Aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza auwawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa mawe

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,202
5,021
Aliyekuwa mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza ndg CLEMENT MABINA ameuwawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa mawe huko maeneo ya Kisesa jijini Mwanza.

Chanzo cha kuuwawa ni kwamba mabina aliwanyang'anya ardhi wananchi hao na kesi ikawa mahakamani na leo mchana Mabina bila kibali cha mahakama alikuwa anapanda miti na kujenga msingi wa nyumba ndipo wanachi wakaenda kumhoji iweje anapanda miti na kuweka msingi kwenye viwanja hivyo ilhali kesi ipo mahakamani?

Mabina akaanza kutoa lugha chafu na kurusha risasi hewani.

Kwa mujibu wa Katibu wa CCM ndg Joyce Masunga (maarufu kama Maziwa Fresh) ni kweli kuwa tukio hili limetokea na tunaendelea kufuatilia kupata habari zaidi.

============

Mwananchi Dec 16, 2013:

Kutoka kwa wanaomfahamu kwa karibu:

=============
PICHA kwa wasiomfahamu:



Clement Mabina akiwa na Rais Kikwete (enzi za uhai wake) CCM Kirumba katika sherehe za kutimiza miaka 35 ya kuzaliwa kwa CCMsherehe hizo za kutimiza miaka 35 ya kuzaliwa kwa CCM

=========

Mwili wa Marehemu

 
Aliyekuwa mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza ndg CLEMENT MABINA ameuwawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa mawe huko maeneo ya Kisesa jijini Mwanza.

Chanzo cha kuuwawa ni kwamba mabina aliwanyang'anya ardhi wananchi hao na kesi ikawa mahakamani na leo mchana Mabina bila kibali cha mahakama alikuwa anapanda miti na kujenga msingi wa nyumba ndipo wanachi wakaenda kumhoji iweje anapanda miti na kuweka msingi kwenye viwanja hivyo ilhali kesi ipo mahakamani?

Mabina akaanza kutoa lugha chafu na
 
Inaendelea.........
Risasi zilipomuishia na kufanikiwa kumuua raia m1 kwa risasi ndipo wananchi wenye hasira kali wakamrudia kumpiga wakiwa na mapanga, mawe na kila dhana ya kijadi, jambo lililopelekea umauti kumkuta. Mauaji yametokea mchana huu majira ya saa 7.
 
Kama ni kweli, basi hii ni mbaya sana! Wangempeleka katika vyombo vya sheria jamani.
 
Mh!!! kwa kuwa ni TETESI ngoja nisubiri uhakika ndio niseme ninachotarajia kusema
 
what is the indication? ukihusisha na utoaji na usimamiaji wa haki
 
Inakuwaje kiongozi wa umma anaamua kutumia mabavu kuhalalisha mambo; na kivipi wananchi wakachukua uamuzi huo. Utawala wa sheria ulikuwa wapi? Any way hata Mvomero wafugaji na wakulima wanatoana roho bila serikali kuchukua initiatives. RIP Mabina
 
Mhh...kumbe pana chezea Sukumaland veve. Tusubiri propaganda kutoka Lumumba maana sasa wako kwenye foleni kupokea buku 7 za kula mchana pale Lumumba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…