madala mujipa
JF-Expert Member
- Feb 23, 2017
- 1,421
- 864
amani kwenu wadau
Nina jamaa yangu kama miaka miwili na nusu nyuma alikumbwa na kisanga cha mwaka baada ya mkewe kuja kumuachia mtoto mdogo wa mwaka mmoja na yeye kutokemea kusikojulikana
Baada ya hapo tulimpa moyo na ushauri ampeleke mtoto kwa bibi yake au kwa ndugu ili wamlee lakini wapi jamaa aligoma kabisa akawa asubuhi anamuandaa mtoto wake na chupa ya maziwa na uji wa ulezi tunapiga nae mishe kama kawaida baada ya muda anambadilisha pampers muda unakwenda
Hivi sasa mtoto amekua na anavutia sana chini ya uangalizi wa jeshi la mtu mmoja baba mtu eti ghafla juzi yule mwanamke ametokea kusikojulikana eti anataka kumuona mtoto na aondoke nae ,muda aliofika pale mtoto na baba yake walikua wamepata abiria wa kumpeleka safari yake tukamshauri amsubiri mzazi mwenzake
basi yule mwanamke akasema kuna sehemu anakwenda lakini hatochelewa...mara yule jamaa na mwanawe wakarudi tukamueleza ujio wa mama mtoto..nikamuona jamaa amebadilika sura ghafla na kusema si alijua amenikomoa sasa anataka nini tena..tukajaribu kumshauri amsikilize..yule mwanamke akarudi pale wakakutana lakini jamaa hakumtoa mtoto mama mtu amuone kiasi cha kutokea mzozo mkubwa tulichomshauri yule bibie ni kuwa aondoke aepushe shari lakini aligoma na jamaa nae kuona gozi gozi akamtia mtoto wake kwenye usafiri wakaondoka na hakurudi tena ,yule mwanamke kuona hakuna anaemjali akajiondokea zake.
Asubuhi jamaa anatuambia yule mwanamke ana kichaa yeye alimuachia mtoto mdogo alijua atashindwa kumlea lakini si huyo amekua
Dah dunia ina mambo yeye alijua amemkomoa lakini jamali amekua kwa kudra hata sisi wenyewe kijiweni hatuamini
jamani mkitupiwa watoto msipaniki ni kushukuru tu
Nina jamaa yangu kama miaka miwili na nusu nyuma alikumbwa na kisanga cha mwaka baada ya mkewe kuja kumuachia mtoto mdogo wa mwaka mmoja na yeye kutokemea kusikojulikana
Baada ya hapo tulimpa moyo na ushauri ampeleke mtoto kwa bibi yake au kwa ndugu ili wamlee lakini wapi jamaa aligoma kabisa akawa asubuhi anamuandaa mtoto wake na chupa ya maziwa na uji wa ulezi tunapiga nae mishe kama kawaida baada ya muda anambadilisha pampers muda unakwenda
Hivi sasa mtoto amekua na anavutia sana chini ya uangalizi wa jeshi la mtu mmoja baba mtu eti ghafla juzi yule mwanamke ametokea kusikojulikana eti anataka kumuona mtoto na aondoke nae ,muda aliofika pale mtoto na baba yake walikua wamepata abiria wa kumpeleka safari yake tukamshauri amsubiri mzazi mwenzake
basi yule mwanamke akasema kuna sehemu anakwenda lakini hatochelewa...mara yule jamaa na mwanawe wakarudi tukamueleza ujio wa mama mtoto..nikamuona jamaa amebadilika sura ghafla na kusema si alijua amenikomoa sasa anataka nini tena..tukajaribu kumshauri amsikilize..yule mwanamke akarudi pale wakakutana lakini jamaa hakumtoa mtoto mama mtu amuone kiasi cha kutokea mzozo mkubwa tulichomshauri yule bibie ni kuwa aondoke aepushe shari lakini aligoma na jamaa nae kuona gozi gozi akamtia mtoto wake kwenye usafiri wakaondoka na hakurudi tena ,yule mwanamke kuona hakuna anaemjali akajiondokea zake.
Asubuhi jamaa anatuambia yule mwanamke ana kichaa yeye alimuachia mtoto mdogo alijua atashindwa kumlea lakini si huyo amekua
Dah dunia ina mambo yeye alijua amemkomoa lakini jamali amekua kwa kudra hata sisi wenyewe kijiweni hatuamini
jamani mkitupiwa watoto msipaniki ni kushukuru tu
