Bingwaman
JF-Expert Member
- Oct 22, 2010
- 548
- 288
Wengi tunamfahamu mwanamuziki Defao kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, lakini ni wachache tunaofahamu wapi alikotokea kimuziki. Defao alianza kupata umaarufu mwanzoni mwa miaka ya 1980 akiwa na bendi ya Grand Zaiko Wawa iliyokuwa ikiongozwa na mchawi wa solo Felix Manuaku Waku. Hapa Defao na kundi zima la Grand Zaiko Wawa wanaporomosha live kibao Salima katika studio za televisheni ya taifa ya Zaire mwaka 1984. Amini, usiamini, Defao ni huyo mwimbaji wa kwanza kushoto. Shimita ni huyo wa pili kushoto aliyevaa nguo za bluu.
Last edited by a moderator: