Alioyasema Ahmedinejad kuhusu 9/11

Alioyasema Ahmedinejad kuhusu 9/11

Joined
Sep 25, 2010
Posts
18
Reaction score
8
Hotuba ya rais wa Iran kuhusu what was claimed a terrorist attack ya 9/11 huko US yanaweza yakawa na ukweli wowote kweli?

Sijui huyu jamaa anawaza nini katika cmments zake kuhusu mambo yanayohusu siasa za ulimwengu huu usioisha vita kwa sababu za watu kama yeye wasiotaka maridhiano ya amani bila kuoneshana mbavu ya kijeshi.

Mmhm me ssemi chochote kwa leo nawaachia nyinyi!
 
Rais wa Iran aliyasema hayo ili tuu kuwaprovoke wamarekani na yeye kujionyesha Irani pia ni super power.
 
Issaya achana nao hao, unaufahamu msemo "Waarabu wa Pemba wanajuana kwa vilemba?" Basi ndio hao Iran na Marekani. Leo hii Iran wakitaka kununua zana za kivita, basi Marekani watawauzia kama vile hakukutokea lo lote vile.
 
Hawa jamaa kweli wanajuana kwa vilemba but we have 2 learn from their mistakes tusije laaniwa kama wao!
 
Kuna mambo ambayo yanatia shaka kuhusu suala zima la kuanguka kwa majengo siku ile na wachambuzi wa majengo na mambo ya milipuko wameshindwa kuelewa ni kwa namna gani majengo yalivyoweza kuanguka kwa style ile tena kwa wakati mmoja,pia kuna mashaka kuhusu mabaki ya ndege zile na nyingine iliyokuwa inaelekea Pentagon kutoonekana wala hakuna mwenye data kuhusu hilo.Mambo hayo ndio yanatia shaka na raisi wa Iran naye ni mmoja wa watu ambao wana shaka na namna ya suala zima lilivyokwenda na kwa kuwa ana uwezo wa kusema kuliko wengine ambao ni waoga mbele ya taifa kubwa kama Marekani.
Kwa sisi ambao tunaamini kuwa siku ile ni magaidi ndio walifanya vile ni vigumu kuamini aliyoyasema Ahmadinejad ila kwake na wengine bado wana maswali magumu ambayo majibu yake mpaka sasa hayajapatikana.
 
hakuna raisi aliyeingiwa na shetani kama ahamadinejad, kwanza kabisa al quaeda wanakiri kwamba wao ndo wamelipua, afu yeye anasema hajalipua kitu...wajerumani wote walishuhudia kuwa holocost ilitokea mbele ya macho yao, yeye anasema haikutokea, hivi ni akili ya aina gani hiyo...wana shida waliompata rais wa aina hiyo. macho ni yetu kuona rais huyu wa iran anapoenda kuteka kaburi la mtume kule wanakoenda kuhiji watoto wa mamamdogo...nuke ikipatikana tu, mandege ya saudia ambayo nchi ya saudia ilinunua Germany kwa kujilinda na iran sidhani kama yatafanya kazi. yetu macho.
 
Back
Top Bottom