Akaunti za Msekwa, Luhanjo zichunguzwe

kwa kweli mzee wetu kama kweli yalioandikwa kuwauzia wafanyabiashara sehemu zisizoruhusiwa kw a
njee zenu ama za ccm ama familia yako kwa kwli ni aibu sana sana mzee wangu....

Mkuu, unaweza kufafanua zaidi kwa faida yetu sisi ambao hatukupata bahati ya kusikiliza radio au kusoma magazeti?
 
au mkewe ndo an mrubuni kukwiba?
make wake wacheza midundiko kanga mpya kila wiki! mzee kupiga hesabu akaona haingii akaona aanze kupiga bei masalia! kweli Tamaa mbaya
 
huo uchunguzi ufanywe na nani? interpol or hawa wa bongo? halafu report apewe nani?
 
Kutokana na kuhusishwa na kashfa ya kutorosha nyara za taifa nje ya nchi kinyume cha sheria, kuna haja ya kuchunguza akaunti za vigogo hawa wawili ili sheria ichukue mkondo wake.

ufisadi wa hawa majamaa siyo utoroshaji wa nyara nje ya nchi tu upo kila mahali..................
 
Wabunge wamlipua Luhanjo wa Ikulu Send to a friend
Wednesday, 17 August 2011 20:18
0digg

08luhanjo.jpg
Katibu Mkuu Kiongozi Phillemon Luhanjo

WAMTUHUMU NDIYO CHANZO KIKUU CHA UFISADI MALIASILI NA UTALII, MWENYEWE ANG'AKA
Neville Meena, Dodoma
KAMATI ya Wabunge wa CCM imeendelea kuwa mwiba kwa Serikali baada ya jana baadhi yao kumtaja kwa jina, Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo kwamba ni chanzo cha ufisadi na uozo katika Wizara ya Maliasili na Utalii.
Wabunge hao wamemtaja Luhanjo ikiwa ni siku moja baada ya kukataa kufungwa mdomo katika kujadili Bajeti ya Maliasili na Utalii na kutaka iwasilishwe kwanza bungeni ili wapate fursa ya kuchangia kama wabunge wengine, kuliko kuwa na msimamo wa kichama katika kuipitisha bila kuijadili kwa kina na uwazi.

Jana, kamati hiyo ilikutana mnamo saa 7:00 mchana katika kikao ambacho kilichukua takriban saa mbili na nusu na kutoa maelekezo magumu yanayoitaka Serikali kuchukua hatua za kukabiliana na wizi, ufisadi na ubadhirifu wa mali ya umma unaofanywa kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii, inayoongozwa na Waziri Ezekiel Maige.

Maelekezo mengine yaliyotolewa na wabunge hao kwa mujibu wa taarifa ambazo zilipatikana ni kumtaka Waziri Maige kushughulikia tatizo la ukabila katika Idara ya Wanyamapori, kufutwa kwa vibali vya kukamata na kusafirisha wanyama hai nje ya nchi na kurejeshwa kwa wanyama waliotoroshwa na kupelekwa nje Novemba mwaka jana, kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho zilidokeza kwamba awali, wabunge hao walikuwa wametishia kukwamisha bajeti ya wizara hiyo kama walivyofanya ile ya Nishati na Madini, lakini waliridhishwa na ahadi za Serikali kwamba itachukua hatua stahili.

Kwa mujibu wa habari hizo, Luhanjo alitajwa kwa jina kwamba amekuwa chanzo cha utendaji mbovu katika Idara ya Wanyamapori iliyoko chini ya wizara hiyo kwa kushawishi uteuzi wa watendaji kwa misingi ya ukabila ili kulinda kile kilichodaiwa kuwa ni maslahi yake binafsi.

"Hata orodha ya watendaji wa idara hiyo ambao wanatoka kwa mheshimiwa huyo wa Ikulu imesomwa pale na tumeomba Serikali ichukue hatua, sasa watafanya nini watajua wao wenyewe," kilisema chanzo hicho cha habari na kuongeza:

"Idara hiyo ni nyeti na ndiyo inasimamia wanyamapori, sasa haiwezekani watendaji wake wote wakatoka sehemu moja tu ya nchi tena kabila moja, hapa tumenusa kitu na tumesema Serikali ikifanyie kazi."

