Aliyenitoroka amerudi na mimba

Aliyenitoroka amerudi na mimba

Nakushauri muache ajifungue alafu mtoto mpeleke kwa baba yake....funga naye ndoa...kabla ya ndoa afanyiwe kicheni pati,vyombo atakavyozawadiwa umwambie ni mali yako kufidia vile alivyoiba...alafu mpe talaka arudi kwao...maisha yanaendelea
 
Ndugu wanajukwaa,

Mnamo mwezi wa 7 tar.1 kama sikosei nilileta uzi hapa kuwa mpenzi/mwanamke niliyekuwa ninaishi nae alisafisha kila kitu na kutoroka wiki moja kabla sijaleta uzi huo.

Kwa kumbukumbu ilikuwa kama tar 22 mwezi wa 6,Jana majira ya mchana nikiwa kwenye chumba changu cha kupanga alichoniacha nikiwa sina kitanda wala nguo ya kubadilisha nikasikia watu wanapiga hodi.

Baada ya kufungua nikamkuta ni yule aliyekuwa mpenzi wangu yupo na rafiki yake na wakati huo alikuwa analia akiomba nimsamehe kwa alichokifanya.

Nikajaribu kumuuliza vitu alivipeleka wapi amedai eti yeye aliviacha ndani hakuchukua chochote isipokuwa wakati anaondoka hakufunga mlango kwahiyo wezi wanaweza kuwa waliingia baada ya yeye kuondoka.

Lakini sikuishia hapo nikamuuliza nini kilimfanya atoroke akaniambia yeye mwenyewe haelewi kwanini alifanya vile na bado ananipenda anahisi ni pepo tu lilimuingia.

Kibaya zaidi nilipoenda kumpima tayari ana mimba ya wiki 3 ila hajaathirika.

Je, kama ndo wewe ungemfanyaje?



Mtoto wa kiume usiwe mjinga....huyo alishatendwa huko alikokwenda na sasa anatafuta sehemu ya kurudi ili ajitafakari na kujipanga upya. Kama alikukosea tayari basi hauna sababu ya kumrudisha. Msamehe ila mpige dochi atajijuwa, kumbuka kuwa hakuna mtu mwenye akili timamu akafanya kitu bila kufikiri au kuwa na sababu. Huyo hakuwa na nia nzuri nawe hivyo mwache aende mbele na akaipeleke hiyo mimba kwa anayestahili kuilea. Usipende kuwa na used spare parts zitakutoa nishai at any time.
 
Pepo lake linataka kulisalimia pepo lako.
Ni issue ndogo tu
 
Usiulize maswali ya kijinga, umemweka ndani tayari halafu unauliza tungefanyaje? We ni Mtanzania kweli?
 
Nakushauri muache ajifungue alafu mtoto mpeleke kwa baba yake....funga naye ndoa...kabla ya ndoa afanyiwe kicheni pati,vyombo atakavyozawadiwa umwambie ni mali yako kufidia vile alivyoiba...alafu mpe talaka arudi kwao...maisha yanaendelea

duh you are the great thinker una mawazo ya mbali kweli.
 
Hilo lakwako jepesi sana...chakufanya mlee huyo mwanamke...usimuache...
 
We mwenyewe pia ujielewi kwanza umeibiwa pili ametoroka tatu karudi na mimba bado unataka ushauri kweli wewe ubongo lala
 
Acha uongo wee kenge... Mimba inaanza kuonekana ktk mkojo baada ya wiki mbili. Na hamna namna ya kuitambua mimba ya wiki tatu labda uwe unaishi na mwanamke na mnafanya countdown ya siku mnazokutana. Hivo acha kudanganya UMMA wa JF
 
Ndugu wanajukwaa,

Mnamo mwezi wa 7 tar.1 kama sikosei nilileta uzi hapa kuwa mpenzi/mwanamke niliyekuwa ninaishi nae alisafisha kila kitu na kutoroka wiki moja kabla sijaleta uzi huo.

Kwa kumbukumbu ilikuwa kama tar 22 mwezi wa 6,Jana majira ya mchana nikiwa kwenye chumba changu cha kupanga alichoniacha nikiwa sina kitanda wala nguo ya kubadilisha nikasikia watu wanapiga hodi.

Baada ya kufungua nikamkuta ni yule aliyekuwa mpenzi wangu yupo na rafiki yake na wakati huo alikuwa analia akiomba nimsamehe kwa alichokifanya.

Nikajaribu kumuuliza vitu alivipeleka wapi amedai eti yeye aliviacha ndani hakuchukua chochote isipokuwa wakati anaondoka hakufunga mlango kwahiyo wezi wanaweza kuwa waliingia baada ya yeye kuondoka.

Lakini sikuishia hapo nikamuuliza nini kilimfanya atoroke akaniambia yeye mwenyewe haelewi kwanini alifanya vile na bado ananipenda anahisi ni pepo tu lilimuingia.

Kibaya zaidi nilipoenda kumpima tayari ana mimba ya wiki 3 ila hajaathirika.

Je, kama ndo wewe ungemfanyaje?





je unahisi mimba ni yako?kama unahuakika mimba ni yako basi msamehee mlee mimba na mtoto maana kuna wanawake wengine wakiwa wajawazito hata ya week mmoja akili zao zinavurugikaga na hata moods zao hubadilika wanakuwa tofauti,na wengine hadi hupata kichaa cha mimba,so msamehee tuu jaribu kumuelewa,huku ukimuangalia kama atarudia kosa kama hilo na kama unahuakika mimba sio yako muache atulie kwanza kama week au mwezi kwako alafu jaribu kuongea nae kistaarabu akuelewe ili muachane kwa amani na utulivu.
 
Acha uongo wee kenge... Mimba inaanza kuonekana ktk mkojo baada ya wiki mbili. Na hamna namna ya kuitambua mimba ya wiki tatu labda uwe unaishi na mwanamke na mnafanya countdown ya siku mnazokutana. Hivo acha kudanganya UMMA wa JF

mimba huanza kuonekana kwenye mkojo baada ya siku 7 yaan baada ya week,na maumbile ni tofauti wengine huonyesha dalili za mimba na maswahiba yake ndani ya week hiyohiyo ya kwanza,kama kuumwaumwa,kichechefu,mood swings na vinginevyo,.....
 
mimba huanza kuonekana kwenye mkojo baada ya siku 7 yaan baada ya week,na maumbile ni tofauti wengine huonyesha dalili za mimba na maswahiba yake ndani ya week hiyohiyo ya kwanza,kama kuumwaumwa,kichechefu,mood swings na vinginevyo,.....

sasa anachokataa yeye ni nini? mi nimemwambia wiki 3 au inaonekana wiki mbili tu then inapotea?
 
achana na huyo mwanamke akajifunze huko sio Mke huyo utakuwa huna akili za kiume kabisa kumrudisha ndani mtu Wa namba hiyo
 
Back
Top Bottom