Ama kweli mvumilivu hula mbovu

Ama kweli mvumilivu hula mbovu

Sumulenga

Member
Joined
Jul 2, 2016
Posts
60
Reaction score
36
wakuu habari,

Hivi serikali ya awamu hii ya tano inampango gani na vijana hawa wanaosubiria ajira? Maana vijana wamekuwa wakihangaika na wakiishi kwa matumaini siku hadi siku.

Wanashindwa kujiingiza katika kutafuta kazi za kudumu au kusaini mikataba kutokana na ukweli kwamba raisi alisisitiza baada ya miez miwili.

Wanatamani kulitumikia taifa lao kutokana na ujuzi walioupata wakiwa vyuoni lakin serikali inaweka kigugumiz kutamka lini watawaajir hawa vijana.

Madhalani, walimu wamefundishwa masuala ya kuandaa andalio LA solo, ama andalio LA kazi. Sasa unaposema wajiajir inamaana kwamba kila baada ya mtaa kuwe na "Tuition centre"?

Ni vyema serikali ikawaweka wazi ili kama mwaka huu hawaajir basi vijana hawa waandae malengo ya mda mrefu. Kuliko kukaa kimya na mda unazidi kisonga mbele Pasi na uhakika.

Serikali toweni tamko LA kueleweka ili vijana wajijue.
 
Solution ni kurudi kijijini kulima..simple serikali ina mambo mengi sio kutoa ajira tu nani aliwaambia wakimaliza kusoma wataajiriwa?
 
Solution ni kurudi kijijini kulima..simple serikali ina mambo mengi sio kutoa ajira tu nani aliwaambia wakimaliza kusoma wataajiriwa?
Acha upuuzi ww na siasa zenu za maji taka.

Kichwani mweupe km chokaa.

USIJIFIKIRIE WW MWENYEW KM WAFIA CHAMA WA LUMUMBA. Fikiria na wengine.
Km una sehemu ya kukuwezesha kuingia chooni. Mshukuru Mungu
 
umesoma shule ya kata ukajitahidi umefaulu vizuri ukaenda chuo kusoma kwa mkopo leo eti ukajiajiri kwa mtaji upi? wewe na phd yako na uprofesa wako leo miaka 25 upo kwenye ajira ya kuajiriwa kwa nini hukuacha kazi ukajiajiri? acheni hizo leo ulitumbuliwa presha juu
 
Solution ni kurudi kijijini kulima..simple serikali ina mambo mengi sio kutoa ajira tu nani aliwaambia wakimaliza kusoma wataajiriwa?
..Hv fulsa ni kulima tu hapa Tanzania!??maana kila anaetoa ushauri ni huo huo rudi kijijini kulima....tupanuane mawazo jamani kilimo vilevile bado sio suruhusho kwa kijana wa kitanzania maana ukweli hata masoko ya hayo mazao bado ni ubabaishaji tu na story zisizoisha....
 
Wajenge viwanda basi jaman uwiioiiieee yeuwiiiiiiiiiiiie auwiiiiiiii yeuwiiiiii jaman nife au????
 
Solution ni kurudi kijijini kulima..simple serikali ina mambo mengi sio kutoa ajira tu nani aliwaambia wakimaliza kusoma wataajiriwa?
Basi serikali ingeacha kufindisha mambo ambayo hawawezi kuyafanyaia kaz bila wao kuwaajir
 
..Hv fulsa ni kulima tu hapa Tanzania!??maana kila anaetoa ushauri ni huo huo rudi kijijini kulima....tupanuane mawazo jamani kilimo vilevile bado sio suruhusho kwa kijana wa kitanzania maana ukweli hata masoko ya hayo mazao bado ni ubabaishaji tu na story zisizoisha....
Kweli kabisa
 
umesoma shule ya kata ukajitahidi umefaulu vizuri ukaenda chuo kusoma kwa mkopo leo eti ukajiajiri kwa mtaji upi? wewe na phd yako na uprofesa wako leo miaka 25 upo kwenye ajira ya kuajiriwa kwa nini hukuacha kazi ukajiajiri? acheni hizo leo ulitumbuliwa presha juu
Ah ah ah wao wanasisitiza kujiajir lakin wao hawaonyeshi mifano
 
..Hv fulsa ni kulima tu hapa Tanzania!??maana kila anaetoa ushauri ni huo huo rudi kijijini kulima....tupanuane mawazo jamani kilimo vilevile bado sio suruhusho kwa kijana wa kitanzania maana ukweli hata masoko ya hayo mazao bado ni ubabaishaji tu na story zisizoisha....
Kulima ni adhabu kwa watz
 
Solution ni kurudi kijijini kulima..simple serikali ina mambo mengi sio kutoa ajira tu nani aliwaambia wakimaliza kusoma wataajiriwa?
Mkuu laki si pesa,

Kulima siyo kazi rahisi kama unavyojua Mkuu.

Hiyo ni kama kujiajiri ni lazima uwe na mtaji mkubwa, nyenzo mbalimbali za kilimo.

Pia kwa hapa Tanzania ambapo mkulima hathaminiki inakuwa ni ngumu sana kutoboa kimaisha kwa sababu utalima vizuri ukija kwenye upande wa soko unakuta ulicho kilima mara bei imeshuka na muda huo una majukumu mengi tu ya kufanya hivyo inakubidi tu uuze kwa bei ya chini ili uweze kutekeleza majukumu mengine.

Kwa hali hiyo kivipi mkulima utatoboa hapa Tanzania?
 
Ajira ni janga la dunia siyo la vijana wa Tanzania pekee hivyo ni jukumu la kila kijana kutafuta ni jinsi gani anaweza kujiajiri
 
Jiajirini ebu fikiria maelfu ya vijana wanaomaliza vyuo kila mwaka serikali haitaweza kuajiri wote,iliyobaki ni kutafuta njia mbadala ya kujiajiri, mbona mnaambiwa kila siku amusikii?
 
Hata kilimo siyo cha kuvamia tu.
Watu wamelima nyanya msimu uliopita wakaishia kuuza ndoo kubwa ya lita 20 iliyojaa mpaka pomoni kwa shilingi 2000 pale Morogoro,unaweza kulima ukaangukia pua tu,tupatieni ajira mwisho wa mwezi tuwe na uhakika.
 
Ah ah ah wao wanasisitiza kujiajir lakin wao hawaonyeshi mifano
Wao wanakimbilia siasa hadi kwenda kuroga ili wafanikiwe,kujiajiri sio rahisi kama wanavyofikiria pia ni karama kutoka kwa mola sio kila mtu anaweza.
 
Back
Top Bottom