Awali, wabunge hao walihusisha hata uhamisho wa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maimuna Tarishi kwamba ulilenga kulinda kile kilichodaiwa kuwa ni "maslahi ya Luhanjo" wizarani hapo lakini baadaye walijulishwa kuwa katibu mkuu huyo hakuwa sehemu ya mkakati huo.

Luhanjo aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, kabla ya kuhamishiwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Baada ya Rais Jakaya Kikwete kuingia madarakani alimteua kuwa Katibu Mkuu Kiongozi kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Martin Lumbanga ambaye sasa yuko Geneva, Uswisi akiiwakilisha Tanzania katika mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyoko nchini humo.

Luhanjo anena
Alipopigiwa simu kujibu madai hayo ya wabunge Luhanjo alionekana kupata taarifa hizo kabla ya kupigiwa simu kwani aliuliza: "Unaulizia hao wabunge waliokutana kwenye kikao na Waziri Mkuu siyo... sasa unasemaje?"

Baada ya kuulizwa juu ya tuhuma hizo alijibu kwa kifupi: "Sikubaliani na hoja zao hizo, si kweli ni majungu, achana na hiyo kitu bwana."

"Mimi ni Katibu Mkuu Kiongozi wa nchi nzima, sasa hayo mambo ya wizara mimi naingiaje huko, si kweli kabisa na mimi sikubaliani nao," alisema kisha kukata simu akijiepusha na kombora hilo.

Kamati ya Bunge
Mapema akisoma maoni ya Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, mwenyekiti wake, James Lembeli alisema kamati yake inasikitishwa na hatua ya Serikali kupuuza mapendekezo yake kuhusu suala la kufuatilia na kurejeshwa kwa wanyama waliotoroshwa nchini.

"Mapendekezo hayo ya kitaalamu yalilenga kuisaidia Serikali kuhakikisha upatikanaji wa wanyama hao. Ni jambo la kufedhehesha Mheshimiwa Spika, kuona kwamba tangu utoroshwaji wa wanyama hao ufanyike Novemba 24, 2010 hadi leo bado Serikali ilikuwa haijui wanyama hao wako wapi hali inayotia shaka na kuhoji kulikoni?," alisema Lembeli na kuongeza:

"Yapo maswali mengi ya kujiuliza kuhusu suala hili la utoroshwaji wa wanyama hao. Katika wanyama 116 waliotoroshwa wenye thamani ya Sh163,732,500 ni pamoja na twiga wanne. Kama ndivyo, Kamati inauliza kwa nini Sheria ya Wanyamapori inayozuia raia wa kigeni kupewa leseni ya kukamata wanyama wakiwamo twiga ambao ni nembo ya taifa haikuzingatiwa?"

Alisema hali hiyo inaashiria kuwapo kwa dalili kubwa ya uzembe na kulindana ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii na kwamba hicho ndicho chanzo cha kigugumizi katika kuchukua hatua.

Lembeli alisema shaka hiyo inajidhihirisha wakati wa uhamisho wa maofisa uliofanyika hivi karibuni na kwamba haukuwagusa kabisa wa kitengo cha Uwindaji wakiwamo wa Arusha na kuongeza kwamba licha ya kadhia hiyo ya kutorosha wanyama, baadhi ya maofisa hao wamepandishwa vyeo.

Kamati hiyo ya Bunge iliitaka Serikali kuwabaini wote waliohusika na kashfa hiyo na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola mara moja, huku ikipendekeza kuwepo kwa ofisa wanyamapori wa kudumu katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro ambacho nyara nyingi zinazosafirishwa nje hupitia.
 
[h=4]Comments [/h] 12345



0 #72 pedro 2011-08-18 23:54 kila bajeti ya wizara vinajitokeza vitu ambavyo misingi yake ni ufisadi,rushwa na uzembe,mhusika mkuu ni serikali,sasa wananchi tunangoja nini,peoples power ndio jibu,wenzetu india wana hanger strike,mgomo wa kula,sis tuanze na maandamano tu kuwaondoa wezi hawa,hakuna msafi
Quote









+3 #71 ahmed00 2011-08-18 21:38 NAPE MNAUYE yupo wapi kujibu tuhuma za boss wake? NAPE!kazi imekushinda au yupo likizo?
Quote









+1 #70 cowiti jl 2011-08-18 21:30 viongozi wengi wa serikali wamekosa maadili ya uongozi hivyo inaitajika ujasiri wa hali ya juu kuwatimua chakusikitisha ni pale rais anaposhindwa kusimamia serikali yake kikamilifu anapaswa kujifunza kulingana na migogoro zinazokabili nchi zingine za kiafrika
Quote









+1 #69 Nchichikwe 2011-08-18 21:17 Mhariri wa Mwananchi nakushanga sana. Kuhusu ardhi walitajwa Mkapa, Mwinyi, Macelela, Sumaye na wengine. Lakini ukurasa wako wa mbele ukaacha kumtaja Mwinyi. Uliporipoti majumuisho ya Tibaijuka ukamuacha. Je una maelekezo ya Ikulu kuwa usimtaje? Tuambieni. Nani aliuza Loliondo pamoja na marehemu Mgumia kama sio Mwinyi? Nani mke wake alitorosha dhahabu kama sio Mwinyi? Nani aliendesha serikali kiholela kama hii ya awamu ya nne kama sio Mwinyi? Nani aliyetuletea Kikwete aliyeshindwa kazi kama sio Mwinyi? Serikali mbovu ya Ali Hassan Mwinyi ndio leo imetufikisha kwa Kikwete aliyeshindwa kazi kabla ya muda wake. Kazi mbovu ya Kikwete imetufanya tushindwe kusimama kifua mbele na kuinadi CCM yetu. Tumeambiwa hivi sana ananda muislamu mwenzake aendeshe nchi na tumetajiwa Asha-Rose Migire na Hussein Mwinyi. Anaitumia turufu ya CUF kuwatisha wana CCM kuwa wasipomweka muislam upinzani na hasa CUF itachukua nchi. Mwinyi kijana wako anakusikiliza mtatupeleka pabaya.
Quote









+1 #68 MTETEZI 2011-08-18 20:38 Huyo Maige hana sifa za kuongoza wizara hiyo, yeye yupo hapo kwa kulinda maslahi ya vigogo. Angalia vitalu vya uwindaji ambavyo ni vinono amewapa wazungu na kampuni za Tanzania zimeambulia vitalu vibovu.

Kwenye misitu ndo usiseme wamepewa wazungu ndio wasimamie, hivi Watanzania hawawezi kutunza hiyo misitu kweli wakati wameilea mpaka ikafika ilipo hivi sasa, ukataji wa miti unasababishwa na serikali mbovu ya ccm kwani wananchi wanakosa nishati mbadala badala yake wanaendelea kutumia kuni na mkaa.

Kuhusu wanyamapori kuibiwa serikali ya ccm ilianza zamani kuruhusu wageni kutorosha wanyama kuanzia enzi za Mwinyi hivyo hiyo ni kawaida yao
Quote









+5 #67 NAOMBE MNISOME. 2011-08-18 20:04 Wadau wangu nendeni blog ys MICHUZI mkaangalie clip ya hotuba ya Nyerere siwafichi ni nearly one hour ila imenitoa machozi na maneno aliyotuachia yameshakuwa reversed 90 degree.Bora angeondoka ameshajua kuwa ameandaa genge la walanguzi kuingia IKULU.God bless his soul.sijui kwa nini Mungu alituzawadia mtu huyu harafu yakafuata mashetani tupu.WATANZANIA TUAMUENI MOJA.
Quote









0 #66 hahahahah 2011-08-18 19:29 safi kabisa m!!!!, yaani sema siwezi kukufaham ila laiti ningejuwa uliponingekuzaw adia zawadi, kwamaana mimi nimuathirika wahilo hawa wahifadhi hakuna mwenye imani hata kidogo baba yangu amekaa SERENGETI MIKUMI MKOMAZI TARANGIRE SAANANE, yaani mpaka nimemamliza chuo kikuu na tena tena kwamsaaada wa mjonba wangu ndio leo baba anapata kanyumba kakumstir, kiukweli hawa askari nishida kwakwenda mbele kwanza wanaishi maporini hakuna kufuga hata kuku tena kwasasa ndio balaaa yaani kuna marupurupu kibao hawalipwi yaani tena kwaubabe wamuhifadhi tu anaaamuwa,tena mimi naona hao wanaowasema nimafisadi hakuna kitu kama hicho hawajamaa mimi niongemuomba waziri aunde tume ya uchunguzi wa MALI ZA WAHIFADHI HAWJAMAA NIMATAJIRI ASIKWAMBIE MTU ninanamashaka sana na zile permit zinazokusanywa kwenye mahifadhi kama hawazichakachuw i sijuwi, MH WAZIRI MAIGE chonde chonde chunguza hawa viumbe na wasaidie hawa askari TANAPA ITADUMU
Quote









