Ajali ya moto Msamvu inaleta picha ya udhaifu wa vyombo vya usalama

k-bee

JF-Expert Member
Aug 30, 2017
919
997
Rejea mada tajwa hapo juu.Tangu ajali itokee asubuhi Polisi na vyombo vingine vya Usalama walikuwa wapi kufika kunako tukio na kutoa elimu kwa wakaz kuto lisogelea gari hilo.

Niwakati wa serikal pia kuweka vipind katika maredio na TV kuwaelimisha hasa vijana madhara ya uwiz wa mafuta pale magari yanapoanguka na kutiririsha mafuta.....! nawapa pole wale walioguswa kwa namna moja ama nyingine na ajal hio
MAONI

VIJANA tuchape kazi tuachane na tamaa ya vitu vidogovidogo ambavyo vitaleta maafa makubwa kwenye jamii

----------------------

Maoni ya mdau Quinine

Haiwezekani tukio lidumu kwa takriban saa nzima bila jeshi la polisi kujua au kuwa na taarifa, watu wamechota wamepeleka nyumbani na kurudi polisi ilikuwa wapi.

Nina imani kama polisi ingefika mapema eneo la tukio idadi ya vifo ingepungua, ingefika na kuzuia watu wasikaribie tanki kwa kuweka uzio 'yellow tape ' au kutumia mbinu zingine na kama watu wangekaidi wangewatawanya hata kwa mabomu ya machozi.

Msamvu ni mjini na tukio lilipotokea ni hatua change kutoka kituo cha polisi na kituo cha zimamoto. Kwa mazingira ya maeneo hayo, lazima kulikuwa na polisi wa doria au polisi wa kawaida au trafiki, na naweza kusema baada ya lori kuanguka inawezekana kabisa kuna wasamalia wema walipiga simu polisi kutoa taarifa.

Nasema ni uzembe wa polisi kwa sababu, iliwezekana kabisa ndani ya dakika kumi gari la doria mitaani tunaita 'tenga' liwe imeshafika pale na polisi kulinda eneo la tukio.
 
Leo nimemkumbuka legendry Mwalusaku. Tatizo watu hatujifunzi
 
Nakuunga mkono, hapo Msamvu ni mjini, tena kwenye pale Msamvu Terminal ni karibu na kuna polisi, kama wange-react mapema, hayo maafa yasingetokea.

Vv
 
Kiasi fulani tunaweza laumu wao, maana adi watu waanze kujikusanya kuchota wangeweza fika mapema wakaweka tape..

Kiasi fulani nasi binadamu hatujifunzi ile gari tuu ikiwa inatembea teyari ni hatarishi bado tunazidi isogelea ,nafikiri ili liwe fundisho

Gari ya kusogelea ni gari ya bia tuu
 
Mnapenda kuongozwa hadi kwenye uhai wenu. Polisi waje wawaambie msichote mafuta kwani hamkujua hata kuchota hayo mafuta ni wizi. Badala ya kuokoa maisha ya waliobanwa kwenye gari nyie mnakimbilia kuiba. Mkome na muache wizi
 
Kwani hao hawana akili?hili kwani ni tukio la kwanza?kama kuna ndugu yako kapatwa na hiyo dhahma kwa kujipeleka mwenyewe usilete hasira zako kwenye vyombo vya dola.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…