Aisee amesema huwezi kufanya maombi ili uchumi ukue.
Akaendelea kulonga hata mimi chungaji sifanyi ujinga kama huo. Paulo mtume anasema "Na asiye fanya kazi na asile" na siyo asiye fanya kazi aombewe.
Sisi wachungaji kazi yetu ni kuombea wazinzi na wanachukua wake zawatu..
Nazani kamkuna mtu.... ahsante msigwa.
Mwigulu "shame on you"
Kama hoja za bunge na michango ya bungeni inaruhusiwa kutaja, maneno ya kidini kama pepo, shetani, wachungaji, maaskofu, masherk, maimamu' n.k, ujue siku za uharibifu zimekaribia (asomae na afahamu) Tanzania inaelekea pabaya ndugu zanguni, hizi dini ni zawakoloni walizitumia ili watutawale na kutuhujumu, ndo likaja lile neno kwamba mtu akikupiga upande huu mgeuzie na wa pili akupige tena, yaani mkoloni akikufanya mtumwa, mpe na malighafi kama maliasili, n.k, lakini ukweli tujiulize sisi wenyewe kwamba tunajenga ama tunabomoa, unapochoma shule ya misheni ama hospital ya misheni watoto wako watasomea wapi? Je? Unataka kutudanganya kwamba Kcmc,bugando,seliani, mtakatifu agostino, hakuna mtu wa dini tofauti anae hudumiwa huko? Ama kufanya kazi huko? Mbona twajimaliza wenyewe? Mimi naunga mkono mia kwa mia tisa kwamba muungano uvunjwe tukajipange upya ili mzanzibari akishindwa kutibiwa mnazi mmoja apelekwe oman na sio muhimbili.