tzbuddy
Member
- Mar 12, 2014
- 33
- 49
Ndege moja Aina ya Caravan yenye abiria 5 na rubani mmoja,Imelazimika kutua Kwa Dharura kwenye Shamba moja Pembeni Mwa kiwanja cha Arusha . Inasemekana ndege hiyo ilipata engine Failure mara baada ya kupaa.Uchunguzi bado unaendelea kufuatana na Tukio hilo.
Pia pongezi kwa Rubani aliyeweza kuokoa maisha ya abiria Hao na ndege kwa ujumla maana haijaharibika.Wengine wenye latest wataendelea kuchangia.
=====
Watu watano wamenusurika kifo baada ya ndege waliokuwa wanasafiria kutoka katika uwanja mdogo wa Arusha kupata hitilafu kwenye injini yake muda mfupi baada ya kuruka.
Kaimu meneja wa uwanja wa ndege wa Arusha Bw, Bashiru Juma amesema ajali hiyo imetokea saa sita na dakika hamsini na tano ikiwa ni dakika tano tu baada ya kuruka ikiwa na abiria wanne na rubani mmoja ikiwa inatoka kwenye uwanja huo kwenda kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kimanjaro.
Kwa mujibu wa Bw Bashiru ajali hiyo ya ndege aina ya Caravan 5h Zeb ya kampuni ya Coastal Air haikuleta madhara na abiria wote pamoja na rubani wametoka salama na pia hakuna uharibifu wowote unaoonekana kwa macho kwenye ndege hoyo na kwamba taratibu vyombo vinavyohusika na masuala ya anga kuchunguza tukio hilo zinaendelea.
Kwa upande mtendaji wa kampuni ya hiyo ya Caoastal Air nchini Capten Dmond Julian amesema abiria walikuwa wanne wawili raia wa ujerumani na wawili raia wa italia na walikuwa walikuwa wanakwenda Zanzibar.
Chanzo: ITV