Alexander Mnyeti amepata wapi utajiri wa kuinunua TCC CLUB ya Chang'ombe?

Kuna mahali inakatazwa kitajirika ndani ya mida mfupi?
Imewahi kusemekana humu kwamba Bundi ametua kwa Mheshimiwa Alexander Mnyeti aliyewahi kuwa mkuu wa mkoa wa Manyara wengi wameuhoji utajiri mkubwa alionao na ambao ameupata kwenye kipindi kifupi sana hawa hawamwamini mheshimiwa haki ya kuwa tajiri bali wanaamini kwamba utajiri huo ulitokana na matumizi mabaya ya madaraka.



Zipo taarifa kwamba Mh Mnyeti ameanza kuchunguzwa na Tume ya Haki za Binadamu na utawala bora hatuna matatizo kuhusu uchunguzi huo ila chini kwa chini inasemekana malalamiko dhidi yake yalipelekwa kwenye tume toka enzi za hayati Rais Magufuli ila hayakufanyiwa kazi kwa sababu zinazoeleweka baada ya mabadiliko ya uongozi wa nchi inaelekea kama uchunguzi huo ni wa kweli tuisihi tume itende haki ifanye uchunguzi wake kwa kina,weledi na umakini.



Wahusika wengi katika kashfa itakayojitokeza ni watu wenye ukwasi mkubwa na hulka ya kutumia milungula wanapindisha utendaji wa wahudumu wa serikali awali mfano wa aliyekuwa wakili wa serikali huko Manyara “mkware “Kishenyi imewahi kutolewa humu kwenye jamvi rushwa ya shilingi milioni tano (5,000,000) ilimuumbua.



Yako maswali mengi ambayo Mheshimiwa Mnyeti anastahili kuyatolea majibu mfano



1:-Je uwanja wa Gwambina huko wilayani Misungwi ulijengwa kwa gharama ngapi?



2:-Mkandarasi alilipwa kiasi gani?



3:-Je kodi husika ililipwa inavyostahili?



4:-Je kuna visima vingapi uwanjani pamoja na sehemu nyingine ambayo alijenga huo uwanja huko Misungwi?mkandarasi wa visima alilipwa shilingi ngapi?(usije ukasema ati oh sasa wamechukua maji-hapana).



5:-Kuna uhusiano gani kati ya kamdarasi hizo na migogoro iliyokuwepo Manyara wakati huo?



Tunaisihi tume itende haki uongozi ni dhamana tatizo wapo viongozi aina ya Mnyeti,Sabaya na wengineo ambao walijivisha ngozi ya uzalendo na kuumiza watanzania wenzao kumbe walikuwa wanamtumia marehemu aliyeondoka kwa faida zao wenyewe viongozi wa namna hii na washirika wao hawafai.



Watipeleka nchi yetu kwenye umafia tunaousikia upo kwenye nchi nyingine sisi tunasubiri kwa hamu matokeo ya uchunguzi wa Tume kusema ukweli hili suala linaonekana ni la Takukuru zaidi ila tusubiri tuone tume itakuja na majibu gani.Tunaendelea kufuatilia



Mwisho.



Wasalaam ni mimi “Nikune huku nikune kule “

View attachment 1826026

View attachment 1826027

View attachment 1826028
 
Watu wanaunganisha matukio.

Mnyeti na Sabaya ndio watu wa kwanza kujihusisha na biashara ya madiwani na wabunge.

Vile vile Mnyeti alikuwa Manyara, kwenye Tanzanite. Huko wa Magu walikuwa wanajibebea tu.
Jana nilikutana na mtu mmoja mwenyeji was Manyara....sikujua kuwa U Dc na U RC Mkoa kama MANYARA ni Lulu...!
 
Binafsi kila nikijaribu sikiliza hizo 'dhambi'za mnyeti naona Tu 'katajirika Sana kwa MDA mfupi'..

Kuna uporaji kafanya kwa wafanyabiashara?
Kuna watu aliwateka?
Alibaka?.
Alimzuia mtu kufanya biashara?

Nina Nina wasiwasi zaidi ya wivu na roho ya kwanini ...hakuna lolote lingine la maana..
Hata kwa Sabaya nami nilikuwa kama unavyo hisi..ila nilikuja amini muda ni hakimu.
Kuwa na subira boss,hawa vijana wa magufuli tuliwaamini lakinikumbe nyuma ya pazia ni washenzi tu
 
Watu wanaunganisha matukio.

Mnyeti na Sabaya ndio watu wa kwanza kujihusisha na biashara ya madiwani na wabunge.

Vile vile Mnyeti alikuwa Manyara, kwenye Tanzanite. Huko wa Magu walikuwa wanajibebea tu.
endeleeni kuunganisha tu huku yenu yakizidi kutengana.
 
Watu wanaunganisha matukio.

Mnyeti na Sabaya ndio watu wa kwanza kujihusisha na biashara ya madiwani na wabunge.

Vile vile Mnyeti alikuwa Manyara, kwenye Tanzanite. Huko wa Magu walikuwa wanajibebea tu.
Unachamba kuliko Asha Boko
 
Jana nilikutana na mtu mmoja mwenyeji was Manyara....sikujua kuwa U Dc na U RC Mkoa kama MANYARA ni Lulu...!
Manyara ni hot keki. Imagine Samia mwenyewe alisema, wakiyaona madini ndio yanaoneshwa wasipoyaona yanaibwa tu ingawa waliweka wanajeshi. Kwanza Magu genge lake lote aliliweka sehemu nzuri nzuri ili waibe, hakuna cycle ya Magu yoyote ambaye bado masikini.
 
Watz wengi nibwachuuzi,watz wengi wakipata pesa ni kyzichungulia kwenye acc na kujenga majumba ya kupangisha.
Lakini ukiwekeza kwenye vitu au fursa adimu wewe ni kimeo.
Naomba wenye vyombo tuache kyfuatilia hizi maana ni ushindi kwa CHADEMA kuona mtu wao mbaya anaadhibiwa.
Baada ya Sabaya iwe tu ni funzo kwa wengine kuwa tuwahudumie wananchi .

Sent from my Infinix X690 using JamiiForums mobile app
Yaani mtu kama ana tuhuma asichunguzwe kwa sababu atawapa kiki CHADEMA? Hii akili ya wapi hii. Mmejimilikisha nchi sasa?
 
Kupata pesa kwa muda mfupi hiyo inawezekana kwenye ulimwengu wa teknolojia.....
tusiishi maisha ya zamani sana....!
Sio vibaya akahojiwa atoe maelezo
 
Hapa naona kama kuna ukweli. Vijana wa Magu wote matajiri kwa sasa
Manyara ni hot keki. Omagine Samoa mwenyewe alisema, wakiyaona madini ndio yanaoneshwa wasippyaona yanaibwa tu ingawa waliweka wanajeshi. Kwanza Magu genge lake lote aliliweka sehemu nzuri nzuri ili waibe, hakuna cycle ya Magu yoyote ambaye bado masikini.
 
Binafsi kila nikijaribu sikiliza hizo 'dhambi'za mnyeti naona Tu 'katajirika Sana kwa MDA mfupi'..

Kuna uporaji kafanya kwa wafanyabiashara?
Kuna watu aliwateka?
Alibaka?.
Alimzuia mtu kufanya biashara?

Nina Nina wasiwasi zaidi ya wivu na roho ya kwanini ...hakuna lolote lingine la maana..
Ache kiherehere subiri kama ni kweli tume ifanye kazi yake zaidi ya hapo utakuwa hutendi haki
 
Back
Top Bottom