Yaani mapito yangu na yako yamefanana ila mimi hakuwa ma mdogo bali sheji yangu mke wa kakangu mzaliwa tumbo moja. Nilimheshimu sana kakangu kiasi nilimwita baba. Alikonitoa ni mbali mno kutoka kolomije ya kwetu na kunimwaga darisalama.
Akanitunza, akanipa kila kitu ka mdogo wake. Kisa kilianza aliposafiri kwa muda mrefu kaniachia mke japo hela ya chakula ni mkewe alikuwa nayo. Ndugu yangu, kuna kausemi kuwa; Mke si ugali tu bali ile shughuli ni muhimu umtimizie. Shem akani mind kinoma. Miye nikamkumbuka kaka nikagoma.
Hapo visa vikaanza. Aliporudi kaka ndo nikasingiziwa nilitaka kumbaka. Nakumbuka nilipigwa kipigo cha mbwa koko. Nikafukuzwa home, nikaishia kwa ba mdogo aliyekuwa hapo.
Nimemaliza skuli, nimepata kazi, kaka katumbuliwa. Miye ndo naishi matawi ya juu, yeye hana mbele wala nyumma.
Nilimsaidia pamoja na familia yake yote zaidi ya miaka 5. Hata alipopata kibarua hakuhama kutoka kwangu hadi mauti ilipomchukua. Sasa nimebakia na shem na familia yake na yangu.
Akanitunza, akanipa kila kitu ka mdogo wake. Kisa kilianza aliposafiri kwa muda mrefu kaniachia mke japo hela ya chakula ni mkewe alikuwa nayo. Ndugu yangu, kuna kausemi kuwa; Mke si ugali tu bali ile shughuli ni muhimu umtimizie. Shem akani mind kinoma. Miye nikamkumbuka kaka nikagoma.
Hapo visa vikaanza. Aliporudi kaka ndo nikasingiziwa nilitaka kumbaka. Nakumbuka nilipigwa kipigo cha mbwa koko. Nikafukuzwa home, nikaishia kwa ba mdogo aliyekuwa hapo.
Nimemaliza skuli, nimepata kazi, kaka katumbuliwa. Miye ndo naishi matawi ya juu, yeye hana mbele wala nyumma.
Nilimsaidia pamoja na familia yake yote zaidi ya miaka 5. Hata alipopata kibarua hakuhama kutoka kwangu hadi mauti ilipomchukua. Sasa nimebakia na shem na familia yake na yangu.