Alama hii inamaninisha nini?

zipalapwata

JF-Expert Member
Oct 19, 2016
283
146
Wadau leo ahsubuh nimewasha gari langu imetokea sign hiyoo kwenye dashboard inamanisha nn please
IMG_20190930_063823_9.jpeg
 
Nini maana ya ABS mkuu?
ABS ni mfumo wa braking (Anti Lock Braking).
Ambao kazi yake ni kusaidia gari kuweza kusimama kwa haraka zaidi na kupunguza utelezi wakati wa usimamaji.
Kuilezea ABS ni changamoto kidogo kwa sababu imekaa kifizikia zaidi, ila kwa haraka haraka elewa
1. kukanyaga brake wakati ukiwa kwenye speed, matairi yanalazimishwa yasitembee ila haimaanishi gari nalo litasimama wakati huo. Mara nyingi litateleza na kuacha alama za matairi kwenye barabara.
2. Ili gari likunje kona linahitaji matairi yawe yanatembea, kwa hiyo kama umekanyaga brakes unazuia matairi yasitembee, ki nadharia hutoweza kukunja kona hata kama umeyakunja matairi yaende uelekeo wa kona hiyo.
Ilikuondoa hizo changamoto mfumo wa ABS unakataza matairi yasitembee kwa wakati fulani na kuyaruhusu tena yatembee kidogo kwa muda kidogo hata kama ukiwa bado umekanyaga brakes.
Hiyo taa kuwaka maana yake, gari lako linahitillafu kwenye huo mfumo, brake zinaweza zikawepo na zikawa zinafanya kazi lakini mfumo wa ABS ndo utakua unakosekana
 
Back
Top Bottom