0 #65 mh!!!!! 2011-08-18 19:11 kiukweli mimi kilio changu nikwawale askari wa TANAPA, ktk wizara hii hawa viumbe ndio wanaopata tabu ya kutaka kuuwa na majangili hawa ndio wanaokoswa koswa na wanyama,hawa ndio wanaotumwa nahao mafisadi kuteka na wanyama na ikigundulika wanaofukuzwa kazi nihawa askari,chaaajab u nikwamba fedha zilizokuwa wanalipwa kama vile 9t za fedha za kuuguliwa kulazwa, fedha za doria kwasasa kunabaadhi ya hifadhi kwao imekuwa historia, wakati huohuo wahifadhi wao wakiendelea kuwa matajiri nawakizidi kujenga majumba ya kifahari na kutembelea magari kuliko waziri,ninaaami n kamwe ujangili wawanyama hautaisha kamwe kwasababu yakuwanyima na kuwanyanyasa hawa wanaowalinda hawa wanyama, haiwezekana TEMBO 10 wauwawe kwakipindi kifupi namna hiyo, MH waziri maige wacha kuagiza kama majeshini hiyo hiyo niasasi ya kiraia wafukuze watu maofisin musikilze shida za hao askari wanamaisha magumu wakati wizara yao ndio wizara tegemezi kiuchumi, yaani askari wa TANAPA mshahara nikichekesho hembu kuweni na roho ya huruma kwahawa watu, naninyi wahifadhi musilete mambo ya kpmbav ebooo zulma kama hamtakufa wapeni posho zao wakianza kuwinda ooo doria oooo patrol kwataarifa yenu hata ningekuwa mimi ningewinda mpaka nione wanangu wanaunafuu wamaisha eboooooo
Quote









+1 #64 hainiingiii 2011-08-18 18:51 chonde chonde mueshimiwa rais wetu kipenzi tunaaamini kwamba wewe unamapenzi mazuri na watz,kama kweli na wewe unatupenda nakuomba hawa wazee fukuzia mbali,mumempa makamba ukatibu mkuu amekyumbisha chama nusura kisambaratike na hiii nikutokana na mawazo yake yakizee na yakizamani,mzee kama hyuy yupo serikalini miaka 40 wanini tena,hawa ndio wanaosema TANZANIA NIWATU NA WATU WENYEWE NDIO SISI,wakikaa na mahawara yao hayo ndio maneno yao rais wangu mpendwa wanahodhi mali za watanzania kama sadaka kweli?kisa alitembelea nchi yake akapokelewa vizuri anatowa zawadi mali za watanzania,bora lawama kuliko fedheha watanzania wengi wasomi wameikimbia nchi kwa u[NENO BAYA] wa hao wazee wanaojivunia kuwepo kwao serikalin muda mrefu, mimi naaamini bado chama hakijaharibu kuihivyo,MH rais ukiona wabunge wako pia wamechoka hunabudi kukanaa nao nakusikiliza mawazo yao kwalengo la wananchi na chama kwaujumla,hawa nikuwafukuza tu nahakuna kitakacho haribika wapo vijana lakini sio kama wakina nape yule nae hana mana nje ya nchi kunavijana wengi sana wasomi na wenye uwezo ukilinganisha na kazi wanazofanya huko kwenye nchi zawatu,
Quote









0 #63 Mpechetula 2011-08-18 18:32 LUHANJO,basi lake ni la akina Mramba,Marcela na abiria wengine wa aina hiyo,kwakuwa kaachwa na basi hilo,apande la saa hii aende akapumzike hajachelewa.Kweheri babu bye!
Quote









+1 #62 Beano 2011-08-18 18:24 @Mwongozo
Si kweli. In initial stages watalindana, lakini once wamepatikana wawili watatu wa ku-join upinzani still wakiwa ndani the systema changes. Sidhani kama umeshajiuliza hali ingekuwaje kama upinzani usingekuwepo. Ikiwa leo CCM wanachekeana kiasi hiki wanapoiba na kuuza mali ya nchi, nani angetuambia ubaya wao? Unataka kuniambia umeshasahau mashinikizo ya upinzani yalivyoifanya serikali iachane na mpango wa kuilipa DOWANS wazi wazi?

