Ajali mbaya kwa mbonde kibaha

Ajali mbaya kwa mbonde kibaha

Kiumbo

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2012
Posts
560
Reaction score
123
Ajali imetokea maeneo ya kwa mbonde baina ya coasta mbili za abiria jioni hii. Takribani watu zaidi 10 wamekufa palepale maiti na damu nyingh sana. Nimeshuhudia.
 
costa iliyokuwa ikitoka moro kwenda dar paa lake lote limefumulia na ndio maiti nyingi zilipotolewa na kupelekwa tumbi.nitawajuza zaidi.
 
Ni kweli.
Wanasema gari zote ni za Mlandizi-Dar. Moja ni Isuzu Journey nyeupe hivi na nyingine ni Toyota Coaster rangi ya "damu ya mzee". Moja ilikuwa inatokea Dar na nyenzake inatokea Mlandizi. Zimegongana uso kwa uso. Coaster ndiyo imefumuka zaidi.

Ni ajali mbaya kwa kweli. Ukiona hamu ya kusafiri inakatika.
 
mungu awapunzishe waliofariki na hawa onyeshe haraka walijeluhiwa..inshallah
 
Wananchi wa Tanzania wanapoteza maisha kila siku katika barabara zetu kwa sababu ya uwembamba wa barabara. Kinachosikitisha ni kwamba hakuna jitihada zinazoonekana zaidi ya kuchora nyumba kwa Alama X, za kutuepusha na dhahama hii. Naendelea kuamini kwamba tunahitaji mabadiliko ya uongozi wa kisiasa nchini. Wazee wanavurunda kwa kufanya kazi kwa mazoea na kujuana.
 
Habari ya kusikitisha hii. Nawapa pole wafiwa wote.
 
Pole sana wale wote waliofikwa na msiba Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi. Amen.
 
Wananchi wa Tanzania wanapoteza maisha kila siku katika barabara zetu kwa sababu ya uwembamba wa barabara. Kinachosikitisha ni kwamba hakuna jitihada zinazoonekana zaidi ya kuchora nyumba kwa Alama X, za kutuepusha na dhahama hii. Naendelea kuamini kwamba tunahitaji mabadiliko ya uongozi wa kisiasa nchini. Wazee wanavurunda kwa kufanya kazi kwa mazoea na kujuana.
Inasikitisha sana! Mind you, ajali hizi hazisababishwi na ufinyu wa bara bara ila tabia yetu ya kutokufuata sheria na rushwa kubwa iliyojaa kila sehemu! Hata Ulaya pamoja na kuwa na bara bara nyingi nzuri, lakini kuna zingine finyu sana na magari yanapishana ila ni nadra sana kuwa na ajali za aina hii tena magari ni mengi zaidi kuliko bongo! Ishu kubwa hapa ni sheria kufuatwa na rushwa kwa polisi wa usalama bara barani!
 
RIP. Tanroads wanatakiwa wajitathmini upya katika ujenzi wa barabara kwani kimsingi ni nyembamba mmno, lakini na sisi wenyewe madereva hatuko makini katika uendeshaji wa magari, mimi naamini pamoja na ubovu wa barabara zetu hawa jamaa wa Tanroad wameweka alama za barabarani sawia kabisa,
 
Pole kwa majeruhi, na waliotangulia mbele ya haki Mungu awarehemu.
 
Ajali imetokea maeneo ya kwa mbonde baina ya coasta mbili za abiria jioni hii. Takribani watu zaidi 10 wamekufa palepale maiti na damu nyingh sana. Nimeshuhudia.

Mwenyenzi MUNGU mwenye mamlaka Mbinguni na Duniani naomba usitusahau waja wako Mungu wangu!

Sisi ni wakosefu kila muda lakini MUNGU wangu ukaturehemu
Nakuomba MUNGU utuzidishie Malaika wako ktk ulinzi wetu Mungu wetu,NAENDA KINYUME KBS NA MWOVU SHETANI YA KWMB HANA MAMLAKA KWA WATU WAKO MUNGU WETU!
Mungu nitakutaja popote pale niwapo kwani nipo kwa mamlaka yako.

Tulinde hata wengine tuliohai muda huu kwn hakika ni Mapenzi yako ndiyo mana tupo!
Walinde hata wale wote waliokufa na wawe ktk Bwana!

MUNGU! Hata majeruhi waliopo wape nguvu na wakukumbuke MUNGU WETU! Ni hayo tu ktk jina la mwanao YESU KIRSTO aliyefia msalabani kwa ajili yetu!

Aaaaaamen!

Na wote waliotangulia mbele ya haki nasema Rest In Peace for all!
 
Wananchi wa Tanzania wanapoteza maisha kila siku katika barabara zetu kwa sababu ya uwembamba wa barabara. Kinachosikitisha ni kwamba hakuna jitihada zinazoonekana zaidi ya kuchora nyumba kwa Alama X, za kutuepusha na dhahama hii. Naendelea kuamini kwamba tunahitaji mabadiliko ya uongozi wa kisiasa nchini. Wazee wanavurunda kwa kufanya kazi kwa mazoea na kujuana.

Ni kweli barabara zetu ni nyembamba,lakini madereva wakifuata sheria tulizonazo pamoja na uwembamba wa barabara bado ajali zingepungua sana,tatizo kubwa la nchi yeyu ni utii wa sheria na wale waliopewa dhamana ya kulinda sheria wao wanakula rushwa tu hiyo ni miradi yao ya kuwatajirisha. Watanzania tujifunze kutii sheria bila kushurutishwa hakika itapunguza sana ajali za barabarani.
 
Watz tutaendelea mpaka lini kupoza maisha yetu kwa ajali za kizembe kila siku? Hatua ipi ya serikali ambayo washachukua na ikaonyesha mafanikio? Serikali yenyewe haioni imekuwa ikishindwa kwa kila kitu? Niwakati sasa wa serikali kuamua kuwaachia wenyekuweza kutuongoza watz, jk upo hapo mkuu?
 
mtangazaji wa habari hii radio one alisema 'mabasi mawili ya abiria yaliweza kugongana uso kwa uso' huwa nakereka sana na watangazaji wa aina hii, kuweza kugongana maana yake nini!!!!

kauli zingine za watangazaji wa redio ambazo hunikera ni kama na ifuatavyo:

hali ya sintofahamu
mimi kama mimi
lisaa limoja nk.
samahanikwa kutoka nje ya mada na poleni wahanga wote.
 
Jamani ni vizuri tuelezana ukweli, hizi ajali nyingi ni uzembe wa kutofuata sheria za barabarani. Pamoja na wembamba wa barabara zetu, kama kila mtumiaji wa barabara (pamoja na watembea kwa miguu) angefuata taratibu maafa mengi yasingetokea.
 
Back
Top Bottom