Allerg ya vumbi na harufu

Allerg ya vumbi na harufu

nameless girl

JF-Expert Member
Joined
Apr 22, 2012
Posts
4,195
Reaction score
2,685
Hey ndugu zangu, nawasalimu wote.

Binafsi nina allergy na vumbi pamoja na vitu vyenye harufu kali. Hata ikitokea nimeweka nguo safi kabatini lakini ikichukua muda mrefu pasipo kuivaa, siku nitakapoigusa ni balaa. Hata nikienda sehemu ambayo chumba cha kulala hakikutumiwa siku nyingi (let say, unaenda masomoni, ukirudi likizo home), nitaugua kwa wiki kadhaa.

Hapa nilipo mafua yamenibana sana kisa vumbi. Napata mawazo kwenye kulala itakuaje mana uwa nakosa pumzi kabisa.

Sasa swali langu kwa madokta, inawezekana kupona allergy yani nisipate hili tatizo kabisa mana ikitokea nipo ugenini inakua tabu kuchagua mara shuka za kulalia mara kitanda. Pia hii kitu inanikosesha raha kabisa.

Eti Mzizimkavu, na wengine wote wanaoweza nishauri, kuna dawa kweli hii kitu ikapona moja kwa moja?
 
There is one Dr mboneko ni mtaalam mzuri tu wa allergy. Yuko Mbezi tangi Bovu maeneo ya kituo cha oilcom anaweza kusaidia
 
Hey ndugu zangu, nawasalimu wote.
Binafsi nina allergy na vumbi pamoja na vitu vyenye harufu kali. Hata ikitokea nimeweka nguo safi kabatini lakini ikichukua muda mrefu pasipo kuivaa, siku nitakapoigusa ni balaa. Hata nikienda sehemu ambayo chumba cha kulala hakikutumiwa siku nyingi (let say, unaenda masomoni, ukirudi likizo home), nitaugua kwa wiki kadhaa.
Hapa nilipo mafua yamenibana sana kisa vumbi. Napata mawazo kwenye kulala itakuaje mana uwa nakosa pumzi kabisa.
Sasa swali langu kwa madokta, inawezekana kupona allergy yani nisipate hili tatizo kabisa mana ikitokea nipo ugenini inakua tabu kuchagua mara shuka za kulalia mara kitanda. Pia hii kitu inanikosesha raha kabisa.
Eti Mzizimkavu, na wengine wote wanaoweza nishauri, kuna dawa kweli hii kitu ikapona moja kwa moja?

pole sana.......

tiba kubwa ya kwanza ya allergy ni kutokusogelea kinachokuletea allergy........ ikitokea umeshakutana na mazingira hayo au inakulazimu kuyafuata hayo mazingira inabidi utumie dawa jamii ya antihistamine kama vile cetrizine.

nb; hizo unazoita vumbi kuwa ndiyo inayokuletea allergy siyo vumbi , mbona ukitembea barabarani kwenye vumbi au ukitimuliwa vumbi na magari pua hazibani?

kinachokuletea hiyo allergy ni vumbi lililochanganyika na aina fulani ya fungus ( kama vumbi la sehemu yenye unyevu nyevu kama vile uvunguni au chumba ambacho hakijatumika muda mrefu) ambao nao hupatikana pia kwenye nguo zilizokaa kabatini muda mrefu bila kutumika.

pia kuna pollen , animals na cocroach remainings(mende na mabaki yake)........
 
Ngambo Ngali, naomba utoe maelekezo zaidi ya kumpata Dr. Mboneko maana alinisaidia sana mtoto wangu kupona ugonjwa wa ngozi.
 
pole kwa tatizo, nafikiri ni vizuri ujaribu tiba mbadala tatizo lako linaweza kuwa historia, kwa maelezo zaidi piga namba 0655290333 au 0764 058454
 
Ngambo Ngali, naomba utoe maelekezo zaidi ya kumpata Dr. Mboneko maana alinisaidia sana mtoto wangu kupona ugonjwa wa ngozi.

