Aliyemshambulia Dr. Stephen Ulimboka ni huyu...

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Hawezi kuwa mwingine.Ni yule ambaye Dr.Ulimboka na Madaktari wenzake wanamlalamikia.Ni katika harakati za kumnyamazisha na kutisha wengine.Ni huyu ambaye amewahi harakaharaka kuunda tume za uchunguzi au kutoa amri ya kufanywa uchunguzi wa kina.Ni huyu ambaye anajiandaa kujichunguza mwenyewe na kujipa ripoti mwenyewe.Atakuwa ni huyu ambaye ameacha kutoa taarifa za nini suluhisho la mgomo wa Madaktari leo Bungeni.Amefanikiwa kufanya alichotaka.Je,atafanikiwa kupata akitakacho?
 
Mkuu, sidhani kama tutakuwa sahihi kuhukumu mtu kwa dhana. unaonaje kama tungetafuta uwezekano wa kuwa na tume huru, itakayo chunguza na kutoa taarifa kwa umma? nani asimamie hili, na nani aanzishe mchango wa gharama za uchunguzi, hilo ni suala lingine. Lakini tusitegemee ukweli kutoka kwenye tume itakayoundwa na tunao dhani kuwa wanaweza kuwa wamehusika kwa njia moja au nyingine. Mimi ni mmoja wa walio tayari kuchangia.
"MUNGU IBARIKI TANGANYIKA, MUNGU IBARIKI ZANZIBARI, RIP TANZANIA"
 
Of course wanaweza, yaani hilo nalo ni neno, lakini labda uniambie kwamba wale jamaa nao ni mashushushu (Vigogo) ambao wanayo influence serikalini hata leo, kwamba wanaweza kuamuru vijana wao wamlimboka daktari wetu. Kama ndivyo yataanikwa tu, humwagi damu ya binadamu ukawa salama, haiwezekani. Kama unadhani nabisha muulize Kaini aliyemuua nduguye Habili wakiwa peke yao porini. Ardhi ni shuhuda mzuri na anajua kuelezea mambo. Bado mimi napata shida sana kutenganisha maneno ya "LIWALO NA LIWE" na tukio zima la Ulimboka connected so closely in time hata katoto kachanga kanaweza kuelewa muunganiko huo. My take, yeyote atajwaye ni kwa jina la serikali. Waombe Mungu sana apone haraka na wala wasijaribu kumfuatilia kummalizia, kwa sababu watatangula wao kumalizwa, maana sasa janja ya nyani madaktari wameishaitambua. Walidhani wanatibu kumbe walichofikiri ni maji ya kuzimia moto ni petrol. Shame on them!

Ulimboka usihofu, utapona tu mwanangu. Wanaokujua na hata wasiokujua, kwa sasa wameunganika kulikabidhi jina lako kwa Mungu aliyekunusuru, ili akuimarishe urudi barabarani tena, kiwembe kikali zaidi kuliko kwanza, sababu umepitishwa kwenye tanuri la moto mkali. Mzee Nelson Mandela alishasema "Mtu maarufu maisha yake ni machungu sana" Huo ndio msalaba Mungu kakukabidhi ubebe, mrudishie Mungu wako Utukufu, maana leo hii unasikiliza watu wanavyoguswa, ambapo adui zako hawakutaka ushuhudie haya masikitiko ya watu hawa. Doctors, be serious, unite!
 
Kila mtu analijua hilo, nadhani ile katuni ya kipanya ya uchaguzi wa Dhaifu na Dikteta inahitajika kufanyiwa marekebisho.
 
mtu anapoibiwa hupata dhambi kubwa kuliko aliyeiba kwa kumdhania kila amuonaye ndo mwizi wake...,,mbona hamwasemi waaliofiwa na wagonjwa wao kwa kukosa huduma sababu ya mgomo nfo wanahusika???
 
Hata tukiunda tume huru mwisho wa siku ripoti itapelekwa kwa nani kwa ajili ya kuishughulikia?who will take action if not the same weak government?weak peresident,weak prime minister?under the same weak political party-Magamba?then kutakuwa na matokeo gani?hapa ni wananchi tu,kuna haja ya kuli-table jambo hili kwa nguvu ya umma.
 
"liwalo na liwe " Mizengo Pinda 27 juni 2012 kwenye bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania

"Sasa hata hatujazungumza wameanza kutangaza mgomo, sasa afadhali tuzungumze kwanza maana mgomo una kasheshe zake, mkigoma hamtaachwa, askari watawapiga virungu na hata wengine kuweza kupoteza maisha, mimi naweza kuwa rahim (mwenye huruma) lakini polisi mkiwafanyia fujo watawatwanga na hata mkigoma baadaye mtarudi kwenye mazungumzo mkiwa na plasta midomoni," Jakaya Kikwete 3 mei 2010 ukumbi wa Diamond Jubilee kuzungumzia mgomo wa tucta ya Mgaya

hawa ndo waliomshambulia dr Ulimboka...
 
hivi serikali ya ccm inadhani inaongoza mbuzi na si binadamu, wanatangaza vita ambapo tumezoea amani! kama wamechoka kutuongoza siwaseme kuliko kutubuluza kama mbuzi? hivi wanadhani tumesahau matatizo ya arusha! wasisazani hatuna uchungu na damu zetu zinazopotea ovyooooo! wananchi tumechoka kubuluzwa, duu kweli nimeamnini haki mbinguni na si duniani. Ulimboka asipopona tutaandamana nchi nzima, kwakuwa mmezoea kutumiminia lisasi tuko tayari mbona majeraha ya arusha bado tunayo hivyo mmeshatupa uzoefu inshort tumezoea, hakuna kulala hadi kieleweke people's poweraaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!
 
"liwalo na liwe " Mizengo Pinda 27 juni 2012 kwenye bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania

"Sasa hata hatujazungumza wameanza kutangaza mgomo, sasa afadhali tuzungumze kwanza maana mgomo una kasheshe zake, mkigoma hamtaachwa, askari watawapiga virungu na hata wengine kuweza kupoteza maisha, mimi naweza kuwa rahim (mwenye huruma) lakini polisi mkiwafanyia fujo watawatwanga na hata mkigoma baadaye mtarudi kwenye mazungumzo mkiwa na plasta midomoni," Jakaya Kikwete 3 mei 2010 ukumbi wa Diamond Jubilee kuzungumzia mgomo wa tucta ya Mgaya

hawa ndo waliomshambulia dr Ulimboka...
Sasa ndio umesema nini yaani kama vile umeshakula cha Arusha,
 
Back
Top Bottom