Ndugu wanajamvi ule mtandao uliojitangaza kama baba lao nadhani unaanza kuchoka.
Hawa jamaa wamebadili pakeji kama ifuatavyo:
Vifurushi Vya Siku
1. sh 399 unapata Dk 7 + 50 SMS + 20MB
2. sh 499 unapata Dk 13 + 300 SMS + 125MB
3. sh 649 unapata Dk 20 + 450SMS + 150MB
4. sh 849 unapata Dk 25 + 500SMS + 250MB
5. sh 999 unapata Dk 30 + 1000SMS + 300MB
VIfurushi Vya Mwezi:
1. sh 9999 unapewa Dk 200 + 500SMS + 500MB
2. sh 19999 unapewa Dk 450 + 1500SMS + 1Gb
3. sh 34999 unapewa Dk 800 + 2500SMS +1.5Gb
Tusubiri kule hakatwi mtu!!!!
Duh nimenunua juzi bundle imeisha cjui imeishaje
Hebu nyambulisha, hizo dakika zipi ni za off-net na zipi ni za on-net au hizo dakika unapiga mtandao wowote?????
Wakati wa Nyerere tukitaka simu za nje tunakwenda "extelecom" ukisema u book kwa simu ya nyumbani unaweza kukaa mwezi hujapata simu, na bei ya chini ilikuwa 3000 kwa dakika 3, fikiria 3,000 ya mwaka 1980 ilikuwaje.
Sasa hivi hizi bei na hata zinapopanda na kushuka kwa ushindani, kwa sisi wa zamani, bado tunaona ni neema.
Madhara ya kutowajali watu wenye kipato cha chini!!!!!!