Huyo Dr Mboneko hawezi kumsaidia yule mtoto mwenye ugonjwa wa ngozi?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
pole sana.......

tiba kubwa ya kwanza ya allergy ni kutokusogelea kinachokuletea allergy........ ikitokea umeshakutana na mazingira hayo au inakulazimu kuyafuata hayo mazingira inabidi utumie dawa jamii ya antihistamine kama vile cetrizine.

nb; hizo unazoita vumbi kuwa ndiyo inayokuletea allergy siyo vumbi , mbona ukitembea barabarani kwenye vumbi au ukitimuliwa vumbi na magari pua hazibani?

kinachokuletea hiyo allergy ni vumbi lililochanganyika na aina fulani ya fungus ( kama vumbi la sehemu yenye unyevu nyevu kama vile uvunguni au chumba ambacho hakijatumika muda mrefu) ambao nao hupatikana pia kwenye nguo zilizokaa kabatini muda mrefu bila kutumika.

pia kuna pollen , animals na cocroach remainings(mende na mabaki yake)........

Asante sana sana sana.
 
There is one Dr mboneko ni mtaalam mzuri tu wa allergy. Yuko Mbezi tangi Bovu maeneo ya kituo cha oilcom anaweza kusaidia

kaka ni PM nambayake au tuweekee location ya huyu Dr vizuri coz me pia na sumbuliwa na fangus wa miaka mingi nimejaribu kutafuta tiba hadi nahisi kukata tamaa sasa..plz
 
kaka ni PM nambayake au tuweekee location ya huyu Dr vizuri coz me pia na sumbuliwa na fangus wa miaka mingi nimejaribu kutafuta tiba hadi nahisi kukata tamaa sasa..plz

Call +255713739940 talk to Sister Sarah who will arrange an appointment for you.
 
habari wana jamvi hili,mimi ni mama wa miaka kadhaa,ninatatizo la allegy ya pua,koo,macho na masikio kwa muda mrefu,yaani harufu kidogo pamoja na vumbi tu ikinipitia naanza kupiga chafya na kupata mafua ,masikio nayo yanawasha balaa,najitahidi nisiingize kitu masikioni ila nashindwa maana hayaachi mpata uyakune,nikienda hospitali naishia kupewa cetrizine na allerid tu ambazo naon km hazinisaidii kitu,mbaya zaidi naona hali hii mtoto wangu wa miaka miwili nayo inaanza kumpata,maana mida ya kuanzia saa kumi alfajiri pua zinaziba anahema kwa tabu mpaka anaamka anakaa,kma kuna mtu anaju tiba ya hili tatizo naomba anisaidie
 
Habari wana jamvi hili, mimi ni mama wa miaka kadhaa, ninatatizo la allegy ya pua, koo, macho na masikio kwa muda mrefu.

Yaani harufu kidogo pamoja na vumbi tu ikinipitia naanza kupiga chafya na kupata mafua, masikio nayo yanawasha balaa, najitahidi nisiingize kitu masikioni ila nashindwa maana hayaachi mpata uyakune.

Nikienda hospitali naishia kupewa cetrizine na allerid tu ambazo naona kama hazinisaidii kitu, mbaya zaidi naona hali hii mtoto wangu wa miaka miwili nayo inaanza kumpata, maana mida ya kuanzia saa kumi alfajiri pua zinaziba anahema kwa tabu mpaka anaamka anakaa.

Kama kuna mtu anaju tiba ya hili tatizo naomba anisaidie.
 
habari wana jamvi hili,mimi ni mama wa miaka kadhaa,ninatatizo la allegy ya pua,koo,macho na masikio kwa muda mrefu,yaani harufu kidogo pamoja na vumbi tu ikinipitia naanza kupiga chafya na kupata mafua ,masikio nayo yanawasha balaa,najitahidi nisiingize kitu masikioni ila nashindwa maana hayaachi mpata uyakune,nikienda hospitali naishia kupewa cetrizine na allerid tu ambazo naon km hazinisaidii kitu,mbaya zaidi naona hali hii mtoto wangu wa miaka miwili nayo inaanza kumpata,maana mida ya kuanzia saa kumi alfajiri pua zinaziba anahema kwa tabu mpaka anaamka anakaa,kma kuna mtu anaju tiba ya hili tatizo naomba anisaidie
Pole sana unapatikana mkoa gani!?

Tatizo lako ni Allergic Rhinitis pamoja na kutumia dawa unapaswa kujiepusha na Allergens na Irritants.
 
Back
Top Bottom