Ajali: Bus la Kampuni ya Frester lapata ajali

Daah hawa Madereva wa bus ni hatari sana huwa hawaoni hatari mbele yao wanakua mwendokasi na hawaogopi gari yeyote iliyo mbele yao na wana makadirio kidogo sana ukiwa na gari ndogo ni rahisi kusubiri lipite ila sio gari kubwa...inatakiwa iwepo fine kubwa kwa Bus linasobabisha ajali hata kuwalipa wahanga kama Zambia au Zimbabwe huo upuuzi utapungua sana..
 
usiku wapo njiani...asubuhi wapo njianiii yani hatari tupu
 
Naona impact haikuwa kubwa, naona matajiri wanakimbizana na pesa za mwisho wa mwaka! Jamani ee, roho za watu hazina spare! Madereva ongezeni umakini barabarani na mwendokasi siku zote unaua
 
Daah tuwe makini barabarani jama. Hali ya hewa hii barabara zinateleza wakati mwingine alama za barabarabi hazionekani vizuri
Tuna uwezo kabisa wa kuwa na njia mbili kwa barabara zote kuu zinazounganisha mikoa yote. Ni vipaumbele vya serikali tu ni vibaya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…