Ajira: Mdada Wa Kazi

Ajira: Mdada Wa Kazi

Duh, elfu 50 masharti yote hayo mkuu, pandishapandisha walau laki kwa kuanzia ndiyo maana hawa wadada hawaishiwi visa kwa sababu mnawakandamiza mno kwenye maslahi..,.
 
Du,masharti mengi mshahara mdogo sasa hivi hata wao wamepandisha mishahara yao la sivyo utampata ila ujue anaweza kukuibia
 
Duh, elfu 50 masharti yote hayo mkuu, pandishapandisha walau laki kwa kuanzia ndiyo maana hawa wadada hawaishiwi visa kwa sababu mnawakandamiza mno kwenye maslahi..,.
hayo masharti au vigezo/majukumu ya kazi?
 
Mkuu hujaelewa... tenn ni huyo mume na mke means walioana ndoa ya mwendokasi! Me namshauri huo mshahara wa 50,000 autunze mtoto akizaliwa wamfanye mfanya kazi wa ndani wawe wanamlipa huo ili umsaidie akifikisha umri wa mahitaji!
mtoto anafixed account yake-Azania Bank,nashukuru kwa ushauri wako.

Mshahara ndio huo,ndugu.
 
mtoto anafixed account yake-Azania Bank,nashukuru kwa ushauri wako.

Mshahara ndio huo,ndugu.

Unajua kuna watu mnaishi kufanya wengine madekio ya anasa zenu? Yaani mfumuko wa bei na maisha kuzidi kuwa ya gharama mnaona sawa tu ila mshahara wa House girl ubaki fixed tokea utawala wa Mzee Mwinyi eti? Ndo maana watoto wataishia kuwekwa kwenye fridge na mashine za kufulia...Na jinsi shule za kata zimepamba moto utasubiri sana kipindi cha likizo upate wa part time!
 
Duh, elfu 50 masharti yote hayo mkuu, pandishapandisha walau laki kwa kuanzia ndiyo maana hawa wadada hawaishiwi visa kwa sababu mnawakandamiza mno kwenye maslahi..,.
Hata ukiwapa hiyo laki haisaidii. Visa havikosekani, kama si hili, lile. Ni ngumu kujua nini wanataka. Labda uwalipe na kazi zote ufanye mwenyewe, ukiwa watoto ndio balaa.
 
Unajua kuna watu mnaishi kufanya wengine madekio ya anasa zenu? Yaani mfumuko wa bei na maisha kuzidi kuwa ya gharama mnaona sawa tu ila mshahara wa House girl ubaki fixed tokea utawala wa Mzee Mwinyi eti? Ndo maana watoto wataishia kuwekwa kwenye fridge na mashine za kufulia...Na jinsi shule za kata zimepamba moto utasubiri sana kipindi cha likizo upate wa part time!
mbona unatokwa povu kiasi hiki,wewe kama uhitaji au sio mtafuta kazi unapiga kimya!Kuna watu mpo kwajiri ya kucrush nakujifanya kujua sana.
 
mbona unatokwa povu kiasi hiki,wewe kama uhitaji au sio mtafuta kazi unapiga kimya!Kuna watu mpo kwajiri ya kucrush nakujifanya kujua sana.

Uwaombe radhi wenye watoto amabao unataka kuwaharibia future za watoto zao kwa mshahara wa 50,000...mgawanyo wa fedha hiyo kwa mwezi ni sawa na sh 1666.67 kiwango ambacho hakikutoshi hata mlo wa mbwa kwa siku...jifunzeni uungwana, siku moja mwanao anaweza kuwa mtumishi wa nyumbani as well!
 
Habari wanajamvi
Natafuta mdada wa kazi,

Sifa/Majukumu:
*Awe mwenyeuhitaji wakazi
*Athamini kazi yake na asi-ifanye kwa mazoea,siku zote.
*Mchapakazi
*Ajue kupika vyakula mbali mbali na kuaanda juisi/maji safi ya kunywa.
*Awe Msafi binafsi na msafi wa nyumba
*Awe msikivu,muelewa na asiwe mtu wakuzurula au ushirika na watu pasipo nasababu za msingi.
*Ajue kusoma na kuandika
*Awetayari kufanya kazi kwa muda wa zaid ya miaka miwili.
*Asiwe mtu wa magenge/maneno na porojo.

Mazingira ya kazi:
*Eneo😀ar Es Salaam,Mbezi Beach
*Nyumba wanaishi mke na mume(vijana)
*Uwezekano wa mtoto siku za mbele,hivyo awe tayar kusaidia katika shughuli za hapa na pale zinazohusiana na mtoto.

Mshahara:
*Elfu hamsini Kwa Mwezi

Kwa mwenye ndugu au jamaa au anayepatikana humu,na ana uhitaji naomba ani-PM.
Pamoja na sifa zote hizo mshahara elfu 50 tu. Nyinyi ndo mnaowageuza watoto wa wengine watumwa. Ebu zaaa wakwako umwajiri kwa elfu 50. Nawachukia sana ninyi mnaowageuza wezenu mapunda. Hapo utakuta adi chupi yako anakufulia
 
Uwaombe radhi wenye watoto amabao unataka kuwaharibia future za watoto zao kwa mshahara wa 50,000...mgawanyo wa fedha hiyo kwa mwezi ni sawa na sh 1666.67 kiwango ambacho hakikutoshi hata mlo wa mbwa kwa siku...jifunzeni uungwana, siku moja mwanao anaweza kuwa mtumishi wa nyumbani as well!
hivi ulielewa maana ya hii post?,sikiza sihitaji mdada wa kazi ambaye ana mtoto tayari!
 
Pamoja na sifa zote hizo mshahara elfu 50 tu. Nyinyi ndo mnaowageuza watoto wa wengine watumwa. Ebu zaaa wakwako umwajiri kwa elfu 50. Nawachukia sana ninyi mnaowageuza wezenu mapunda. Hapo utakuta adi chupi yako anakufulia
unakuta mtu kama wewe hunakazi...
let me give you one principle, everyone has price...so ukioni wewe haikufit,piga kimya!
 
MTU mwenyewe unaonekanaa mbabeee wakati unashidaaa ya kupataa msaidiz wakazi
 
Pamoja na sifa zote hizo mshahara elfu 50 tu. Nyinyi ndo mnaowageuza watoto wa wengine watumwa. Ebu zaaa wakwako umwajiri kwa elfu 50. Nawachukia sana ninyi mnaowageuza wezenu mapunda. Hapo utakuta adi chupi yako anakufulia
mkuu,umepata mchumba uliyekuwa unamtafuta kwenye ile thread
 
Back
Top Bottom