Hili suala la ukabila na udini ni dhana ya kiupotoshaji inayotumiwa na CCM kulinda kitumbua chake
. Kama si mjanja wa kushtukia mambo mapema siku zote utawatukuza CCM tena wakati wanakuibia. Nikukumbushe mwaka 1995 aliyekuwa mkuu wa jeshi la polisi Omar Mahita aliutangazia umma kuwa amekamata kontena la visu na majambia na kuwa polisi wana ushahidi kuwa vimeletwa na chama fulani ili kuleta vita nchini. Mipini ya visu hivyo ilikuwa na rangi za bendera ya CUF na hiyo ilikuwa dhana ya kuwafanya wananchi wanyonge wa fikra waone kuwa CUF=VITA.

Leo hii kwa kutambua udhaifu wa kielimu wa watu wa mikoa ya pwani, CCM imekuja na sera ya UDINI. Hilo ni jambo lisilo na ushahidi kwani ukiondoa wao CCM hamna mpinzani aliyewahi kuwa na sura ya ki-DINI. Sasa wewe umepigia mstari kuwa VYAMA VINGI LAZIMA VITATUGAWA KWA MISINGI YA UDINI, UKABILA N.K

Inanishangaza huoni namna CCM imetugawa tayari, tena katika misingi mibaya na yenye kudhalilisha. Ndani ya CCM monopolization of power tuna two inhumane classes; WEZI NA WAIBIWAJI.

Wanachofanya CCM ni kuhakikisha rasilimali za nchi zinaishia mifukoni mwao huku wengine tukiwa tumetulia. Na hapo wanakuja na dhana ya AMANI NA UTULIVU. Tunafundishwa kuwa wanyenyekevu tunapoibiwa na hayo unayoyaita maono yatakayoletwa na upinzani ni lubricants za kulainisha akili zetu ili zisifanye kazi kwa kelele.

CCM ni janga la Kitaifa.

Quote









+1 #61 Mossad 2011-08-18 17:55 Wakati Luhanjo akiwa katibu wa wizara ya maliasili alimuweka GM wa plantation moja hivi nyanda za juu kusini kutoka kabila fulani ambao wana tabia ya kuwekana kwenye idara ya misitu, ss inakuwaje watu wengine kama mwongozo unataka kudanganya watu kuwa vyama vingi vitaleta ukabila. Hicho alichofanya yeye kilikuwa nini kama siyo ukabila?
Quote









-1 #60 mwongozo 2011-08-18 17:47 @beano
upinzani ukiwepo unafanya chama tawala walindane. wakipambana wenyewe kwa wenyewe ktk bunge la chama kimoja, maendelo hupatikana kwa kasi.

kesho nitatoa orodha ndefu inayoonesha advantages na disadvantages za single party system. nitafanya hivyo kwenye multiparty system vilevile.

msukumo unatokana na upinzani nakubali lkn wakiwa ktk chama kimoja watafanya hivyohivyo. historia inaonesha hivyo. katika disadvantages za vyama vingi ni WABUNGE WA CHAMA TAWALA HULINDANA DHIDI YA WAPINZANI.

on my side najua kuwa upinzani ni chachu ya maendeleo lkn nachukia sana UKABILA, UDINI, UKANDA nk.... vyama vingi lazima vitupeleke huko. nina ushahidi wa 100% kwa tafiti nilizo zifanya hapa nchini na afrika kwa ujumla. thats why nashauri tuwe na chama kimoja na watu washindane na kupasua mabomu humohumo. U HAV TO NOTE IT THAT: NACHUKIZWA NA UFISADI UNAOFANYWA NA BAADHI YA WATENDAJI SERIKALINI.
Quote









