Stroke
JF-Expert Member
- Feb 17, 2012
- 38,561
- 48,909
AJIRA NGUMU JAMANI!!!!! Jamaa m1 alienda kuomba kazi kwenye ZOO. Akaambiwa nafasi ya kazi ipo, hatuna sokwe. " Hivyo utajifanya Sokwe na tutakupa ngozi utavaa" Jamaa siku ya kwanza akavaa walipokuja watalii mambo yalienda vizuri. Siku iliyofuata banda lake liliwekwa kwa juu ya banda la simba. Jamaa katika kuongeza ongeza mbwembwe akawa anarukaruka, kwa bahati mbaya si akaangukia ndani ya banda la simba. . Akawa anapiga kelele " mamaa, nakufaa" mara yule simba akamwambia, " Acha ufala wewe, keele za nini sasa? mi mwenyewe binadamu, rudi kwenye banda lako kabla watalii hawajaja watatushtukia bure!!!