bless on
JF-Expert Member
- May 22, 2026
- 698
- 1,632
Siku moja, Albert Einstein alikuwa ndani ya treni akitoka Chuo Kikuu cha Princeton. Kondakta akaanza kupita kukagua tiketi za abiria mmoja mmoja. Alipomfikia Einstein, mzee akaanza kupekua mifuko ya koti lake tiketi haipo.
Akaingia mifuko ya suruali, akatafuta ndani ya koti lake dogo la safari, wapi! Hakuna kitu. Mwishowe akaanza kuitafuta hata kwenye kiti alichokuwa amekalia.
Kondakta alipoona vile, akamwambia kwa heshima
“Dr. Einstein, mimi nakujua vizuri. Kila mtu hapa anakujua, na nina uhakika kabisa ulinunua tiketi. Usiwe na wasiwasi, achana nayo.”
Einstein akaitikia kwa kichwa na kumshukuru. Kondakta akaendelea na kazi yake ya kukagua tiketi za abiria wengine. Lakini alipokuwa karibu kutoka nje ya lile behewa, alipiga jicho nyuma na kumuona Einstein amepiga magoti chini, bado anatafuta ile tiketi uvunguni mwa kiti.
Kondakta akashangaa, akarudi tena na kumwambia:
“Kama nilivyokwambia, kila mtu anakujua wewe ni nani. Hakuna shida kabisa. Huhitaji kuhangaika kuitafuta hiyo tiketi.”
Einstein akainua kichwa chake, akatabasamu na kumjibu,
“Asante sana rafiki yangu. Mimi pia najua mimi ni nani. Lakini shida ni kwamba, sijui naenda wapi! Ndio maana naitafuta hii tiketi kwa udi na uvumba nijue safari yangu inaishia wapi.”
Story hii inatufundisha kuwa Hata uwe na akili gani ya kutatua magumu ya ulimwengu, bado unaweza kukwama kwenye vitu vidogo kama kujua kituo unachoshukia!
Akaingia mifuko ya suruali, akatafuta ndani ya koti lake dogo la safari, wapi! Hakuna kitu. Mwishowe akaanza kuitafuta hata kwenye kiti alichokuwa amekalia.
Kondakta alipoona vile, akamwambia kwa heshima
“Dr. Einstein, mimi nakujua vizuri. Kila mtu hapa anakujua, na nina uhakika kabisa ulinunua tiketi. Usiwe na wasiwasi, achana nayo.”
Einstein akaitikia kwa kichwa na kumshukuru. Kondakta akaendelea na kazi yake ya kukagua tiketi za abiria wengine. Lakini alipokuwa karibu kutoka nje ya lile behewa, alipiga jicho nyuma na kumuona Einstein amepiga magoti chini, bado anatafuta ile tiketi uvunguni mwa kiti.
Kondakta akashangaa, akarudi tena na kumwambia:
“Kama nilivyokwambia, kila mtu anakujua wewe ni nani. Hakuna shida kabisa. Huhitaji kuhangaika kuitafuta hiyo tiketi.”
Einstein akainua kichwa chake, akatabasamu na kumjibu,
“Asante sana rafiki yangu. Mimi pia najua mimi ni nani. Lakini shida ni kwamba, sijui naenda wapi! Ndio maana naitafuta hii tiketi kwa udi na uvumba nijue safari yangu inaishia wapi.”
Story hii inatufundisha kuwa Hata uwe na akili gani ya kutatua magumu ya ulimwengu, bado unaweza kukwama kwenye vitu vidogo kama kujua kituo unachoshukia!