AJALI ZA BARABARANI NA MAGARI YA SERIKALI NCHINI TANZANIA KUNA NINI?

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Mwezi Mei 21 2018, watu watatu walifariki kutokana na ajali ya gari mali ya kituo cha Uwekezaji(TIC) cha Tanzania, huku uchunguzi wa Polisi ukibainisha kwamba chanzo cha ajali kilitokana na mwendo kasi wa gari uliosababishwa na dereva wa gari hilo.

Julai 29 2018, gari la Wizara ya Viwanda na uwekezaji lilipata ajali wakati dereva wa gari hilo akiwakwepa watembea kwa miguu wawili. Watu wawili walifariki huku wengine kadhaa wakipatwa na majeraha.

Agosti 4 2018, Waziri wa Mali asili na Utalii Dk Khamis Kigwangalla, alipata ajali mbaya iliyopelekea kifo cha mtu mmoja ambapo Waziri Kigwangalla alipata majeraha mabaya na gari alilopanda kuharibika vibaya.
Oktoba 21 2018, wafanyakazi watano wa Wizara ya Kilimo walifariki kwa ajali ya gari wakitumia gari la Serikali, huku ikielezwa kwamba chanzo cha ajali ni mwendokasi uliozidi kiwango.
Novemba 3 2018, Watu saba waliokuwa wakisafiri katika gari STL 6250 mali ya CAG wamekufa papo hapo na wengine watatu kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na gari SU 41173 mali ya NSSF,
 
Mwezi Mei 21 2018, watu watatu walifariki kutokana na ajali ya gari mali ya kituo cha Uwekezaji(TIC) cha Tanzania, huku uchunguzi wa Polisi ukibainisha kwamba chanzo cha ajali kilitokana na mwendo kasi wa gari uliosababishwa na dereva wa gari hilo.

Julai 29 2018, gari la Wizara ya Viwanda na uwekezaji lilipata ajali wakati dereva wa gari hilo akiwakwepa watembea kwa miguu wawili. Watu wawili walifariki huku wengine kadhaa wakipatwa na majeraha.

Agosti 4 2018, Waziri wa Mali asili na Utalii Dk Khamis Kigwangalla, alipata ajali mbaya iliyopelekea kifo cha mtu mmoja ambapo Waziri Kigwangalla alipata majeraha mabaya na gari alilopanda kuharibika vibaya.
Oktoba 21 2018, wafanyakazi watano wa Wizara ya Kilimo walifariki kwa ajali ya gari wakitumia gari la Serikali, huku ikielezwa kwamba chanzo cha ajali ni mwendokasi uliozidi kiwango.
Novemba 3 2018, Watu saba waliokuwa wakisafiri katika gari STL 6250 mali ya CAG wamekufa papo hapo na wengine watatu kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na gari SU 41173 mali ya NSSF,
Hawa madereva wachunguzwe na wahakikiwe upya... tatizo walihakiki vyeti vyao bila kuhakiki ujuzi yaan practical
 
Ajali ni ajali tu boss.
Mbona ajali za magari ya serikali ni chache mno ukilinganisha na magari ya kawaida.

Msikariri kuwa wanaostahili kupata ajali ni raia wa kawaida tu.
 
Hawa wapumbavu wanajifanya huwa barabara ni zao kisa ni magari ya serikali ..wanafikiria ajali huwa zinatambua kuwa haya ni magari ya serikali na mengine sio ,acha wafe mpaka watakapo jifunza
 
Wacha wafe tu....ile mitorch ya polisi inaona gari zetu tu zinazoanza na TXX CY6......haya STL, STK, SU, PT, ZT, UT, hata foleni saa zingine hazikai na wanawapungia mikono kabisa na salute juu. Kumbe ajali haziangalii hilo......twafaaaaa
 
Wanasema, ukicheka na Nyani utakula mabua. Hili ni janga la Taifa lakini wakubwa wanalifumbia macho. Mwaka 84 nchi ilimpoteza Waziri Mkuu kwa ajili ajali za barabarani. Hapo awali ilikuwa ni raia wa kawaida, Sasa hivi ajali zimeanza kukwangua viongozi wa Serikali. Juzijuzi kakoswa waziri wa mambo ya ndani. Kama hili janga halitakuwa addressed properly, ip0 siku Taifa litapatwa na simanzi.
 
Back
Top Bottom