Ally Mayayi atangaza kugombea Urais TFF

Ally Mayayi atangaza kugombea Urais TFF

Frank Wanjiru

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2012
Posts
24,625
Reaction score
43,901
Nyota wa zamani wa Yanga Sc na timu ya Taifa,Taifa Stars, Ally Mayay Tembele ametangaza nia ya kushiriki uchaguzi mkuu wa TFF mwaka huu kama mgombea nafasi ya Urais wa Shirikisho hilo unaotarajiwa kufanyika Agosti 16, 2025 Jijini Tanga.

Mwakilishi wa nahodha huyo wa zamani wa Stars atamchukulia fomu hiyo hii leo mchana tayari kwa kugombea nafasi hiyo kwenye uchanguzi mkuu wa Shirikisho la Soka nchini TFF.
 
Nyota wa zamani wa Yanga Sc na timu ya Taifa,Taifa Stars, Ally Mayay Tembele ametangaza nia ya kushiriki uchaguzi mkuu wa TFF mwaka huu kama mgombea nafasi ya Urais wa Shirikisho hilo unaotarajiwa kufanyika Agosti 16, 2025 Jijini Tanga.

Mwakilishi wa nahodha huyo wa zamani wa Stars atamchukulia fomu hiyo hii leo mchana tayari kwa kugombea nafasi hiyo kwenye uchanguzi mkuu wa Shirikisho la Soka nchini TFF.
Utopolo aongoze TFF???
 
Binafsi namtakia kila la heri.

Na ni wakati sasa wa Shirikisho kurejea mikononi mwa wenye mpira wao. Mambo ya kuruhusu wanasiasa kuongoza Shirikisho, yametuletea mvurugano mwingi sana.

NB: Wallace Karia usijaribu kujiongezea muda mwingine wa kuliongoza hilo shirikisho! Hakikisha unafuata nyayo za watangulizi wako. Mihula yako miwili inakutosha sana. Na pia siyo vizuri kumpandikiza chawa wako wa kuendeleza siasa za simba na Yanga kwenye shirikisho.

Waachie wenye mpira wao ili waliongoze hilo shirikisho kwa kufuata sheria na kanuni za mpira wa miguu! Na siyo mashinikizo kutoka kwa wanasiasa wenzako.
 
Binafsi namtakia kila la heri.

Na ni wakati sasa wa Shirikisho kurejea mikononi mwa wenye mpira wao. Mambo ya kuruhusu wanasiasa kuongoza Shirikisho, yametuletea mvurugano mwingi sana.

NB: Wallace Karia usijaribu kujiongezea muda mwingine wa kuliongoza hilo shirikisho! Hakikisha unafuata nyayo za watangulizi wako. Mihula yako miwili inakutosha sana. Na pia siyo vizuri kumpandikiza chawa wako wa kuendeleza siasa za simba na Yanga kwenye shirikisho.

Waachie wenye mpira wao ili waliongoze hilo shirikisho kwa kufuata sheria na kanuni za mpira wa miguu! Na siyo mashinikizo kutoka kwa wanasiasa wenzako.
Karia anataka kumpandikiza chawa wake, Influence bado anayo kubwa sana kwenye tume ya uchaguzi wa TFF, kapeleka uchaguzi Tanga kwenye ngome yake.
 
Uongozi ni zaidi ya simba na yanga nyie wafia timu.! Wachezaji wengi wa zamani hawajasoma kwahiyo mpira wa kisasa una mikutano mingi tu nje ya nchi ! Huyo ally mayai anaenda kuongea nini huko nchi za watu mtu hata English hajui
 
Mambo mengine wawe hata wanapeleka mikoa mingine ambayo haijakua kisoka ili waimotivate, mambo mengi kama ni nje ya dar basi Tanga.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom