Ajira Portal

Ajira Portal

Tuchki

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2017
Posts
1,740
Reaction score
1,446
Habari wanajukwaa samahani kwa wenye uzoefu wa ajira portal wanisaidie maana kila nikiomba kazi siitwi hata kwenye interview na kila mara najaribu kuapply.

Mnaoitwa kwenye interview mnatumia mbinu gani mnisaidie maana umri unaenda na mimi nataka niajiriwe serikalini.
 
Habar wanajukwaa samahani kwa wenye uzoefu wa ajira portal wanisaidie maana kila nikiomba kazi siitwi hata kwenye interview na kila mara najaribu kuapply.
Mnaoitwa kwenye interview mnatumia mbinu gani mnisaidie maana umri unaenda na mimi nataka niajiriwe serikalini
Tuma picha tuone muonekano wa profile yako tuanzie hapo
 
Habar wanajukwaa samahani kwa wenye uzoefu wa ajira portal wanisaidie maana kila nikiomba kazi siitwi hata kwenye interview na kila mara najaribu kuapply.
Mnaoitwa kwenye interview mnatumia mbinu gani mnisaidie maana umri unaenda na mimi nataka niajiriwe serikalini
Ww itakuwa unaikumbuka portal kipindi nafasi zimetangazwa unakuwa na wenge hyo inatakiwa ijazwe taratibu tena sasa hv ndio ngumu kuliko zamani maana ukikosea option ya kufuta ngumu unatakiwa umakini na usisahu Ku verify vyeti vyako toa copy peleka mahakamani pamoja na original zako zile copy zitakazo kuwa verified ndio unazi upload,
 
Ww itakuwa unaikumbuka portal kipindi nafasi zimetangazwa unakuwa na wenge hyo inatakiwa ijazwe taratibu tena sasa hv ndio ngumu kuliko zamani maana ukikosea option ya kufuta ngumu unatakiwa umakini na usisahu Ku verify vyeti vyako toa copy peleka mahakamani pamoja na original zako zile copy zitakazo kuwa verified ndio unazi upload,

Mahakama ipi mkuu
 
Wanakupa sababu gani yakutokukuita ?

Kikawaida kama umefanikiwa kutuma maombi wanatakiw kukujibu ni kwann hawaja ku shortlist kwenye interview na mara nyingi wamekuwa wakifanya ivyo! na kama hawajakujibu niwajibu wako kupiga helpdesk kuuliza kwanini hujaitwa!
 
Wanakupa sababu gani yakutokukuita ?

Kikawaida kama umefanikiwa kutuma maombi wanatakiw kukujibu ni kwann hawaja ku shortlist kwenye interview na mara nyingi wamekuwa wakifanya ivyo! na kama awajakujibu niwajibu wako kupiga helpdesk kuuliza kwanni ujaitw!

Sawa
 
Wanakupa sababu gani yakutokukuita ?

Kikawaida kama umefanikiwa kutuma maombi wanatakiw kukujibu ni kwann hawaja ku shortlist kwenye interview na mara nyingi wamekuwa wakifanya ivyo! na kama awajakujibu niwajibu wako kupiga helpdesk kuuliza kwanni ujaitw!

Mara nyingi naambiwa sijaqualify mpaka nimekata tamaaa jamani
 
Ajira portal saivi wapo serious...
1. Hakikisha profile yako umejaza vizuri. Kila kipengele ukijaze yaani profile ifike angalau asilimia 80.
2. Hakikisha vyeti vyako vipo verified na mwanasheria.
3. Pitia page kila siku... mara nyingi wanaowahi kuapply ndo chance kubwa ya kuitwa.
4. Weka CV current
5. Sehemu ya picha hakikisha ina picha yako official... yaani presentable.
6. Barua ya kuombea kazi lazima iwe official. Iwe na anuani yako na ya utumishi bila kisahau kutia sahihi... yaani kama huwezi mambo ya kuprint na kuscan tengeneza e-signature.
Barua zisizo na signature hazipewi kipaumbele.
7. Hakikisha kazi unayoomba unakidhi vigezo
8. Sasahivi wanataka uweke na namba ya NIDA
9. Maombi kwa Mungu wako ni muhimu zaidi.
 
Ajira portal saivi wapo serious...
1. Hakikisha profile yako umejaza vizuri. Kila kipengele ukijaze yaani profile ifike angalau asilimia 80.
2. Hakikisha vyeti vyako vipo verified na mwanasheria.
3. Pitia page kila siku... mara nyingi wanaowahi kuapply ndo chance kubwa ya kuitwa.
4. Weka CV current
5. Sehemu ya picha hakikisha ina picha yako official... yaani presentable.
6. Barua ya kuombea kazi lazima iwe official. Iwe na anuani yako na ya utumishi bila kisahau kutia sahihi... yaani kama huwezi mambo ya kuprint na kuscan tengeneza e-signature.
Barua zisizo na signature hazipewi kipaumbele.
7. Hakikisha kazi unayoomba unakidhi vigezo
8. Sasahivi wanataka uweke na namba ya NIDA
9. Maombi kwa Mungu wako ni muhimu zaidi.
Haya yote 9 mkuu 10 ni kuomba Mungu tu maana wale Sasa hivi hawatabiriki😁😁
 
Yaani Sasa hv watu wamekuwa na wasiwasi wa kutoitwa Interview reasonz zimekuwa nyingi sana.

Mara hujatimiza miaka 18, mara huna namba ya kadi ya CCM, mara unaambiwa hujakidhi vingine kwa kuwa hujaolewa au hujaoa yaani ni visanga tu🤣🤣🤣
Hiyo kuomba Mungu nimeiweka namba 9 mkuu maana unaweza fanya yote na bado hola...
 
Na mkaka wa watu ana 32
Duuh wamemuonea kabisa,, Leo nimeona kwenye page yako Facebook wamepost zile sheria zao.. kiukweli watu wamewashambulia sana, tena zaidi wamelalamika kuhusu kukatwa majina yao hzi Ajira za TRA..
Ila hata hawajibu Comments
 
Back
Top Bottom