Ambao watakosa kuandikishwa kwenye daftari la mpiga kura wanaruhusiwa kuishtaki tume ya uchaguzi?

Uandikishaji wa BVR umekuwa ukiendelea katika hali ya kulegalega na kuna uwezekano kuna watu wengi hawataandikishwa.Je ambao watakosa haki ya kuandikishwa kutokana na makosa ya tume ya uchaguzi wanaweza kudai haki yao mahakamani?

Binafsi Naona kusubiri mpaka zoezi likamilike tutakuwa tumechelewa na baadhi ya raia wema kukosa haki yao ya msingi. Nilitarajia mpaka sasa wanaharakati, viongozi wa dini na wanasiasa wawe tayari na majina ya walioshindwa kujiandikisha kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uzembe wa time, nilitarajia kuwa nimesikia tamko la tume juu ya watu hao. Haiingii akilini kujaza waangalizi wasaidizi wakati wa kupiga kura na kushindwa kuwa na waangalizi wakati wa uandikishaji ili kubaini kasoro na kuishauri tume!
 
Huu ni wakati wa kukusanya ushahidi wa mapungufu yanayojitokeza na kisha Tume iburuzwe mahakamani.

A pont is a point. Wanasheria nchini tafadhali anza mkakati wa kuzipitia sheria na tunahitaji msaada wenu safari hii. Tunataka atakayeshinda kama ni mafisadi basi iwe ni wazi kuwa watanzania tunapenda mafisadi na hapo hatuna la kufanya maana ndio democrasia lakini si kwa kunyima watu haki yao ya msingi kabisa kikatiba!!!
 
Wewe acha sound zako NEC haiwezi kushinikizwa kuandikisha wazembe ambao hawakujitokeza vituoni, wengine ni wahamiaji haramu unawakusanya vipi? Wewe ni mamlaka gani?

Sio uzembe kamanda, ila mashine za uandikishaji ndio zembe.
maana tupo kila siku katika vituo vya uandikishwaji, ila tunarudishwa manyumbani kila siku,kutokana na ufanisi wa mashine kuwa kulegalega.

Nimaajabu mtu kwenda kituoni asubuhi ya saa moja anakaa mpaka jioni bila kuandikishwa, alafu anaambiwa aje kesho yake.
Je watakaokwenda hiyo kesho,wataandikishwa lini.?

UZEMBE SIO WA WANANCHI, ILA UZEMBE NI WA MASHINE KUWA NA UFANISI MDOGO,KULINGANA NA IDADI YA WATU.
 
Na kama mtu ametimiza umri mwezi wa 8?

acha utani, umri huo siyo wa kuruhusiwa kupiga kura. Hivyo hana sifa ya kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Huyo usimnyang'anye haki yake ya kucheza wakati huu wa likizo.:playball::playball::playball::playball:
 
acha utani, umri huo siyo wa kuruhusiwa kupiga kura. Hivyo hana sifa ya kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Huyo usimnyang'anye haki yake ya kucheza wakati huu wa likizo.:playball::playball::playball::playball:
Unapopiga kura inabidi uwe na miaka.mingapi? na kura zitapigwa lini?
 
Wanaharakati na wanasheria wangeanza kuchukua hatua sasa kwa kuanzia na maeneo ambayo tayari uandikishaji umeshapitA.
 
Unapopiga kura inabidi uwe na miaka.mingapi? na kura zitapigwa lini?

