Alex Msama atimua Mhariri mtendaji (Dira) fisadi

Alex Msama atimua Mhariri mtendaji (Dira) fisadi

Kamanda Mlo

Member
Joined
Feb 9, 2012
Posts
10
Reaction score
4
Habari zilizotufikia wiki iliyopita zinadai kwamba mmiliki wa Gazeti la DIRA ya Mtanzania Alex Msama amemtimua Mhariri mtendaji wa gazeti hilo Charles Mulinda kwa madai kwamba ana uhusiano wa karibu na MAFISADI, tetesi hizo zikaendelea kutiririka kwamba Mhariri huyo hivi sasa ametimkia kwa MAFISADI. Hivi ni kweli? Anayejua undani wa sakata hili naomba atiririke hapa.
 
Jana nilikuwa kwenye kijiwe kimoja maeneo ya Kariakoo,nikasikia wanasema kwamba ametimuliwa na amejiunga na Gazeti la Mtanzania,sasa bado sijathibitisha madai haya kwa sababu ilikua jioni mida ya saa 12 lakini ndivyo inavyosemwa,lakini naendelea kufuatilia hilo nadhani kufikia jioni nitakuwa na jibu kamili.
 
That's why Dira hivi karibuni limekuwa hivyo lilivyo!!! hii fani ya habari Tanzania
imevamiwa sijui mwisho wake nini"
 
Habari zilizotufikia wiki iliyopita zinadai kwamba mmiliki wa Gazeti la DIRA ya Mtanzania Alex Msama amemtimua Mhariri mtendaji wa gazeti hilo Charles Mulinda kwa madai kwamba ana uhusiano wa karibu na MAFISADI, tetesi hizo zikaendelea kutiririka kwamba Mhariri huyo hivi sasa ametimkia kwa MAFISADI. Hivi ni kweli? Anayejua undani wa sakata hili naomba atiririke hapa.

Hizo habari zaweza kuwa za kweli au si za kweli, ila Msama Mwenyewe naye fisadi hajawalipa wafanyakazi wake mishahara wanamdai na sasa anahaha kujinasua na waandishi hao
 
mbona nasikia hata Martina Malira wa Tanzania Daima anapeleka kila andiko lake kwa Nape kabla hajaweka gazetini, ndio maana kwa sasa CHADEMA hawalitumii sana gazeti hilo maana hiyo habari wanayo siku nyingi. Taarifa za Dr Slaa zinapelekwa huko kwanza Nape azi edit ndio zitoke ndio maana mnaona siku hizi kama habari za viongozi hao zikitoka ni vurugu za kunukuliwa vibaya kwa kwenda mbele, je Ansbert Ngurumo analijua hilo na ataliweza?

Huyu Malira ndio yule mnakumbuka akiwa Tanzania Daima alikua anapewa machapisho na wakina Premi Kibanga na anayatoa kwenye Daima kama yalivyo, hakuna waandishi tuombe Mungu Seneta Kerry afanyie malalamiko ya watanzania kazi mapema Mwanahalisi lirudi, nashangaa serikali nzima kujiingiza kumlinda Zoka leo hii aibu kubwa na mungu asaidie viongozi wake wawekewe vikwanzo ndio mambo ya kukumbatiana yatakapokwisha.

Leo hii tazama wanavyohangaika na huyo Mulugo walikomtoa watajua wenyewe, Ramadhani Indogho hawezi ku survive, lazima atakumbwa na mob justice watu wanamnyamazia wakwemo very close wa kazini kwake lakini something is cooking, abadilishe ubini na watoto wake
 
habari za kutolipana mishahara ni tatizo kwa media house karibu zote kwani yeye msama nani asidaiwe?serikali yenyewe na mihela kibao inadai sembuse Msama?
 
