Nilikosea kutuma pesa kiasi cha shilling 65000/-kutoka Airtel money kwenda tigo pesa ktk namba 0678984060 ambapo ilikuwa majira ya saa tisa alasiri.
Haraka haraka nikapiga simu Airtel kutoa report na kuomba msaada ili pesa izuiwe baada ya kugundua niliemtumia amezima simu.airtel wakaniambia tatizo langu limepokelewa na kwamba litafanyiwa kazi ndani ya masaa 24.masaa yalipita nikaendelea kuwapigia huku na wao wakiniambia niendelee kusubiri hatimae leo wakanipa jibu ambalo lilinistua kwamba Tigo hawajajibu taarifa yao kwa hiyo tatizo lipo Tigo.nikaona bora niwapigie tigo kupata ukweli maana danadana zimezidi.
Nimepiga Tigo naambiwa taarifa ilichelewa na kwamba pesa ilishatolewa kwa hiyo nimeambulia kupewa pole na kuambiwa Asante kwa kutumia huduma zao wananitakia siku njema hawana njia nyingine ya kunisaidia wakati huo alietoa pesa anajulikana lakini wao eti hawana njia ya kunisaidia.
Nini naweza kufanya ili kupata pesa zangu msaada please.
Haraka haraka nikapiga simu Airtel kutoa report na kuomba msaada ili pesa izuiwe baada ya kugundua niliemtumia amezima simu.airtel wakaniambia tatizo langu limepokelewa na kwamba litafanyiwa kazi ndani ya masaa 24.masaa yalipita nikaendelea kuwapigia huku na wao wakiniambia niendelee kusubiri hatimae leo wakanipa jibu ambalo lilinistua kwamba Tigo hawajajibu taarifa yao kwa hiyo tatizo lipo Tigo.nikaona bora niwapigie tigo kupata ukweli maana danadana zimezidi.
Nimepiga Tigo naambiwa taarifa ilichelewa na kwamba pesa ilishatolewa kwa hiyo nimeambulia kupewa pole na kuambiwa Asante kwa kutumia huduma zao wananitakia siku njema hawana njia nyingine ya kunisaidia wakati huo alietoa pesa anajulikana lakini wao eti hawana njia ya kunisaidia.
Nini naweza kufanya ili kupata pesa zangu msaada please.