Hebu uwe makini ndg. Miaka 8 huyo anapiga kura ya kumchagua kiongozi wake wa darasa? Nina mashaka na wewe. Usikomae kwa kitu usichokijua. Uliza kwa wenzako uelimishwe kabla hujaanza kuchukua hatua ya kuweka mawazo yako hewani yasomwe na wengi. Utasutwa
 
watu wengi wanaokosa kujiandikisha ni kwa uzembe wao ukiangalia kwa makini siku saba ni nyingi na zinatosha kabisa kuandikisha
 
weka hapa hayo makosa sio kelele za bavicha hapa
Umeenda siku ya kwanza saa.kumi.usiku mpaka inafika jioni hujaandikishwa siku ya pili hivohivo mpaka siku ya saba imepita.Then ukakosa kuandikishwa kwa sababu mashine hazikuwa na uwezo wa kuandikisha watu wote je hili ni kosa la nani?
 
acha utani, umri huo siyo wa kuruhusiwa kupiga kura. Hivyo hana sifa ya kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Huyo usimnyang'anye haki yake ya kucheza wakati huu wa likizo.:playball::playball::playball::playball:

Na kama mtu ametimiza umri mwezi wa 8?

Unapopiga kura inabidi uwe na miaka.mingapi? na kura zitapigwa lini?

Hebu uwe makini ndg. Miaka 8 huyo anapiga kura ya kumchagua kiongozi wake wa darasa? Nina mashaka na wewe. Usikomae kwa kitu usichokijua. Uliza kwa wenzako uelimishwe kabla hujaanza kuchukua hatua ya kuweka mawazo yako hewani yasomwe na wengi. Utasutwa

We Bukama Batoko sijui kama unakijua unachoandika.Hivi upo makini na kazi yako kweli embu rudia tena kusoma ndo uje uandike hapa nimeweka quotes zote ili usome kiurahisi
 
Wewe ulewe viroba ukae bar waandikishaji wakufuate bar

hivi hizo bangi za bavicha unazipendea nn

Mkuu nafikiri hufuatilii kinachoendelea, kuna watu walikua kwenye foleni siku ya mwisho ya uandikishwaji kwenye kituo chao. Muda wa kufunga ulivyofika wakaambiwa waondoke waje kesho yake.

Siku iliyofuata watu wa tume hawakutokea. We unafikiri hawa watu watapeleka wapi malalamiko yao?
 
Uandikishaji wa BVR umekuwa ukiendelea katika hali ya kulegalega na kuna uwezekano kuna watu wengi hawataandikishwa.Je ambao watakosa haki ya kuandikishwa kutokana na makosa ya tume ya uchaguzi wanaweza kudai haki yao mahakamani?

Kibaya wale wa mwanzo mwanzo ktk foleni hizi za BVR ,nahisi tu!/WANAWEZA KUWA WANA CCM / wakimalizika tu BVR zinaanza KUGOMA.
OMBI:- kwa NEC
--->>VITAMBULISHO VYA ZAMANI VIRUHUSIWE tunawaomba kwa moyo MKUNJUFU KWA MWENDO WA MASHINE HIZI WENGI TUTAIKOSA HAKI YETU!
 
Kibaya wale wa mwanzo mwanzo ktk foleni hizi za BVR ,nahisi tu!/WANAWEZA KUWA WANA CCM / wakimalizika tu BVR zinaanza KUGOMA.
OMBI:- kwa NEC
--->>VITAMBULISHO VYA ZAMANI VIRUHUSIWE tunawaomba kwa moyo MKUNJUFU KWA MWENDO WA MASHINE HIZI WENGI TUTAIKOSA HAKI YETU!

Du! Unamawazo mgando! Hata teknolojia nayo mmeipa chama? Jamani acheni hayo mawazo ya kuwadanganya wananchi, kama wewe unayeonekana unamwanga na teknolojia unakuwa na mawazo mafinyu hivi, kwa watu wa kawaida utawapotosha wewe. Acha tabia zako za kuwa mdanganyifu hivyo. Teknolojia haiana chama.
 
Mimi nadhani kuwa wakipeleka shauri lao mahakamani na hasa wakiwa ni wengi wanaweza hata kusimamisha zoezi la uchaguzi hadi nao waandikishwe kwa kuwa ni haki yao kisheria na sio fadhila!
 
Back
Top Bottom