana huyu ameamua kujiajiri kwa kuuza ubuyu pendwa wa visiwani, mtamu na mzuri kama sifa zilivyo za ubuyu ule wa visiwani, akiuza kwa kuutembeza mitaani mwingine anajumlisha kwa watu wengine. Amekua na soko la kuridhisha kidogo kwa kuwa umetokea kupendwa sana mjini mafinga, jambo kubwa ambalo linampa mtihani ni mtaji wake kuwa mdogo.
Hivyo ukiwa kama Mama, Baba, Kaka, Dada anaomba kwa hali na mali umsaidie mawazo, ushauri ni jinsi gani anaweza kukuza biashara yake na ili aendelee na biashara hiyo kwani ndoto za kuajiriwa ni kama vile zimekufa acha za kujitolea ndo kabisa
Anachukua ubuyu ndoo ndogo 3@20000/=
Usafiri kutoka visiwani hadi mkoani 20000/=
Vifungashio pamoja na label. 15000/=
Jumla hutumia 95000/= na hupata 115000/= ambapo faida huwa 20000/=
NAWASILISHA


KWA USHAURI NA MAWAZO
Leo nimekutana na jamaa yangu ivi muhitimu wa chuo kikuu akiwa anauza ubuyu ni classmate wangu primary, Basi tukapata wasaa wa kupiga stori mbili tatu ambazo kwa kiasi kikubwa ulipelekea kuamini ule msemo wangu kwamba kwa Tanzania hii elimu sio dili, jamaa alikua ana akili balaa sema ndo ivo tu sasa hivi anatembeza ubuyu kazi ambayo ilipaswa kufanywa na watu wa aina yetu sisi.
Tuliokimbia shule kitambo


lakini saivi angalau nasi tunamiliki funguo ya chumba. Sijisifii ila huo ndo ukweli hata wewe apo unaesoma huu uzi kama umefika elimu ya juu jilinganishe uwezo wako kimaisha na yule ulie mwacha darasa la saba ni Mbingu na Ardhi.Jamaa kwa jina anaitwa Jimmy, ni muhitimu wa kozi ya ualimu katika masomo ya jiografia na kiswahili (EGK) 2021. Katika moja ya chuo kilichopo visiwani. Ni kijana alietoka katika familia ya wakulima, akipata mkopo wa serikali wa 50% ambao amekua akijilipia ada pamoja na kusaidia nyumbani kwao.
Baada ya kuhitimu masomo yake akaamua kuomba nafasi katika shule mbalimbali kwa kujitolea ili aweze kuongeza uzoefu ili zikitokea nafasi sehemu awe na uzoefu fulani, lakini wahenga husema "Ng'ombe wa maskini hazai, akizaa kitoto kinakufa" ndo kitu kilichomtoke kwani mpaka wakati huu hakuna jibu lolote toka kwenye shule alizoomba kijana huyu, mpaka inafika mahali anakata tamaa ya kuendelea kufanya maombi hayo.
Kwa sasa kijana huyu ameamua kujiajiri kwa kuuza ubuyu pendwa wa visiwani, mtamu na mzuri kama sifa zilivyo za ubuyu ule wa visiwani, akiuza kwa kuutembeza mitaani mwingine anajumlisha kwa watu wengine. Amekua na soko la kuridhisha kidogo kwa kuwa umetokea kupendwa sana mjini mafinga, jambo kubwa ambalo linampa mtihani ni mtaji wake kuwa mdogo.
Hivyo ukiwa kama Mama, Baba, Kaka, Dada anaomba kwa hali na mali umsaidie mawazo, ushauri ni jinsi gani anaweza kukuza biashara yake na ili aendelee na biashara hiyo kwani ndoto za kuajiriwa ni kama vile zimekufa acha za kujitolea ndo kabisa
Anachukua ubuyu ndoo ndogo 3@20000/=
Usafiri kutoka visiwani hadi mkoani 20000/=
Vifungashio pamoja na label. 15000/=
Jumla hutumia 95000/= na hupata 115000/= ambapo faida huwa 20000/=
NAWASILISHA



KWA USHAURI NA MAWAZO

