Aliyenitoroka amerudi na mimba

Aliyenitoroka amerudi na mimba

youngsharo

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2015
Posts
2,491
Reaction score
500
Ndugu wanajukwaa,

Mnamo mwezi wa 7 tar.1 kama sikosei nilileta uzi hapa kuwa mpenzi/mwanamke niliyekuwa ninaishi nae alisafisha kila kitu na kutoroka wiki moja kabla sijaleta uzi huo.

Kwa kumbukumbu ilikuwa kama tar 22 mwezi wa 6,Jana majira ya mchana nikiwa kwenye chumba changu cha kupanga alichoniacha nikiwa sina kitanda wala nguo ya kubadilisha nikasikia watu wanapiga hodi.

Baada ya kufungua nikamkuta ni yule aliyekuwa mpenzi wangu yupo na rafiki yake na wakati huo alikuwa analia akiomba nimsamehe kwa alichokifanya.

Nikajaribu kumuuliza vitu alivipeleka wapi amedai eti yeye aliviacha ndani hakuchukua chochote isipokuwa wakati anaondoka hakufunga mlango kwahiyo wezi wanaweza kuwa waliingia baada ya yeye kuondoka.

Lakini sikuishia hapo nikamuuliza nini kilimfanya atoroke akaniambia yeye mwenyewe haelewi kwanini alifanya vile na bado ananipenda anahisi ni pepo tu lilimuingia.

Kibaya zaidi nilipoenda kumpima tayari ana mimba ya wiki 3 ila hajaathirika.

Je, kama ndo wewe ungemfanyaje?
 
youngsharo

Wewe unahitaji kuambiwa nini katika mazingira hayo? Mbona kila kitu kipo wazi, achana na huyo mwanamke hakufai. Ila kama una ugonjwa wa kupenda na kujitoa akili basi endelea.
 
Last edited by a moderator:
embu kua mkubwa na acha mawazo mgando aisee we ushaibiwa na ushapigiwa bado unataka ushauri?
 
nimeuliza ivo kwa maana kuwa; nikamfungulie mashtaka ya kuniibia au nimpe talaka tu basi aende na safari zake?

Ndugu kama hujipendi jaribu tena kumkaribisha ukae nae, keshakuliza mara ya kwanza hapo amerudi akupige tena akaongeze mtaji.
 
Ur not serious kuuliza ufanyeje dah! Inaonekana unampenda japo karudi na mimba asee
 
Back
Top Bottom