Ndio maana waandishi wanapoonewa wengine tunashindwa kuwatetea,Waandishi ndio wanaoongoza kupotosha umma.Wengi wanafikiri siku moja watapata nafasi walizopata akina Salva! Mambo yanabadilika sana na huko tuendako vyeo vya kupeana kisiasa vitakwisha.

Waandishi jiheshimuni na mlinde maslahi ya umma ili jamii iwepe heshima mnayostahili badala ya vijiasante vya kinafiki kutoka kwa wataka madaraka.
 
Sio kweli msama hajamfukuza mulinda kazi mimi naujua ukweli wote hata kama mulinda anatumia na mafisaid. Huyo mullinda najiaharibia mwenyewe anatumiaka vibaya na msama amekuwa akimbeba muda mrefu na yeye mullinda kama mhariri mtendajia aliandika makala chafu sana ya kumtukana kamanda charles kenyela msama wala hakumfukuzua akamwambia kistaarabu na akawa anaendelea kufanya kazi.

Juzi kati kaandikiwa memo na meneja utawala ya kujieleza kuhusu utendaji wake na utoro kazini na mambo mengine na kutokuwa na vyeti vya uandishi wa habari maelezo hawamtambui msama akaambiwa amuondowe ila akawa hajamuondoa. Mullinda anapenda ubosi hapendi kuulizwa wala kuwa chini ya mtu ndio maana baada ya kujibu memo akaandika barua ya kuacha kazi.
 
Binafsi huwa siwaelewi kabisa watu wa fani hii... Ukisikiliza jinsi waandiahi wa kibongo wakimhoji kiongozi unaweza kutapika kama wewe ni makini. Anamhoji kwa kumbembeleza, maswali ya moja kwa moja na hamna swali linalotokana na majibu.

Rushwa ni mbaya sana.
 
mbona nasikia hata Martina Malira wa Tanzania Daima anapeleka kila andiko lake kwa Nape kabla hajaweka gazetini, ndio maana kwa sasa CHADEMA hawalitumii sana gazeti hilo maana hiyo habari wanayo siku nyingi. Taarifa za Dr Slaa zinapelekwa huko kwanza Nape azi edit ndio zitoke ndio maana mnaona siku hizi kama habari za viongozi hao zikitoka ni vurugu za kunukuliwa vibaya kwa kwenda mbele, je Ansbert Ngurumo analijua hilo na ataliweza?

Huyu Malira ndio yule mnakumbuka akiwa Tanzania Daima alikua anapewa machapisho na wakina Premi Kibanga na anayatoa kwenye Daima kama yalivyo, hakuna waandishi tuombe Mungu Seneta Kerry afanyie malalamiko ya watanzania kazi mapema Mwanahalisi lirudi, nashangaa serikali nzima kujiingiza kumlinda Zoka leo hii aibu kubwa na mungu asaidie viongozi wake wawekewe vikwanzo ndio mambo ya kukumbatiana yatakapokwisha.

Leo hii tazama wanavyohangaika na huyo Mulugo walikomtoa watajua wenyewe, Ramadhani Indogho hawezi ku survive, lazima atakumbwa na mob justice watu wanamnyamazia wakwemo very close wa kazini kwake lakini something is cooking, abadilishe ubini na watoto wake

Umeongea kwa kuchanganya madesa. Ila nikusaidie:

Ni kweli Martin Marela mhariri wa Tanzania Daima Jumatano huwa ana tabia hiyo ya kutoa siri kabla ya kuchapishwa gazetini tangu zamani. Aliwahi pia kutuhumiwa kumrekodi Deo Balile wakati akiwa Mhariri wa Mtanzania akizungumza kuhusu Reginald Mengi na Malera alimpelekea Mengi recording hiyo kumchongea Balile ili yeye apewe pesa na Mengi. Hii ni tabia yake siku nyingi kwa hiyo sishangazwi kama sasa anampelekea taarifa Nape kabla ya kuchapishwa.

Back to the thread.

