Mogadishuu
Member
- Jun 22, 2019
- 33
- 65
Huu ni usemi nilisikia kwa Sheikh mmoja hivi, nahisi amenigusa mimi kabisa. Nimekosea kupenda hivyo nimeyakosea Maisha yangu kabisa. Nipo kwenye ndoa lakini niliyemuoa nilikuja gundua simpendi japo yeye ananipenda sana na ninayempenda siwezi kumuoa ilimradi tabu tupu.
Natamani siku zirudi nyuma nirekebishe makosa lakini haiwezekani sijui hata nifanye nini. Natamani niishi peke yangu tu lakini najiuliza mimi ni mwanaume nikishikwa na hamu itakuwaje? Nizini? Siwezi. Au nibaki kwenye ndoa lakini tuishi mbali mbali na huyo mke wangu, maana simtendei haki kuwa nae karibu, namkosea mpaka nafsi inanisuta.
Naona bora nibaki peke yangu tu, niwahudumie familia nikiwa mbali nao, nimpe na uhuru huyo mke wangu kama akipata mtu nimpe talaka ili aolewe na mwingine.
Na huyo ninayempenda hatuwezi kuwa wote tena. Shida
Natamani siku zirudi nyuma nirekebishe makosa lakini haiwezekani sijui hata nifanye nini. Natamani niishi peke yangu tu lakini najiuliza mimi ni mwanaume nikishikwa na hamu itakuwaje? Nizini? Siwezi. Au nibaki kwenye ndoa lakini tuishi mbali mbali na huyo mke wangu, maana simtendei haki kuwa nae karibu, namkosea mpaka nafsi inanisuta.
Naona bora nibaki peke yangu tu, niwahudumie familia nikiwa mbali nao, nimpe na uhuru huyo mke wangu kama akipata mtu nimpe talaka ili aolewe na mwingine.
Na huyo ninayempenda hatuwezi kuwa wote tena. Shida