Mpitagwa
JF-Expert Member
- Feb 10, 2012
- 2,339
- 1,119
Huu si uchawi ni aina ya mitambiko ya jamii ya kimaasai kama umefanya jambo baya labda umeua haujaonekana au hakuna ushahidi wa kukutia hatiani.Wazee wa kimila jamii ya kimaasai Malaigwanani wataitisha mkutano na kutangaza nia ya kuvunja Chungu sababu itawekwa wazi,waliohusika watatakiwa kujitokeza na kurejesha kitu kilichoibiwa labda ni Mbuzi au Kuku.Chungu hakivunjwi bila kutangaza hilo ni sharti la kwanza kabisa.
Mfano nimewahi kuona matangazo ya kusudio la kuvunja Chungu likiwa limepata baraka za Mwenyekiti wa Kitongoji na kubandikwa sehemu mbali mbali ili wahusika walisome na ikiwezekana wajitathimini na pengine waombe msamahaa kwa mujibu wa mila au itakavyoamuliwa na muathirika wa sakata hilo.
Tukirejea kwa mgombea XYZ sijamtaja jina mpaka sasa kwakuwa hili jambo ni nyeti sana ,kama umekula fedha zake na umempigia kura hapo hakuna madhara kabisa shida ni iwapo umekula fedha zake kura ukampigia mtu mwingine au haukwenda kupiga kura kabisa.
Kama ni hivyo hii itawazuru wamasai tu lakini watu wamataifa hawatazulika. Imagine XYZ angekuwa Lowassa na hicho chungu kiwe na uwezo wa kuzulu mtu yeyote haijalishi kabila gani. CCM wangebaki wangapi?