Al Shabaab yateka msikiti Garissa

Al Shabaab yateka msikiti Garissa

Status
Not open for further replies.

Ishmael

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2011
Posts
15,039
Reaction score
6,018
Viongozi Kaskazini mwa Kenya wamesema kuwa wapiganaji wa kundi la kigaidi kutoka Somalia la Al Shaabab waliuteka msikiti mmoja katika kaunti ya Garissa kwa masaa kadhaa.

Wapiganaji hao waliwahutubia waumini waliokuwa msikitini kwa karibu saa mbili kabla ya kutokomea mwituni.
Waliikosoa serikali ya Kenya na kuonya waumini dhidi ya kuwa majasusi wa serikali ya Kenya.

Mwezi uliopita Al Shaabab walivamia chuo kikuu cha Garissa na kuwaua watu 150 wengi wao wanafunzi.
150521104646__al_shaabab_waliuteka_msikiti_mmoja_katika_kaunti_ya_garissa_kwa_muda_na_kuonya_wenyeji_dhidi_ya_kuisaidia_serikali_ya_kenya_na_ujasusi_624x351_bbc_nocredit.jpg



Kundi hilo kutoka Somalia linaaminika kuwa na wafuasi nchini Kenya ambapo limetekeleza mashambulizi kadha katika jitihada ya kuilazimisha serikali ya Kenya kuondoa majeshi yake nchini Somalia.

Majeshi ya Kenya ni miongoni mwa kikosi cha kulinda amani cha muungano wa Afrika Amisom ambao wanaisaidia serikali dhaifu ya Somalia kupigana na waasi wa Al Shabaab.

Al Shabaab yateka msikiti Garissa - BBC Swahili
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom