Naomba wana JF wanisaidie kufahamu, inakuwaje maiti zote za ndege ya yemen air zinapatikana visiwa vya mafia tu na sio sehemu nyingine? au visiwa hivyo vina nguvu za giza? majibu ya kisayansi ni bora zaidi.
We Kaitaba vipi ndugu yangu?
Unataka majibu ya Kisayansi wakati unauliza kitu ambayo si cha kisayansi?
We Ulitaka hao marehemu wapatikane wapi ndo uone hakuna ulozi??
Ajali ni ajali ndugu yangu, ondoa imani za kiswahili kwenye hii mambo haya.
Kwanini maiti zisipatikane zanzibar, mombasa, yaani zisambae pwani mbali mbali, cha ajabu zote zinapatikana mafya, na muda mfupi uliopita vipande vya ndege navyo vimepatikana mafya, kulikoni mafya?
Mafia ni karibu zaidi ya Comoro kuliko Zanzibar na Mombasa na iko kwa sababu ya pepo za Kusi (southern monsoon) ndio maana baadhi maiti na mabaki ya ndege yameonekana Mafia.