Nikiwa nimelala chumbani na my wife,mara nikapatwa na shortcall ya haja ndogo.Nikaamka na kwenda zangu toilet.Ile narudi ndani,nikiwa sebuleni,nikasikia mwanangu Elvis ambaye huwa analala na housegirl wangu akilia.Nikachukua uamuzi wa kuingia chumba cha hg wangu nikamkuta mwanangu amesahaulika,hajafunikwa shuka,neti imechomoka,mbu wanamtafuna mwanangu,hg kajifunika yeye tu.Kosa nililofanya ni kuvuta upande wa shuka aliojifunika hg ili nimfunike mwanangu,weeeee! Alikurupuka ghafla,aliponiona akaanza kupayuka;'shemeji sitaki ivo,ushindwe na ulegee'.Ninachoshukuru wakati yeye akipayuka ivo,mi nilikuwa busy kumfunika mwanangu kisha nikamwambia aweke net vizuri halafu asimsahau tena mtoto kama alivyofanya hapo kabla.Hapo ndipo Jaguar nikaeleweka,binti akatuliza mzuka na kuendelea na usingizi.Bahati nzuri wakati binti akipayuka vile,wife alikuwa kalala fofofo na wala hakustukia ule mchezo.Sijui ingekuwaje angemsikia hg akipayuka halafu anikute nikiwa chumbani kwa hg,duuh nimekoma!
Si unajua tena mabeki 3 wengi huwa wanawaheshimu wake zetu kama dada zao,kwa hiyo huyu gael clichy wangu alikuwa anamuita mke wangu dada kwa heshima na pia mimi huwa ananiita shem.Huyo hg ni shemeji yako pia? Msingi wa kukuita shemeji unatokea wapi? Mkuu kama hii story umeipika vile!!!!!
hamna cha kasheshe walanini alifuata nini huko siangeenda kumwamsha my wife wake aendeakamwangalie mtoto.kihelehele kingemponza.kesho usirudie tena.