Ni kweli Mulinda yuko New Habari na wiki iliyopita niliona safu yake ya MCHOKONOZI ikiwa katika Gazeti la RAI. Huyu jamaa (MULINDA) ndie aliyekuwa akiandika habari za akina Premi Kibanga na yule mwanaume wake tapeli anayejifanya usalama wa taifa ambaye alimfanya JK akazindue hoteli kule Arusha iliyojengwa kwenye hifadhi ya Barabara. Hakuwa Malera bali Charles Mulinda wa DIRA ambaye sasa ndio amehamia New Habari
 
Kwani Msama ni Muandishi au Ni mmiliki? Kwanini aingilie FANi ya watu? kisa pesa?
 
Martin Malera namfahamu tangu akiwa Don Bosco ile tabia ya umbea mbea kumbe imekua na kuchanua. Sasa hivi ni kama gear -box ya ufisadi. Ni informer wa MAFISADI. Hakika hatufiki mbali kwa mapambano dhidi ya Mafisadi. The right person is doing the wrong thing against the PUBLIC.
 
nikasikia wanasema kwamba ametimuliwa na amejiunga na Gazeti la Mtanzania

Ni kweli Mulinda yuko New Habari na wiki iliyopita niliona safu yake ya MCHOKONOZI ikiwa katika Gazeti la RAI.

Inaonekana habari corporation inazidi kujipanga kisawa sawa. Ngoja tuendelee kuiangalia hii move itaishia kwa nani baada ya Kibanda na Mulinda (hawa wawili walipata kuwa Tanzania Daima, wakawa wanamshambulia sana Mzee Sita)
 
Inaonekana habari corporation inazidi kujipanga kisawa sawa. Ngoja tuendelee kuiangalia hii move itaishia kwa nani baada ya Kibanda na Mulinda (hawa wawili walipata kuwa Tanzania Daima, wakawa wanamshambulia sana Mzee Sita)

Mkuu umetumia fasihi mambo leo. Ni mtu timamu tu kichwani atakayekuelewa. Laigwanan yupo very strategic
 
Inaonekana habari corporation inazidi kujipanga kisawa sawa. Ngoja tuendelee kuiangalia hii move itaishia kwa nani baada ya Kibanda na Mulinda (hawa wawili walipata kuwa Tanzania Daima, wakawa wanamshambulia sana Mzee Sita)

Umesema kweli mwita nakumbuka gazeti la TANZANIA DAIMA kwa siku za nyuma kila jumatano lilikuwa ni kumshambulia mzee sitta na washirika wake bungeni kupitia kwa charles mulinda, sasa angalau mwanga umepatikana baada ya yeye kujinga na kibanda new habari, hawa ni wamoja toka zamani
 
Binafsi huwa siwaelewi
kabisa watu wa fani hii... Ukisikiliza jinsi waandiahi wa kibongo
wakimhoji kiongozi unaweza kutapika kama wewe ni makini. Anamhoji kwa
kumbembeleza, maswali ya moja kwa moja na hamna swali linalotokana na
majibu.

Rushwa ni mbaya sana.
Nani kakuzuia kuwa mwandshi ili uwahoji maswali unayotaka? uandishi unaruhusu kila mtu kuingia, maana ni haki ya kila raia kutoa na kupokea habari
 
Msama mwenyewe msafi? Mbona yeye akila chake anawageuka wahariri?
Habari
zilizotufikia wiki iliyopita zinadai kwamba mmiliki wa Gazeti la DIRA ya
Mtanzania Alex Msama amemtimua Mhariri mtendaji wa gazeti hilo Charles
Mulinda kwa madai kwamba ana uhusiano wa karibu na MAFISADI, tetesi hizo
zikaendelea kutiririka kwamba Mhariri huyo hivi sasa ametimkia kwa
MAFISADI. Hivi ni kweli? Anayejua undani wa sakata hili naomba atiririke
hapa.
 
Back
Top Bottom