AIRTEL kumjulisha adui yangu location ni kosa?

sexon2000

JF-Expert Member
Apr 18, 2010
299
65
Siku chache zilizopita nilipokea simu toka kwa mtu ninyemfahamu japokuwa si mtu mwema. Nafahamu anatafuta uhai wangu kwa siri. Kwa kujua hilo huwa akiniuliza niko wapi simwambii ukweli. Aliniuliza uko wapi, nikamwambia niko Morogoro ila nilkuwa maeneo ya Ubungo usawa wa stendi ya mkoa.

Baada ya siku mbili akanijulisha kuwa kwa nini najifanya mjanja wakati yeye amefuatilia AIRTEL wamemwambia exact location nilipokuwa. na walimpa location kwa e-mail na akaifoward kwangu, bahati mbaya akasahau kuficha adresses za wafanyakazi wa Airtel. Nikaenda airtel na kuhakiki kuwa kweli wapo na senior officers bila wao kujua kwa nini nawaulizia.

1. Je wanasheria mnanishauri nini kisheria?, nifungue kesi na ni jinai au? Damage ni kiasi gani?
2. Je Airtel maana ni sponsors wa hii JF mnasemaje katika hili?
3. Usalama wangu uko wapi kama Airtel wanaweza to taarifa za location kwa urahisi hivi?
4. Usalama wa watanzania wanaotumia AIRTEL uko wapi? wanaweza shirikiana na majambazi hawa watu

Msaada tafadhari
 
mkuu as far as I know kutoa personal information za mtu kwa mtu mwingine bila ruhusa ya muhusika ni kosa na hawaruhusiwikabisa hapo kama una ushahidi wa kutosha fungua kesi.
 
Du mkuu umeshatoka kimaisha usipuuze huu ushauri nenda fungua kesi,sheria za tcra zinasema wazi kabisa ni kosa la jinai kutoa taarifa za mteja outside unless ni ofisa wa polisi na pia isainiwe na mkuu wa teknicol au director wa acces network,pia hao watu wa airtel ukiwaambia unafungua kesi watastuka maana watapoteza kazi so unaweza ukala mpunga kwao tena,da mshikaji ushatoka kimaisha fungua kesi fungua kesi kaka,Kutoa taarifa za mteja ni bonge la kosa hata tcra wanajua hili.
 
offcourse unapaswa kuwashitaki kwa kosa la kuingilia uhuru wako binafsi unaolindwa kikatiba.haki yako imevunjwa nenda mahakamanio na ushahidi wa kutosha upate haki yako kwa mujibu wa sheria
 
Nawashukuru kwa ushauri. Nawafungulia kesi. Nitawasiliana na mwanasheria leo ili kuwafungulia kesi. Thanx JF
 
hapo hamna kitu kuna tofauti sana kati personal inormation na personal location,walichokifanya wafanyakazi wa Airtel ni kosa kwa maadili ya kazi yao lkn hakikupi wewe uhalali wa kuwashtaki.
Pia km unwindwa mpk unatishiwa kuuawa hujaripoti polisi kuna ninin hapo?
 
Wafanyakazi wa makampuni ya simu na mabenki huwa wanatoa siri binafsi za wateja wao kwa mfano mdogo wangu alikuwa na akaunti exim bank mbeya baada ya mzee kukuta risiti ya kudeposit cash alikwenda moja kwa moja exim bank tawi la mwanjelwa mbeya wakampatia salio lililopo kwenye akaunti na siku ya mwisho alipo deposit cash, pili tigo kuna ndugu yangu girlfriend wake alikuwa anasumbuliwa sana na jamaa mmoja akaenda tigo jamaa wakampa full detail za jamaa pamoja na muda ambao jamaa alikuwa anapiga simu.
 
Wafanyakazi wa makampuni ya simu na mabenki huwa wanatoa siri binafsi za wateja wao kwa mfano mdogo wangu alikuwa na akaunti exim bank mbeya baada ya mzee kukuta risiti ya kudeposit cash alikwenda moja kwa moja exim bank tawi la mwanjelwa mbeya wakampatia salio lililopo kwenye akaunti na siku ya mwisho alipo deposit cash, pili tigo kuna ndugu yangu girlfriend wake alikuwa anasumbuliwa sana na jamaa mmoja akaenda tigo jamaa wakampa full detail za jamaa pamoja na muda ambao jamaa alikuwa anapiga simu.
:
:
walimpa hivihivi tu? be clear
 
ni kweli wamekosea tena sana, ila tunakoelekea sio kuzuri. mwachie mtikila hii tabia
 
Back
Top Bottom