Ajira za utumishi kizungumkuti!

Ajira za utumishi kizungumkuti!

Hedex

Member
Joined
Jun 15, 2015
Posts
26
Reaction score
11
Habari zenu waungwana!

Mwezi wa saba hawa jamaa wa utumishi walichukua dodoso kwa baadhi ya wanafunzi wachache wa mwaka wa mwisho wenye ufaulu mzuri pale IFM. ambapo walipigiwa simu kwenda kujaza hizo dodoso na baadhi yao walishafuatiliwa taarifa zao kwa wadhamini waliowajaza ktk hzo dodoso.

Ila tunaona sasa imekua kimya mpaka leo na hakuna taarifa zozote wala aina za kazi ambazo zilikuwa zikitakiwa, Naomba kama kuna yeyote mwenye taarifa kuhusiana na hao jamaa atujuze!!!
 
Habari zenu waungwana!

Mwezi wa saba hawa jamaa wa utumishi walichukua dodoso kwa baadhi ya wanafunzi wachache wa mwaka wa mwisho wenye ufaulu mzuri pale IFM. ambapo walipigiwa simu kwenda kujaza hizo dodoso na baadhi yao walishafuatiliwa taarifa zao kwa wadhamini waliowajaza ktk hzo dodoso.

Ila tunaona sasa imekua kimya mpaka leo na hakuna taarifa zozote wala aina za kazi ambazo zilikuwa zikitakiwa, Naomba kama kuna yeyote mwenye taarifa kuhusiana na hao jamaa atujuze!!!

Tulia wewe kuna watu wanaufaulu mzuri na wana miaka zaidi ya 3 mtaani hawana ajira wewe hata cheti hujapata unalilia........!!
 
ulichoongea ni kweli....hata mwaka 2013 walikuja wakawafanyia usaili washkaji tuliokuwa tukisoma nao hapo IFM....waliwafanyia kama 8 hivi wa IT...nafahamu kwa kuwa nilisoma IT pia ...washkaji wakajua washalamba ajira tayari wanasubiri kuitwa...hadi leo hakuitwa hata mmoja....endelea kusubiri ukiitwa bahati yako
 
Jitahid kuwa na subira, mbona kiherehere hvyo!!
 
Kwa taarifa yako hao sio utumishi unaowafikiria wewe,Utumishi gani unaopigwa simu ukajaze dododso bila kuomba kazi?,utumishi gani ambao taarifa za mjazaji dodoso zinafuatiliwa kwa wadhamini?,Jiongeze wewe la sivyo utaipoteza hiyo nafasi,hao jamaa wanaweza kukufuatilia hapa hadi wakakubaini licha ya kutumia ID fake na hapo ndo utakuwa mwisho wako....
 
Sawa wakuu nilikuwa nauliza tu Maana hakuna info zozote Anyway michakato mingine iendelee!!
Asante.
 
Hata mwaka jana UDOM walikuja na kuna vijana walibahatika kuchukuliwa ila taifa hili kubwa sab hata sijui walipelekwa wapi.
 
Ha ha ha ha nmecheka aiseee.....hao jamaa watakuchukua wakikuona unafaa.
 
Back
Top Bottom