0 #59 Mossad 2011-08-18 17:44 Wizi na Ufisadi ni dhambi ambayo hakuna kiongozi yeyote wa CCM atakayeweza kuikwepa, na hiyo inatokana na mfumo uliojengeka ndani ya Chama hicho.
Nakushangaa wewe unayejiita mwongozo unaposema kuwa vyama vingi vitatugawa kidini, kikabila na kkanda..hizo ni fikra hasi zitokanazo na mgando wa fikra na mawazo pembenuzi. Hivyo vyote ulivyovitaja havipo ndani ya serikali ya CCM?. Hujui kuwa kila siku rais wako anahubiri udini au unadhani watu hawajui ni jinsi gani ukabila unavyotawala ktk nyanja mbalimbali ndani ya serikali ya CCM?. Mfano mdogo ni hicho kizee Luhanjo wakati akiwa katibu ktk wizara ya maliasili alimuweka General Manager wa kabila lake kutoka kanda fulani hapa Tanzania ambaye alikuwa anakusanya mapato na kiasi fulani kinatumwa kwake....U don need to use microscope to see how these pple ar stealing our Resources, use ur naked eyes Guy!.
Kwa Mtanzania anayeipenda nchi yake kwa sasa sio wakati wa kuhubiri ishu za ukabila, udini wala uchama, tunatakiwa tujaribu kutizama kipi ni kikwazo kinachoporomosh a uchumi wetu kila kukicha na nini chanzo kilichopelekea tuwe ktk umaskini huu tulio nao sasa na jinsi gani ya kutatua majanga hayo.
Tusitumie hili jukwaa kusambaza chuki zisizo na msingi.
Quote









+3 #58 Beano 2011-08-18 17:18 @Mwongozo
Vyama vingi kutugawa kikabila, kidini na vinginevyo huo ni mtazamo wako. Hujui unachoshangilia kitaishia wapi. Vyama vya upinzani ndio msingi wa vuguvugu lote hili unaloliona ndani ya bunge na nje kwenye utekelezaji. Huu uthubutu wa wabunge wa CCM katika kusema mabaya ya wenzao ni hofu ya kupoteza majimbo yao kwa wapinzani, (Hususan CHADEMA) Sasa usifikie sehemu ukasahau kuwa wanasema kwenye vikao vyao vya chama na sio panapostahili kusemea. Kwa mtazamo wangu haitoshi kushangilia kwani yataishia kusemwa ili yasikike kuwa yamesemwa na fulani lkn utekelezaji wake usiwapo.

Vyama vya upinzani ktk nchi yoyote ndio chachu na changamoto ya kuifanya serikali iwajibike. Jinamizi la CHADEMA mgongoni mwa CCM ndio linawafanya wabunge wa CCM kunyoosheana vidole na kamwe usifikiri those were their primary intentions when entering the house.

Pongezi zangu kwa wabunge wa CHADEMA kwani ni uwepo wao ndio umeamsha hamasa ya kumulika maovu miongoni mwa wana-CCM wabunge ambao hapo kabla hawakuwa na uthubutu na nia ya kufanya hivyo. Hakuna kitu CCM wanaweza kuamua bila shinikizo toka nje, na ndio maana nchi yetu inaibiwa hadi TWIGA.
Quote







12345
 
inawezekana wazo lako ni zuri lakin naweza kusema kuwa kwa serikali hii tuliyonayo halina maana..watu waekutwa na mabilioni wengine sasa matrilion lakin hakuna kinachofanyika zaid ya bra bra..kwani wote ni chungu kimoja! hatuna serikali ya kusimamia ufisadi nchi hii ..sasa tumesikia matrilion ya shimbo sijui nani atafuata...
 
wale tayari wako chini ya uangalizi, wanachunguzwa na kikosi kazi maalum, task force.

That is what we were told about EPA, Kagoda na mengine mengi..uchunguzi unafanyika, uchunguzi umekamilika, wamefikishwa mahakamani au hakuna ushahidi wa kutosha kuwafikisha mahakamani, au hawana kesi ya kujibu, au warudishe....kwa sasa kuna system nzuri iba iba iba...then tulia hakuna atakayekukamata. ila ukiiba kidogo kama laki 2 au 3 utakamatwa na kufungwa.
 
