Airtel nao wafanya yao tena

Airtel nao wafanya yao tena

barafuyamoto

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2014
Posts
32,405
Reaction score
29,802
Habari zenu,

Sijajua nafasi ya TCRA ni ipi ktk kumlinda mlaji. Naona makampuni ya simu yanafanya yatakavyo.

Airtel hatimaye na wao kifurushi cha 500 cha yatosha sasa SIO CHA MASAA 24. Kama una dk zako zimebakia ikifika saa sita usiku, ZINAPUKUTIKA.

Pia nilikuwa na dk kadhaa za yatosha ya 500 ambazo nilikuwa na carry forward kama sizitumii zote ila naona sasa HAMNA ku carry forward maana dk zangu zote nazo wamekwapua licha ya kutop up ndani ya muda.

Huu ni ukiritimba uliovuka mipaka, juzi juzi voda nao wefinya MB mpaka 1, HAIPENDEZI KABISA. Na hawa jamaa huwa wanafanya mabadiliko kwa kuambiana, Tujiandae na Tigo nao watabadili kitu si muda mrefu.
 
Ata ile MB 100 za bure za kuanzia saa 12 hadi saa 2 asubuhi NAYO WAMEISTOPISHA BILA TAARIFA..
 
tiGo jiandaeni,nyie mtaachiwa mb 2 tu!
 
Bado wanasema wanatu favor sana
 
mngojeeni m=Vietnam atawatia adabu...
 
Nakumbuka kwamba tcra walitoa agizo kwa mitandao kutenganisha vifurushi vya internet na vya kawaida(dakk na sms)
 
Tatizo ni TCRA wala sio hii mitandao.
Ni kweli.Tatizo ni TCRA.
Katika biashara huria kunatakiwa kuwa na ushindani wa makampuni ili mwisho wa siku mlaji afaidike.
Hali ilivyo sasa ni kwamba makampuni yote ya simu yanakula njama kumkamua mlaji.Ndo maana vifurushi vya makampuni yote vinafanana, bei zinapandishwa kwa wakati mmoja kwa makampuni yote na vifurushi vinapunguzwa kwa wakati mmoja.
Hili ni kosa.TCRA amkeni.
 
Duuh wapi TCRA.? Mambo kama haya yako wazi kabisa!
 
Viatel nadhani ndo watakuwa mkombozi wetu huko tuendako kama itakavyokuwa kwa Lowasa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom