Ally Salum Hapi, Ukweli huishi milele daima kaka.!

Ally Salum Hapi, Ukweli huishi milele daima kaka.!

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,255
Reaction score
8,027
Wahenga walishawahi kunena kua "Uongo hufika kwa njia ya mkato lakini huishi kwa muda mfupi" na "Ukweli huchelewa kufika lakini hudumu milele"

Leo asubuhi akihojiwa na kituo cha StarTV kwenye mjadala unaohusu hali ya kisiasa kwa ujumla nchinj DC wakinondoni ndugu Alli Hapi ametoa tafsiri ya neno Demokrasia kua ni "Ni kuwapatia wananchi huduma muhimu kama Maji,Afya,Elimu,barabara nk." Kwakweli nikaamini kua kuna watu hufanya makusudi kabisa kuuweka pembeni ukweli na kuamua kuongea tu ilimradi watu flani flani waridhike.

Hivi kweli ndugu Alli akikutana na mtoto wa darasa la tatu akamuuliza "Neno demokrasia lina maana gani? halafu huyu mtoto akajibiwa jibu kama hili ataelewa nini? hivi demokrasia ni kutimiza ahadi ulizoahidi kwa wananchi kweli? Kupeleka Umeme kijijini ni demokrasia? Demokrasia ina maana gani hasa?Abraham Lincoln ailiposema kua demokrasia ni utawala wa watu kwa ajili ya watu nkwa watu alimaanisha nini? Inamaana hata hili hulielewi kaka?

Hata Marehemu Muamar Gadafi wa Libya na Sadam Husein wa Iraq nao walikua wakiwapatia wananchi wao huduma zote tena kwa 100% mpaka mwingine aliwasaidia hata vijana kuona na kuwalipa pesa za matumizi wasiokua na kazi.Lakini wananchi hawa walikua wakilia kila siku kua hakuna Demokrasia, walilia kua hakuna Uhuru wa kufanya siasa,walilia kua hakuna Uhuru wa kuongea ama kukosoa serikali yao, walioonekana kupinga serikali waliitwa wachochezi na wengine kuitwa wahaini, wengine waliopinga serikali waliuawa,waliteswa,walifungwa na wengine walikimbilia uhamishoni.

Unachokiona Libya na Iraq kwa sasa ni kwa sababu wananchi walitaka Demokrasia na sio huduma za kijamii,kwa sababu walipatiwa kila walichotaka ispokua demokrasia tu.


Kiufupi ndugu yangu Alli Hapi wewe ni msomi mzuri sana na mjenga hoja mzuri, simamia ukweli huwezi kufukuzwa kazi kwa sababu ya kuusema. Kwa nafasi uliyonayo kwa sasa you are supposed to be focused and distinguished person na sio kuogopa kuusema ukweli.Ukweli huchelewa kufika lakini hudumu milele na Uongo hufika kwa haraka ila huishi kwa muda mfupi.
 
Naunga mkono hoja,ajitathimini kwa upya huyu bwana
 
Wahenga walishawahi kunena kua "Uongo hufika kwa njia ya mkato lakini huishi kwa muda mfupi" na "Ukweli huchelewa kufika lakini hudumu milele"

Leo asubuhi akihojiwa na kituo cha StarTV kwenye mjadala unaohusu hali ya kisiasa kwa ujumla nchinj DC wakinondoni ndugu Alli Hapi ametoa tafsiri ya neno Demokrasia kua ni "Ni kuwapatia wananchi huduma muhimu kama Maji,Afya,Elimu,barabara nk." Kwakweli nikaamini kua kuna watu hufanya makusudi kabisa kuuweka pembeni ukweli na kuamua kuongea tu ilimradi watu flani flani waridhike.


Hivi kweli ndugu Alli akikutana na mtoto wa darasa la tatu akamuuliza "Neno demokrasia lina maana gani? halafu huyu mtoto akajibiwa jibu kama hili ataelewa nini? hivi demokrasia ni kutimiza ahadi ulizoahidi kwa wananchi kweli? Kupeleka Umeme kijijini ni demokrasia? Demokrasia ina maana gani hasa?Abraham Lincoln ailiposema kua demokrasia ni utawala wa watu kwa ajili ya watu nkwa watu alimaanisha nini? Inamaana hata hili hulielewi kaka?


Hata Marehemu Muamar Gadafi wa Libya na Sadam Husein wa Iraq nao walikua wakiwapatia wananchi wao huduma zote tena kwa 100% mpaka mwingine aliwasaidia hata vijana kuona na kuwalipa pesa za matumizi wasiokua na kazi.Lakini wananchi hawa walikua wakilia kila siku kua hakuna Demokrasia, walilia kua hakuna Uhuru wa kufanya siasa,walilia kua hakuna Uhuru wa kuongea ama kukosoa serikali yao, walioonekana kupinga serikali waliitwa wachochezi na wengine kuitwa wahaini, wengine waliopinga serikali waliuawa,waliteswa,walifungwa na wengine walikimbilia uhamishoni.

Unachokiona Libya na Iraq kwa sasa ni kwa sababu wananchi walitaka Demokrasia na sio huduma za kijamii,kwa sababu walipatiwa kila walichotaka ispokua demokrasia tu.


Kiufupi ndugu yangu Alli Hapi wewe ni msomi mzuri sana na mjenga hoja mzuri, simamia ukweli huwezi kufukuzwa kazi kwa sababu ya kuusema. Kwa nafasi uliyonayo kwa sasa you are supposed to be focused and distinguished person na sio kuogopa kuusema ukweli.Ukweli huchelewa kufika lakini hudumu milele na Uongo hufika kwa haraka ila huishi kwa muda mfupi.
Wanajitoa ufahamu lakini wanaelewa fika kuhusu kila jambo
 
Kwa Tanzania maana hiyo ys demokrasia bado ina hold. Ndiyo maana hata leo utawasikia wanasiasa wanasema 'miaka hamsini ya uhuru , nchi haina 1, 2,3. Maana yake wananchi bado wako level ya chini ya hairakia ya mahtaji ya Maslow.
 
Huyu alitaka kuongoza mapinduzi ya kumpindua Kipara enzi hizo pale Udsm. Ila kipara alikuwa mjanja sana na mapinduzi hayakufanikiwa. Sijui kipara atakuwa wapi sasa hivi? Nilitegemea angekuwa na kacheo kidogo. Alikuwa politician kuliko Salum.
 
Siku hizi usomi wenyewe wanauweka pembeni anaongopa akitenguliwa anaogopa ataishi vipi mjini..
 
  • Thanks
Reactions: BAK
hapi ni kijana anayejitambua.tatizo alikuwa anatetea mkate wake. msameheni wadau....
Kama anaweza kuongopa wazi wazi namna hiyo kwa ajili ya kutetea mkate wake, hahitaji kusamehewa na watu. Nasema hivi kwa sababu msamaha huo hautamsaidia chochote kwa kuwa ameamua kujitenga na watu ili kulinda nafasi yake kwa mtawala. Kwake mtawala anatosha, hahitaji watu...
 
Kwa kweli nami nilikitazama hiko kipindi kwa kweli nilishangaa sana. Sijui watu wanaogopa sema ukweli hata Kama wanaujua au wanalinda nafasi zao
 
Alli Hapi ametoa tafsiri ya neno Demokrasia kua ni "Ni kuwapatia wananchi huduma muhimu kama Maji,Afya,Elimu,barabara nk."

Naona pale Lumumba siku hizi kuna chuo cha siasa. Ndiko viongozi wa sasa wanakopata definitions za namna hii.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Makanisani watenda dhambi hutengwa,vile vile mahekaluni,huyu jamaa sijui ,okay Mungu atahukumu.

Aibu inamwendea mwalimu wake wa Civics,na Prof Majamba aliyemfundisha LLb kwamba democracy ni huduma ya maji na umeme.

Kama digrii watu wangemyamyanywa basi nahisi senete ya UDSM wangesha mnyamganya
 
Demokrasia ni dhana ambayo haina tafsiri moja, na hakuna maana moja ya demokrasia inayo kubalika na dunia nzima
Labda useme ulitaka aongelee demokrasia kwa mtazamo wa ki magharibi, hapo uta kuwa sahihi.
Tafsiri ya Gaddafi ilikuwa ina mashiko yake lakini, ilikosa vinasaba vya u magharibi na watu wake ndio walitaka wawe na demokrasia kama hiyo ndio waka mtoa.
Hapi alikuwa sahihi ila si kwa mtazamo wa ki magharibi. Na wewe uko sahihi ila si kwa mtazamo wa ki jamaa, na ki dhahania nyingine za demokrasia
 
Back
Top Bottom