Kama umesikiliza redio za leo na kama umesoma magazeti ya leo kwa kweli ni huzuni kubwa sana sana katika watu ambao sikuwahi kufikiria kuhujumu uchumi wa nchi hii ni huyu mzee ..binafsi nilijua kikwete aliingia kwa fedha za rostam so huyu ukimwita mhujumu sishangai..ila huyu babu amenishtua wandugu

kwa kweli mzee wetu kama kweli yalioandikwa kuwauzia wafanyabiashara sehemu zisizoruhusiwa kwa njee zenu ama za ccm ama familia yako kwa kwli ni aibu sana sana mzee wangu

nimebaki najiuliza kama wewe upo kwenye list ya wale wale mze wangu uko ccm nani wasafi jamani??

Mbona mnatia aibu ccm shame on you aibu kabisa jamani

Mwenyekiti wa CCM, Mh. Jakaya Kikwete, ana mamlaka, uwezo na wajibu wa kumfunga paka kengele.

Naamini kuwa JK ana machungu na raslimali za nchi yetu, kama tulivyo sisi wananchi. Kama ni kinyume chake, Mwenyezi Mungu yupo, inshallah!
 
Hivi ile account ya wale jamaa wa majeshi kule off shore imefika wapi? ni kama trilioni tatu sijui? Ambayo ilikuwa walipwe wapiganaji wetu? sijamsikia tena yuele mzee S. H. I. M. B-----akizungumzia hilo.
 
wazee wanang'ang'ania vyeo, kwani hamkujua kuwa cheo ni dhamana?????????????
 
Du ama kweli What comes around goes around,Bado mengi sana yanakuja,hukumu nayo nani?
 
Kama umesikiliza redio za leo na kama umesoma magazeti ya leo kwa kweli ni huzuni kubwa sana sana katika watu ambao sikuwahi kufikiria kuhujumu uchumi wa nchi hii ni huyu mzee ..binafsi nilijua kikwete aliingia kwa fedha za rostam so huyu ukimwita mhujumu sishangai..ila huyu babu amenishtua wandugu

kwa kweli mzee wetu kama kweli yalioandikwa kuwauzia wafanyabiashara sehemu zisizoruhusiwa kwa njee zenu ama za ccm ama familia yako kwa kwli ni aibu sana sana mzee wangu

nimebaki najiuliza kama wewe upo kwenye list ya wale wale mze wangu uko ccm nani wasafi jamani??

Mbona mnatia aibu ccm shame on you aibu kabisa jamani

Ndiyo maana tunasema kama chama cha magamba hakikuondoka madarakani nchi hii inakokwenda ni kuzimu. Hawa jamaa hakuna mwenye nafuu na wanalindana katika kuimaliza nchi huku walio wengi wakifa kwa umaskini. Na sasa hivi hawaoni wala kusikia maana ufisadi umeshawapofusha macho na akili zao. Haiingii akilini kama mtu mdogo kama mkurugenzi wa wanyama pori anaweza kuwa na ubavu wa kuchukua wanyama pori na kuwasafirisha all the way kutoka mbugani mpaka kia na kuwaingiza kwenye ndege wanyama kama faru, twiga na wengineo yeye kama yeye, na idadi kubwa kama hiyo ya wanyama mpaka wenye nembo ya taifa hili bila kweli kuwa na wakubwa nyuma yake???
haiingii akilini jamani haiingii akiliniiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii. Na wakubwa kabisa wamo, wamo, wamo. Na ndiyo maana katika serious issue kama hii leo mtu anasimamishwa kazi na malipo yake pale pale. Sielewi wala haieleweki, Maskini Tanganyika!!!!!!!??? Nikiona mtu anaishabikia ccm natamani nim.......................
 
Kutokana na kuhusishwa na kashfa ya kutorosha nyara za taifa nje ya nchi kinyume cha sheria, kuna haja ya kuchunguza akaunti za vigogo hawa wawili ili sheria ichukue mkondo wake.

Lakini wewe si ni ccm? sasa wachunguzwe ili iweje? na unayetaka achunguzwe si ni makamu mwenyekiti wa chama! manake yake nini? Na waliokwisha kuchunguzwa wako wapi?
Kuna ubovu katika chama na uongozi mzima na ili hamtaki kulibali endeleeni hivyo hivyo mpaka mtakapoambiwa nchi imeuzwa na mnatakiwa mhamie somalia ndo mtalijua jiji
 
Back
Top Bottom