Ajira za uhamiaji zapelekwa JKT

Ajira za uhamiaji zapelekwa JKT

mukandala

Member
Joined
Aug 23, 2014
Posts
5
Reaction score
0
Kutokana na urasimu, ubadhilifu na utapeli uliojitokeza katika mchakato wa kuajiri nguvu kazi katika idara ya uhamiaji, imebainika dhahiri kwamba hata utendaji kazi wao ungefanana moja kwa moja na yale yaliyojitokeza katika kupatikana kwao.

Kamati ndogo iliyoundwa ilipendekeza mchakato wa ajira hizo ufanywe na wizara. Hata hivyo, hiyo imeonekana sio suluhisho bali ni kuongeza tatizo kwani viongozi wengi wa wizara pia wanna ndugu na jamaa zao ambao wanatamani waajiriwe katika idara hiyo.

Pamoja na hayo, idara husika ya uhamiaji ipo chini ya wizara hivyo viongozi na mambo huenda yakawa yaleyale. Ili kuepusha yote hayo, imependekezwa kuwa ajira hizo zipelekwe kwa vijana wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwani kuna wengi wenye sifa na uwezo mkubwa wa kufanya shughuli hizo.
 
EEEEENH!

walioko uraiani huku ndio imekula?
 
Serikali yetu inapenda sana majibu mepesi mepesi. Hiki i kitendo cha kutibu tatizo kwa kutengeneza tatizo jingine.
 
Walishindwa ni ni zoezi hili kulipeleka JKT toka mwanzo? Na he? Ndivyo utaratibu wa waizara ulivo?
 
...silly decisions aise.., yaani nchi ya kise*la kweli hii... Kwahiyo na sisi mliotumwaga na kusema tusubiri mpaka TANGAZO lingine la AJIRA inakuwaje?
 
walichofanya ni kiini macho waliolalamikiwa ni wale waliopitishwa juzi wao wameenda kuwashugurikia makonstebo na masajenti ambao tayari walishamaliza mafunzo kwa kifupi wale sabini hawajaguswa bado na bado wako ofisini wanapeta
 
Tatizo kila kiongozi ana watu wake na nafasi ni chache hivyo kuna ndugu wa wakubwa watakosa. Wanaogopa kulipuana
 
...JKT, MAGEREZA, JWTZ, UHAMIAJI, MGAMBO, hapo kila KITENGO kinajitegemea... Sasa kama mnafanya UZANDIKI kwa kupasiana wenyewe kwa wenyewe tena kutoka VITENGO tofauti haina uhalali hata kutuambia uhamiaji kuna NAFASI za AJIRA.
 
walichofanya ni kiini macho waliolalamikiwa ni wale waliopitishwa juzi wao wameenda kuwashugurikia makonstebo na masajenti ambao tayari walishamaliza mafunzo kwa kifupi wale sabini hawajaguswa bado na bado wako ofisini wanapeta

....yaani INAUMIZA kweli kuona MAAMUZI yameegemea UPANDE huu tu,.. Kama UMEWAFUTILIA ajira zao hata waliofuzu kwa JUHUDI zao iweje wale WAKAGUZI wasaidizi Nafasi zao hazikufutwa!!
 
....SAUTI za waliopita KIHALALI zinazimwa kwa kisingizio cha MCHAKATO eti haukuwa SAHIHI... Tunawashukuru Kwa KUZIMA sauti zetu... Yote MAPITO tu.
 
du kila kitu kikipelekwa JKT, sisi mtaani tutakoma.

...myself sioni tena haja ya kukaa na vyeti,.. kusoma UMESOTA mpaka kufikia point angalau unapokea cheti, KAZI unasotea halafu kibaya zaidi majitu kama ya UHAMIAJI yanakuletea KIGUNDU eti japo UMEFUZU usahili na kuitwa kwenye AJIRA halafu unafutwa kwa kuambiwa haikuwa HALALI..
 
Back
Top Bottom